< Psaumes 75 >

1 Psaume d'Asaph, Cantique [donné] au maître chantre, [pour le chanter] sur Altasheth. Ô Dieu! nous t'avons célébré; nous t'avons célébré; et ton Nom était près de nous; on a raconté tes merveilles.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Quand j'aurai accepté l'assignation, je jugerai droitement.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Le pays s'écoulait avec tous ceux qui y habitent; mais j'ai affermi ses piliers; (Sélah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 J'ai dit aux insensés: n'agissez point follement; et aux méchants: ne faites point les superbes.
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 N'affectez point la domination, et ne parlez point avec fierté.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 Car l'élévation ne vient point d'Orient, ni d'Occident, ni du désert.
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 Car c'est Dieu qui gouverne; il abaisse l'un, et élève l'autre.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Même il y a une coupe en la main de l'Eternel, et le vin rougit dedans; il est plein de mixtion, et [Dieu] en verse; certainement tous les méchants de la terre en suceront et boiront les lies.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Mais moi, j'en ferai le récit à toujours, je psalmodierai au Dieu de Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 J'humilierai tous les méchants; mais les justes seront élevés.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psaumes 75 >