< Ézéchiel 13 >

1 La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils d'homme, prophétise contre les Prophètes d'Israël qui [se mêlent] de prophétiser, et dis à ces Prophètes qui prophétisent de leur propre mouvement: écoutez la parole de l'Eternel.
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
3 Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: malheur aux Prophètes insensés qui suivent leur propre esprit, et qui n'ont point eu de vision.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
4 Israël, tes Prophètes ont été comme des renards dans les déserts.
Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
5 Vous n'êtes point montés aux brèches, et vous n'avez point refait les cloisons pour la maison d'Israël, afin de vous trouver au combat à la journée de l'Eternel.
Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
6 Ils ont eu des visions de vanité, et des divinations de mensonge, en disant: l'Eternel a dit; et toutefois l'Eternel ne les avait point envoyés; et ils ont fait espérer que leur parole serait accomplie.
Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
7 N'avez-vous pas vu des visions de vanité, et prononcé des divinations de mensonge? cependant vous dites: l'Eternel a parlé; et je n'ai point parlé.
Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
8 C'est pourquoi ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: parce que vous avez prononcé la vanité, et que vous avez eu des visions de mensonge, à cause de cela j'en [veux] à vous, dit le Seigneur l'Eternel.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
9 Et ma main sera sur les Prophètes qui ont des visions de vanité, et des divinations de mensonge; ils ne seront plus [admis] dans le conseil de mon peuple, ils ne seront plus écrits dans les registres de la maison d'Israël, ils n'entreront plus en la terre d'Israël; et vous saurez que je suis le Seigneur l'Eternel.
Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
10 Parce, oui parce qu'ils ont abusé mon peuple, en disant: Paix! et [il] n'[y avait] point de paix. L'un bâtissait la paroi, et les autres l'enduisaient de mortier mal lié.
“‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
11 Dis à ceux qui enduisent [la paroi] de mortier mal lié, qu'elle tombera; il y aura une pluie débordée, et vous, pierres de grêle, vous tomberez [sur elle], et un vent de tempête la fendra.
kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
12 Et voici, la paroi est tombée; ne vous sera-t-il donc pas dit: où [est] l'enduit dont vous l'avez enduite?
Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
13 C'est pourquoi ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: je ferai éclater en ma fureur un vent impétueux, et il y aura une pluie débordée en ma colère, et des pierres de grêle en [ma] fureur pour détruire entièrement.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
14 Et je démolirai la paroi que vous avez enduite de mortier mal lié, je la jetterai par terre, tellement que son fondement sera découvert, et elle tombera; vous serez consumés au milieu d'elle, et vous saurez que je suis l'Eternel.
Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
15 Ainsi je consommerai ma colère contre la paroi, et contre ceux qui l'enduisent de mortier mal lié; et je vous dirai: la paroi n'est plus, ni ceux qui l'ont enduite;
Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
16 [Savoir] les Prophètes d'Israël, qui prophétisent touchant Jérusalem, et qui voient pour elle des visions de paix; et néanmoins il n'y a point de paix, dit le Seigneur l'Eternel.
wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
17 Aussi, toi fils d'homme, tourne ta face contre les filles de ton peuple qui prophétisent de leur propre mouvement, et prophétise contre elles.
“Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
18 Et dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: malheur à celles qui cousent des coussins pour s'accouder le long du bras jusques aux mains, et qui font des voiles [pour mettre] sur la tête des personnes de toute taille, pour séduire les âmes. Séduiriez-vous les âmes de mon peuple; et vous garantiriez-vous [vos] âmes?
na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
19 Et me profaneriez-vous envers mon peuple pour des poignées d'orge, et pour des pièces de pain en faisant mourir les âmes qui ne devaient point mourir, et faisant vivre les âmes qui ne devaient point vivre, en mentant à mon peuple qui écoute le mensonge?
Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
20 C'est pourquoi ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici, j'en [veux] à vos coussins, par lesquels vous séduisez les âmes pour les faire voler [vers vous]; et je déchirerai ces [coussins] de vos bras, et je ferai échapper les âmes que vous avez attirées afin qu'elles volent [vers vous].
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
21 Je déchirerai aussi vos voiles, et je délivrerai mon peuple d'entre vos mains, et ils ne seront plus entre vos mains pour en faire votre chasse; et vous saurez que je suis l'Eternel.
Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
22 Parce que vous avez affligé sans sujet le cœur du juste, lequel je ne contristais point, et que vous avez renforcé les mains du méchant, afin qu'il ne se détournât point de son mauvais train, [et] que je lui sauvasse la vie.
Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
23 C'est pourquoi vous n'aurez plus aucune vision de vanité, ni aucune divination, mais je délivrerai mon peuple d'entre vos mains; et vous saurez que je suis l'Eternel.
kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”

< Ézéchiel 13 >