< Job 29 >

1 Darauf fuhr Hiob also fort, seine Rede vorzutragen:
Ayubu akaendelea na kusema,
2 O daß ich wäre wie in früheren Monden, wie in den Tagen da mich Gott beschützte;
Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
3 als seine Leuchte über meinem Haupte schien, und ich bei seinem Licht durch Dunkel wandelte,
taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
4 so, wie ich war in meines Sommers Tagen, als Gottes Freundschaft über meinem Zelte waltete,
Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
5 als der Allmächtige noch mit mir war, rings um mich meine Knaben;
wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
6 als ich meine Schritte in Dickmilch badete, und der Fels neben mir Bäche Öls ergoß;
wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
7 als ich zum Thore ging hinauf zur Stadt, auf dem freien Platze meinen Sitz aufschlug.
Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
8 Wenn mich die Knaben sahen, verbargen sie sich, und die Greise erhoben sich und blieben stehn;
vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
9 Häuptlinge hielten inne mit Reden und legten die Hand auf ihren Mund.
Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
10 Der Edlen Stimme verbarg sich, und ihre Zunge klebte an ihrem Gaumen.
Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
11 Denn wo ein Ohr nur hörte, da pries es mich selig, und wo ein Auge sah, da gab es mir Zeugnis.
Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
12 Denn ich rettete den Elenden, der um Hilfe schrie, und die Waise und den, der keinen Helfer hatte.
kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
13 Der Segen des Verlorenen kam über mich, und das Herz der Witwe macht ich jubeln.
Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
14 Gerechtigkeit zog ich an, und sie zog mich an, wie Talar und Turban zog ich an meine Rechtschaffenheit.
Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
15 Auge ward ich dem Blinden und Fuß war ich dem Lahmen.
Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
16 Ein Vater war ich den Armen und die Rechtssache des mir Unbekannten untersuchte ich;
Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
17 ich zerschmetterte dem Frevler die Kinnladen und warf ihm die Beute aus den Zähnen.
Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
18 So dachte ich denn: “Bei meinem Neste werde ich verscheiden und wie der Phönix meine Tage mehren.
Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
19 Meine Wurzel steht über dem Wasser offen, und der Tau übernachtet in meinen Zweigen.
Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
20 Meine Würde ist stets neu bei mir, und mein Bogen verjüngt sich in meiner Hand.”
Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
21 Mir hörten sie zu und warteten und lauschten schweigend meinem Rate.
Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
22 Wenn ich geredet, sprachen sie nicht mehr, und meine Rede troff auf sie herab.
Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
23 So warteten sie auf mich wie auf Regen und wie nach Spätregen sperrten sie den Mund auf.
Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
24 Ich lächelte ihnen zu, wenn sie verzagten, und das heitre Antlitz trübten sie mir nie.
Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
25 Gern wählte ich den Weg zu ihnen, saß da als Haupt und thronte wie ein König in der Heerschar, wie einer, der Trauernde tröstet.
Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.

< Job 29 >