< 1 Chroniques 7 >

1 Et les enfants d'Issacar, furent ces quatre Tolah, Puah, Jasub et Simron.
Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
2 Et les enfants de Tolah furent Huzi, Réphaja, Jériel, Jahmaï, Jibsam, et Samuël; chefs des maisons de leurs pères qui étaient de Tolah; gens forts et vaillants en leurs générations. Le compte qui en fut fait aux jours de David fut de vingt-deux mille six cents.
Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
3 Les enfants de Huzi, Jizrahia; et les enfants de Jizrahia, Micaël, Hobadia, Joël, et Jiscija, en tout cinq chefs.
Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
4 Et avec eux, suivant leurs générations, et selon les familles de leurs pères, [il y eut] en troupes de gens de guerre trente-six mille hommes; car ils eurent plusieurs femmes et plusieurs enfants.
Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
5 Et leurs frères selon toutes les familles d'Issacar, hommes forts et vaillants, étant comptés tous selon leur généalogie, furent quatre-vingt et sept mille.
Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
6 [Les enfants] de Benjamin furent trois, Bélah, Béker, et Jédihaël.
Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
7 Et les enfants de Bélah furent, Etsbon, Huzi, Huziël, Jérimoth, et Hiri; cinq chefs des familles des pères, hommes forts et vaillants; et leur dénombrement selon leur généalogie monta à vingt-deux mille et trente-quatre.
Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
8 Et les enfants de Béker [furent], Zemira, Joas, Elihézer, Eliohenaï, Homri, Jérimoth, Abija, Hanathoth, et Halemeth; tous ceux-là furent enfants de Béker.
Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
9 Et leur dénombrement selon leur généalogie, selon leurs générations, [et] les chefs des familles de leurs pères, monta à vingt mille deux cents hommes, forts et vaillants.
Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
10 Et Jédihaël eut pour fils Bilhan. Et les enfants de Bilhan furent, Jéhus, Benjamin, Ehud, Kénahana, Zethan, Tarsis, et Ahisahar.
Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
11 Tous ceux-là furent enfants de Jédihaël, selon les chefs [des familles] des pères, forts et vaillants, dix-sept mille deux cents hommes, marchant en bataille.
Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
12 Suppim et Huppim furent enfants de Hir; et Husim fut fils d'Aher.
Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
13 Les enfants de Nephthali furent Jahtsiël, Guni, Jetser, et Sallum, [petits-] fils de Bilha.
Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
14 Les enfants de Manassé, Asriël, que [la femme de Galaad] enfanta. Or la concubine Syrienne de Manassé avait enfanté Makir père de Galaad.
Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
15 Et Makir prit une femme de la parenté de Huppim et de Suppim; car ils avaient une sœur nommée Mahaca. Et le nom d'un des petits-fils de Galaad fut Tselophcad; et Tselophcad n'eut que des filles.
Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
16 Et Mahaca, femme de Makir, enfanta un fils et l'appela Pérés, et le nom de son frère Serés, dont les enfants furent, Ulam et Rékem.
Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
17 Et le fils d'Ulam fut Bedan. Ce sont là les enfants de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé.
Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
18 Mais sa sœur Moleketh enfanta Ishud, Abihézer, et Mahla.
Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
19 Et les enfants de Semidah furent, Ahiam, Sekem, Likhi, et Aniham.
Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
20 Or les enfants d'Ephraïm furent, Sutelah; Béred son fils, Tahath son fils, Elhada son fils, Tahath son fils.
Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
21 Zabad son fils, Sutelah son fils, et Hézer, et Elhad. Mais ceux de Gad, nés au pays, les mirent à mort, parce qu'ils étaient descendus pour prendre leur bétail.
Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
22 Et Ephraïm leur père [en] mena deuil plusieurs jours; et ses frères vinrent pour le consoler.
Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
23 Puis il vint vers sa femme, qui conçut, et enfanta un fils; et elle l'appela Bériha, parce qu'[il fut conçu] dans l'affliction arrivée en sa maison.
Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
24 Et sa fille Séera, qui bâtit la basse et la haute Beth-horon, et Uzen-Séera.
Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
25 Son fils fut Repha, puis Reseph, et Telah son fils, Tahan son fils,
Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
26 Lahdan son fils, Hammihud son fils, Elisamah son fils,
Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
27 Nun son fils, Josué son fils.
Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
28 Leur possession et habitation fut Béthel, avec les villes de son ressort, et du côté d'Orient, Naharan; et du côté d'Occident, Guézer, avec les villes de son ressort, et Sichem, avec les villes de son ressort, jusqu'à Haza, avec les villes de son ressort.
Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
29 Et dans les lieux qui étaient aux enfants de Manassé, Bethséan, avec les villes de son ressort, Tahanac, avec les villes de son ressort, Méguiddo, avec les villes de son ressort, Dor, avec les villes de son ressort. Les enfants de Joseph, fils d'Israël, habitèrent dans ces villes.
Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
30 Les enfants d'Aser furent, Jimna, Jisua, Isaï, Bériha, et Sérah leur sœur.
Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
31 Et les enfants de Bériha furent, Héber, et Malkiël, qui fut père de Birzavith.
Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
32 Et Héber engendra Japhlet, Somer, Hotham, et Suah leur sœur.
Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
33 Les enfants de Japhlet furent Pasah, Bimhal, et Hasvath. Ce sont là les enfants de Japhlet.
Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
34 Et les enfants de Semer furent Ahi, Rohega, Jéhubba, et Aram.
Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
35 Et les enfants d'Hélem son frère furent, Tsophah, Jimnah, Sellés, et Hamal.
Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
36 Les enfants de Tsophah furent Suah, Harnepher, Suhal, Béri, Jimra,
Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
37 Betser, Hod, Samma, Silsa, Jithran, et Béera.
Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
38 Et les enfants de Jéther furent, Jephunné, Pispa, et Ara.
Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
39 Et les enfants de Hulla furent, Arah, Hanniël, et Ritsia.
Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
40 Tous ceux-là furent enfants d'Aser, chefs des maisons des pères, gens d'élite, forts et vaillants, chefs des principaux, et leur dénombrement selon leur généalogie, qui fut fait quand on s'assemblait pour aller à la guerre, fut de vingt-six mille hommes.
Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.

< 1 Chroniques 7 >