< בראשית 10 >

ואלה תולדת בני נח שם חם ויפת ויולדו להם בנים אחר המבול 1
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
בני יפת--גמר ומגוג ומדי ויון ותבל ומשך ותירס 2
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
ובני גמר--אשכנז וריפת ותגרמה 3
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
ובני יון אלישה ותרשיש כתים ודדנים 4
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
מאלה נפרדו איי הגוים בארצתם איש ללשנו--למשפחתם בגויהם 5
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
ובני חם--כוש ומצרים ופוט וכנען 6
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
ובני כוש--סבא וחוילה וסבתה ורעמה וסבתכא ובני רעמה שבא ודדן 7
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
וכוש ילד את נמרד הוא החל להיות גבר בארץ 8
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
הוא היה גבר ציד לפני יהוה על כן יאמר כנמרד גבור ציד לפני יהוה 9
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
ותהי ראשית ממלכתו בבל וארך ואכד וכלנה בארץ שנער 10
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
מן הארץ ההוא יצא אשור ויבן את נינוה ואת רחבת עיר ואת כלח 11
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
ואת רסן בין נינוה ובין כלח--הוא העיר הגדלה 12
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
ומצרים ילד את לודים ואת ענמים ואת להבים--ואת נפתחים 13
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
ואת פתרסים ואת כסלחים אשר יצאו משם פלשתים--ואת כפתרים 14
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
וכנען ילד את צידן בכרו--ואת חת 15
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
ואת היבוסי ואת האמרי ואת הגרגשי 16
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
ואת החוי ואת הערקי ואת הסיני 17
Wahivi, Waariki, Wasini,
ואת הארודי ואת הצמרי ואת החמתי ואחר נפצו משפחות הכנעני 18
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
ויהי גבול הכנעני מצידן--באכה גררה עד עזה באכה סדמה ועמרה ואדמה וצבים--עד לשע 19
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
אלה בני חם למשפחתם ללשנתם בארצתם בגויהם 20
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
ולשם ילד גם הוא אבי כל בני עבר--אחי יפת הגדול 21
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
בני שם עילם ואשור וארפכשד ולוד וארם 22
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
ובני ארם--עוץ וחול וגתר ומש 23
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
וארפכשד ילד את שלח ושלח ילד את עבר 24
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
ולעבר ילד שני בנים שם האחד פלג כי בימיו נפלגה הארץ ושם אחיו יקטן 25
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
ויקטן ילד את אלמודד ואת שלף ואת חצרמות ואת ירח 26
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
ואת הדורם ואת אוזל ואת דקלה 27
Hadoramu, Uzali, Dikla,
ואת עובל ואת אבימאל ואת שבא 28
Obali, Abimaeli, Sheba,
ואת אופר ואת חוילה ואת יובב כל אלה בני יקטן 29
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
ויהי מושבם ממשא באכה ספרה הר הקדם 30
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
אלה בני שם למשפחתם ללשנתם בארצתם לגויהם 31
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
אלה משפחת בני נח לתולדתם בגויהם ומאלה נפרדו הגוים בארץ--אחר המבול 32
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< בראשית 10 >