< Ézéchiel 14 >

1 Or quelques-uns des Anciens d'Israël vinrent vers moi, et s'assirent devant moi.
Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
2 Et la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
3 Fils d'homme, ces gens-ci ont posé leurs idoles dans leurs cœurs, et ont mis devant leur face l'achoppement de leur iniquité; serais-je recherché d'eux sérieusement?
“Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
4 C'est pourquoi parle-leur, et leur dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel. Quiconque de la maison d'Israël aura posé ses idoles dans son cœur, et aura mis devant sa face l'achoppement de son iniquité, et viendra vers le Prophète, Je [suis] l'Eternel, je lui ai répondu [tout] ce que je lui veux répondre, [puisqu'il] vient avec la multitude de ses idoles.
Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
5 Afin que je prenne la maison d'Israël par leur propre cœur, car eux tous se sont éloignés de moi par leurs idoles.
Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
6 C'est pourquoi dis à la maison d'Israël: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel, convertissez-vous, et faites qu'on se retire de vos idoles, et détournez-vous de toutes vos abominations.
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
7 Car quiconque de la maison d'Israël, ou des étrangers qui séjournent en Israël, se sera séparé de moi, et aura posé ses idoles dans son cœur, et mis l'achoppement de son iniquité devant sa face, s'il vient vers le Prophète pour m'interroger par lui, je suis l'Eternel, on lui a répondu tout ce qu'on a à lui répondre de ma part.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
8 Et je me tournerai contre cet homme, et je le ferai servir de signe, et de jouet, et je le retrancherai du milieu de mon peuple; et vous saurez que je [suis] l'Eternel.
Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
9 Et s'il arrive que le Prophète soit séduit, et qu'il profère quelque parole, moi l'Eternel j'aurai séduit ce Prophète-là, et j'étendrai ma main sur lui, et je l'exterminerai du milieu de mon peuple d'Israël;
“‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
10 Et ils porteront la peine de leur iniquité; la peine de l'iniquité du Prophète sera toute telle que la peine de celui qui l'aura interrogé;
Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
11 Afin que la maison d'Israël ne s'éloigne plus de moi, et qu'ils ne se souillent plus par tous leurs crimes; alors ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu, dit le Seigneur l'Eternel.
“‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
12 Puis la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema,
13 Fils d'homme, lorsqu'un pays aura péché contre moi, en commettant une infidélité, et que j'aurai étendu ma main contre lui, et que je lui aurai rompu le bâton du pain, et envoyé la famine, et retranché du milieu de lui tant les hommes que les bêtes;
“Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
14 Et que ces trois hommes, Noé, Daniel et Job, y seraient, ils délivreraient leurs âmes par leur justice, dit le Seigneur l'Eternel.
hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
15 Si je fais passer les mauvaises bêtes par ce pays-là, et qu'elles le désolent, tellement que ce [ne] soit [que] désolation, sans qu'il y ait personne qui [y] passe à cause des bêtes;
“Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
16 [Et] que ces trois hommes-là s'y trouvent; je suis vivant, dit le Seigneur l'Eternel, qu'ils ne délivreront ni fils ni filles, eux seulement seront délivrés, et le pays [ne] sera [que] désolation.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
17 Ou si je fais venir l'épée sur ce pays-là, et si je dis: que l'épée passe par le pays, et qu'elle en retranche les hommes et les bêtes;
“Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
18 Si ces trois hommes-là se trouvent au milieu du pays, je suis vivant, dit le Seigneur l'Eternel, qu'ils ne délivreront ni fils, ni filles; mais eux seulement seront délivrés.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19 Ou [si] j'envoie la mortalité sur ce pays-là, et que je répande ma colère contre lui, jusques à faire ruisseler le sang, tellement que je retranche du milieu de lui les hommes et les bêtes;
“Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
20 Et que Noé, Daniel et Job s'y trouvent, je [suis] vivant, dit le Seigneur l'Eternel, qu'ils ne délivreront ni fils ni filles; [mais] ils délivreront leurs âmes par leur justice.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
21 Car ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: combien plus quand j'aurai envoyé mes quatre plaies mortelles, l'épée, et la famine, et les bêtes nuisibles, et la mortalité, contre Jérusalem, pour en retrancher les hommes et les bêtes?
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
22 Et toutefois, voici, quelques réchappés y demeureront de reste, [savoir] ceux qu'on s'en va faire sortir, et fils et filles; voici, ils viennent vers vous, et vous verrez leur train [de vie], et leurs actions, et vous serez satisfaits du mal que j'aurai fait venir contre Jérusalem, et de tout ce que j'aurai fait venir sur elle.
Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
23 Vous en serez, dis-je, satisfaits, lorsque vous aurez vu leur train [de vie], et leurs actions; et vous connaîtrez que je n'aurai point exécuté sans cause tout ce que j'aurai fait en elle, dit le Seigneur l'Eternel.
Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 14 >