< Job 28 >

1 Wohl giebt es einen Fundort für das Silber, eine Stätte für das Gold, das man läutert.
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
2 Eisen wird aus dem Erdreiche geholt, und Gestein schmilzt man zu Erz.
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
3 Ein Ende hat man der Finsternis gemacht und bis zur äußersten Grenze durchforscht man das im tiefsten Dunkel verborgene Gestein.
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
4 Man bricht einen Schacht fern von den droben Wohnenden; vergessen von dem droben schreitenden Fuß, fern von den Menschen hangen, schweben sie.
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
5 Aus der Erde geht Brotkorn hervor, und ihr Tiefen werden wie mit Feuer umgewühlt.
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
6 Des Saphirs Fundstätte ist ihr Gestein, Goldstäubchen werden ihm zu teil.
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
7 Den Weg kennt nicht der Adler, noch erspäht ihn des Geiers Auge.
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
8 Nicht betreten ihn die stolzen Raubtiere, noch schreitet auf ihm der Leu.
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
9 An den Kiesel legt man die Hand, wühlt von Grund aus die Berge um.
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
10 Durch die Felsen schlägt man Gänge, und allerlei Kostbares erschaut das Auge.
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
11 Die Wasseradern verbindet man, daß sie nicht thränen, und bringt Verborgenes ans Licht.
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
12 Die Weisheit aber, wo findet man sie, und wo ist der Fundort der Erkenntnis?
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
13 Kein Mensch kennt den Weg zu ihr, und sie ist nicht zu finden im Lande der Lebendigen.
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
14 Die Meerestiefe spricht: “In mir ist sie nicht!” und das Meer spricht: “Sie ist nicht bei mir!”
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
15 Mit gediegenem Golde wird sie nicht erkauft, noch wird Silber dargewogen als ihr Preis.
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
16 Sie läßt sich nicht aufwiegen mit Ophirgold, mit kostbarem Schoham und Sapphir.
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
17 Gold und Glas kommen ihr nicht gleich, noch tauscht man sie ein für güldenes Geschirr.
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
18 Korallen und Krystall kommen nicht in Betracht, und der Besitz der Weisheit geht über Perlen.
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
19 Äthiopiens Topas kommt ihr nicht gleich, mit reinstem Golde wird sie nicht aufgewogen.
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
20 Die Weisheit also - woher kommt sie, und wo ist der Fundort der Erkenntnis?
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
21 Verhüllt ist sie vor den Augen aller Lebenden, auch den Vögeln unter dem Himmel ist sie verborgen.
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
22 Abgrund und Tod sprechen: “Wir haben mit unseren Ohren ein Gerücht von ihr gehört.”
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
23 Gott kennt den Weg zu ihr und er weiß um ihren Fundort.
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
24 Denn er schaut bis zu der Erde Enden; was irgend unter dem Himmel ist, sieht er.
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
25 Als er des Windes Wucht abwog und dem Wasser sein Maß bestimmte,
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
26 als er dem Regen sein Gesetz gab, und seinen Pfad dem Wasserstrahle,
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
27 da sah er sie und machte sie kund, stellte sie hin und durchforschte sie.
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
28 Und zum Menschen sprach er: Siehe, Furcht des Herrn, das ist Weisheit, und das Böse meiden, ist Verstand!
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”

< Job 28 >