< Psalm 30 >

1 Ein Lied. Ein Gesang zur Tempelweihe. Von David. Erheben will ich Dich, wenn Du mich aus der Tiefe zögest, Herr, und wenn Du meine Feinde über mich nicht jubeln ließest.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Ich rufe, Herr, mein Gott, zu Dir, Du mögest Heil mir schenken.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Der Unterwelt entziehe mich! Mein Leben rette, Herr, aus denen, die zur Grube fahren. - (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Lobsingt dem Herrn, ihr seine Frommen! Lobpreiset seinen heiligen Namen!
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 Sein Zorn währt einen Augenblick, ein Leben seine Huld. Und kehrt am Abend Weinen ein, am Morgen ist schon Jubel da.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Ich sage ganz getrost und zweifle nie daran:
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 "Du, Herr, in Deiner Huld, Du stehst mir da als fester Berg; verhüllest Du jedoch Dein Angesicht, dann packt mich Grauen." -
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Ich rufe, Herr, zu Dir; zu meinem Herren flehe ich:
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 Was nützt Dir mein Verstummen, wenn ich hinab zur Grube stiege? Kann Dich ein Stäubchen preisen und Deine Treue künden?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Herr! Höre! Sei mir gnädig! Sei mir ein Helfer, Herr!
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Verwandle Du in Reigen meine Trauer! Befrei mich von dem Bußgewand! Umgürte mich mit Freude!
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 Dann singt ein lebend Wesen Dir und wird nie still. Dann preise ich Dich, Herr, mein Gott, auf immer.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Psalm 30 >