< 2 Rois 1 >

1 Or après la mort d'Achab Moab se rebella contre Israël.
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
2 Et Achazia tomba par le treillis de sa chambre haute qui était à Samarie, et en fut malade; et il envoya des messagers, et leur dit: Allez consulter Bahal-zébub, dieu de Hékron, [pour savoir] si je relèverai de cette maladie.
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
3 Mais l'Ange de l'Eternel parla à Elie Tisbite, en disant: Lève-toi, monte au devant des messagers du Roi de Samarie, et leur dis: N'y [a-t-il] point de Dieu en Israël, que vous alliez consulter Bahal-zébub, dieu de Hékron?
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
4 C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel: Tu ne descendras point du lit sur lequel tu es monté, mais certainement tu mourras. Cela dit, Elie s'en alla.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
5 Et les messagers s'en retournèrent vers Achazia, et il leur dit: Pourquoi êtes-vous revenus?
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
6 Et ils lui répondirent: Un homme est monté au-devant de nous, qui nous a dit: Allez, retournez vous-en vers le Roi qui vous a envoyés, et dites-lui: Ainsi a dit l'Eternel: N'y a-t-il point de Dieu en Israël, que tu envoies consulter Bahal-zébub dieu de Hékron? A cause de cela tu ne descendras point du lit sur lequel tu es monté, mais certainement tu mourras.
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
7 Et il leur dit: Comment était fait cet homme qui est monté au devant de vous, et qui vous a dit ces paroles?
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
8 Et ils lui répondirent: C'est un homme vêtu de poil, qui a une ceinture de cuir, ceinte sur ses reins; et il dit: C'est Elie Tisbite.
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
9 Alors il envoya vers lui un capitaine de cinquante hommes, avec sa cinquantaine, lequel monta vers lui. Or voilà, il se tenait au sommet d'une montagne, et [ce capitaine] lui dit: Homme de Dieu, le Roi a dit que tu aies à descendre.
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
10 Mais Elie répondit, et dit au capitaine de la cinquantaine: Si je suis un homme de Dieu, que le feu descende des cieux, et te consume, toi et ta cinquantaine! Et le feu descendit des cieux, et le consuma, lui et sa cinquantaine.
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
11 Et [Achazia] envoya encore un autre capitaine de cinquante hommes avec sa cinquantaine, qui prit la parole, et lui dit: Homme de Dieu, ainsi a dit le Roi: Hâte-toi de descendre.
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
12 Mais Elie répondit, et leur dit: Si je suis un homme de Dieu, que le feu descende des cieux et te consume, toi et ta cinquantaine; et le feu de Dieu descendit des cieux, et le consuma, lui et sa cinquantaine.
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
13 Et [Achazia] envoya encore un capitaine d'une troisième cinquantaine avec sa cinquantaine, et ce troisième capitaine de cinquante hommes monta, et vint, et se courba sur ses genoux devant Elie, et le supplia, et lui dit: Homme de Dieu, je te prie que tu fasses cas de ma vie, et de la vie de ces cinquante hommes tes serviteurs.
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
14 Voilà, le feu est descendu des cieux, et a consumé les deux premiers capitaines de cinquante hommes, avec leurs cinquantaines; mais maintenant [je te prie], que tu fasses cas de ma vie.
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
15 Et l'Ange de l'Eternel dit à Elie: Descends avec lui, n'aie point peur de lui. Il se leva donc, et descendit avec lui vers le Roi,
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
16 Et lui dit: Ainsi a dit l'Eternel: Parce que tu as envoyé des messagers pour consulter Bahal-zébub dieu de Hékron, comme s'il n'y avait point de Dieu en Israël, pour consulter sa parole: tu ne descendras point du lit sur lequel tu es monté, mais certainement tu mourras.
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
17 Il mourut donc, selon la parole de l'Eternel, qu'Elie avait prononcée; et Joram commença à régner en sa place, la seconde année de Joram, fils de Josaphat, Roi de Juda, parce qu'Achazia n'avait point de fils.
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Le reste des faits d'Achazia, lesquels il fit, n'est-il pas écrit au Livre des Chroniques des Rois d'Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

< 2 Rois 1 >