< דברי הימים א 2 >

אלה בני ישראל ראובן שמעון לוי ויהודה יששכר וזבלון 1
Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni,
דן יוסף ובנימן נפתלי גד ואשר 2
Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
בני יהודה ער ואונן ושלה--שלושה נולד לו מבת שוע הכנענית ויהי ער בכור יהודה רע בעיני יהוה--וימיתהו 3
Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
ותמר כלתו ילדה לו את פרץ ואת זרח כל בני יהודה חמשה 4
Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
בני פרץ חצרון וחמול 5
Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
ובני זרח זמרי ואיתן והימן וכלכל ודרע--כלם חמשה 6
Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
ובני כרמי--עכר עוכר ישראל אשר מעל בחרם 7
Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
ובני איתן עזריה 8
Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
ובני חצרון אשר נולד לו--את ירחמאל ואת רם ואת כלובי 9
Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
ורם הוליד את עמינדב ועמינדב הוליד את נחשון נשיא בני יהודה 10
Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
ונחשון הוליד את שלמא ושלמא הוליד את בעז 11
Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
ובעז הוליד את עובד ועובד הוליד את ישי 12
Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
ואישי הוליד את בכרו את אליאב--ואבינדב השני ושמעא השלשי 13
Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
נתנאל הרביעי רדי החמישי 14
wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
אצם הששי דויד השבעי 15
wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
ואחיתיהם צרויה ואביגיל ובני צרויה אבשי ויואב ועשהאל--שלשה 16
Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
ואביגיל ילדה את עמשא ואבי עמשא יתר הישמעאלי 17
Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
וכלב בן חצרון הוליד את עזובה אשה--ואת יריעות ואלה בניה ישר ושובב וארדון 18
Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni.
ותמת עזובה ויקח לו כלב את אפרת ותלד לו את חור 19
Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri.
וחור הוליד את אורי ואורי הוליד את בצלאל 20
Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.
ואחר בא חצרון אל בת מכיר אבי גלעד והוא לקחה והוא בן ששים שנה ותלד לו את שגוב 21
Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu.
ושגוב הוליד את יאיר ויהי לו עשרים ושלוש ערים בארץ הגלעד 22
Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi.
ויקח גשור וארם את חות יאיר מאתם את קנת ואת בנתיה--ששים עיר כל אלה בני מכיר אבי גלעד 23
(Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.
ואחר מות חצרון בכלב אפרתה ואשת חצרון אביה ותלד לו את אשחור אבי תקוע 24
Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.
ויהיו בני ירחמאל בכור חצרון הבכור רם ובונה וארן ואצם אחיה 25
Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
ותהי אשה אחרת לירחמאל ושמה עטרה היא אם אונם 26
Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
ויהיו בני רם בכור ירחמאל--מעץ וימין ועקר 27
Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
ויהיו בני אונם שמי וידע ובני שמי נדב ואבישור 28
Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
ושם אשת אבישור אביהיל ותלד לו את אחבן ואת מוליד 29
Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
ובני נדב סלד ואפים וימת סלד לא בנים 30
Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
ובני אפים ישעי ובני ישעי ששן ובני ששן אחלי 31
Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
ובני ידע אחי שמי יתר ויונתן וימת יתר לא בנים 32
Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
ובני יונתן פלת וזזא אלה היו בני ירחמאל 33
Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
ולא היה לששן בנים כי אם בנות ולששן עבד מצרי ושמו ירחע 34
Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
ויתן ששן את בתו לירחע עבדו לאשה ותלד לו את עתי 35
Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
ועתי הליד את נתן ונתן הוליד את זבד 36
Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
וזבד הוליד את אפלל ואפלל הוליד את עובד 37
Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
ועובד הוליד את יהוא ויהוא הליד את עזריה 38
Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
ועזריה הליד את חלץ וחלץ הליד את אלעשה 39
Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
ואלעשה הליד את ססמי וססמי הליד את שלום 40
Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
ושלום הוליד את יקמיה ויקמיה הליד את אלישמע 41
Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
ובני כלב אחי ירחמאל מישע בכרו הוא אבי זיף ובני מרשה אבי חברון 42
Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.
ובני חברון--קרח ותפח ורקם ושמע 43
Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.
ושמע הוליד את רחם אבי ירקעם ורקם הוליד את שמי 44
Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai.
ובן שמי מעון ומעון אבי בית צור 45
Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.
ועיפה פילגש כלב ילדה את חרן ואת מוצא ואת גזז וחרן הליד את גזז 46
Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.
ובני יהדי--רגם ויותם וגישן ופלט ועיפה ושעף 47
Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.
פילגש כלב מעכה ילד שבר ואת תרחנה 48
Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana.
ותלד שעף אבי מדמנה את שוא אבי מכבנה ואבי גבעא ובת כלב עכסה 49
Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa.
אלה היו בני כלב בן חור בכור אפרתה--שובל אבי קרית יערים 50
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu,
שלמא אבי בית לחם חרף אבי בית גדר 51
Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.
ויהיו בנים לשובל אבי קרית יערים הראה חצי המנחות 52
Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi,
ומשפחות קרית יערים--היתרי והפותי והשמתי והמשרעי מאלה יצאו הצרעתי--והאשתאלי 53
pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.
בני שלמא בית לחם ונטופתי עטרות בית יואב וחצי המנחתי הצרעי 54
Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori,
ומשפחות ספרים ישבו (ישבי) יעבץ תרעתים שמעתים שוכתים המה הקינים הבאים מחמת אבי בית רכב 55
pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.

< דברי הימים א 2 >