< Ezekiel 40 >

1 In the fyue and twentithe yeer of oure passyng ouer, in the bigynnyng of the yeer, in the tenthe dai of the monethe, in the fourtenthe yeer after that the citee was smytun, in this same dai the hond of the Lord was maad on me, and he brouyte me thidur in the reuelaciouns of God.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
2 And he brouyte me in to the lond of Israel, and he leet me doun on a ful hiy hil, on which was as the bildyng of a citee goynge to the south;
Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
3 and he ledde me in thidur. And lo! a man, whos licnesse was as the licnesse of bras, and a coorde of flex was in his hond, and a reed of mesure in his hond; forsothe he stood in the yate.
Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
4 And the same man spak to me, Thou sone of man, se with thin iyen, and here with thin eeris, and sette thin herte on alle thingis, whiche Y schal schewe to thee, for thou art brouyt hidur, that tho be schewid to thee; telle thou alle thingis whiche thou seest to the hous of Israel.
Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
5 And lo! a wal withouteforth, in the cumpas of the hous on ech side; and in the hond of the man was a rehed of mesure of sixe cubitis and a spanne, that is, an handibreede; and he mat the breede of the bildyng with o rehed, and the hiynesse bi o rehed.
Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
6 And he cam to the yate that bihelde the weie of the eest, and he stiede bi degrees of it; and he mat the lyntil of the yate bi o rehed the breede, that is, o lyntil bi o rehed in breede;
Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
7 and he mat o chaumbre bi o rehed in lengthe, and bi o rehed in breed, and fyue cubitis bitwixe chaumbris;
Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
8 and he mat the lyntil of the yate bisidis the porche of the yate with ynne, bi o rehed.
Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
9 And he mat the porch of the yate of eiyte cubitis, and the frount therof bi twei cubitis; sotheli the porche of the yate was with ynne.
ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
10 Certis the chaumbris of the yate at the weie of the eest weren thre on this side, and thre on that side; o mesure of thre, and o mesure of the frountis on euer ethir side.
Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
11 And he mat the breede of the lyntel of the yate of ten cubitis, and the lengthe of the yate of threttene cubitis.
Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
12 And he mat a margyn of a cubit bifor the chaumbris, and o cubit was the ende on ech side; forsothe the chaumbris weren of sixe cubitis on this side and on that side.
Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
13 And he mat the yate fro the roof of the chaumbre til to the roof therof, the breede of fyue and twenti cubitis, a dore ayens a dore.
Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
14 And he made frountes bi sixti cubitis, and at the frount an halle of the yate on ech side bi cumpas;
Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
15 and bifor the face of the yate that stretchith forth til to the face of the porche of the ynner yate, he mat fifti cubitis.
Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
16 And he mat wyndows naraw with out and large with ynne, in the chaumbris and frountis of tho, that weren with ynne the yate on ech side bi cumpas. Sotheli in lijk maner also wyndows weren in the porchis bi cumpas with ynne; and the peynture of palm trees was grauun bifor the frountis.
Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
17 And he ledde me out to the outermere halle, and lo! tresories, and pawment arayed with stoon in the halle bi cumpas; thretti tresories in the cumpas of the pawment;
Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
18 and the pawment was bynethe in the front of the yatis, bi the lengthe of the yatis.
Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
19 And he mat the breede fro the face of the lowere yate til to the frount of the ynnere halle with outforth, an hundrid cubitis at the eest, and at the north.
Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
20 And he mat bothe in lengthe and in breede the yate that bihelde the weie of the north, of the outermore halle.
Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
21 And he mat the chaumbris therof, thre on this side, and thre on that side, and the frount therof, and the porche therof, bi the mesure of the formere yate; the lengthe therof of fifti cubitis, and the breede therof of fyue and twenti cubitis.
Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
22 Sotheli the wyndows therof, and the porche, and the grauyngis, weren bi the mesure of the yate that bihelde to the eest; and the stiyng therof was of seuene degrees, and a porche was bifore it.
Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
23 And the yate of the ynnere halle was ayens the yate of the north, and ayens the eest yate; and he mat fro the yate til to the yate an hundrid cubitis.
Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
24 And he ledde me out to the weie of the south, and lo! the yate that bihelde to the south; and he mat the frount therof, and the porche therof, bi the formere mesuris;
Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
25 and the wyndows therof, and the porchis in cumpas, as othere wyndows; the lengthe of fifti cubitis, and the breede of fyue and twenti cubitis.
Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
26 And bi seuene degrees me stiede to it, and `an halle was bifor the yatis therof; and palme trees weren grauun, oon in this side, and another in that side in the frount therof.
Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
27 And the yate of the ynnere halle was in the weie of the south; and he mat fro the yate til to the yate in the weie of the south, an hundrid cubitis.
Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
28 And he ledde me in to the ynnere halle, to the south yate; and he mat the yate bi the formere mesuris;
Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
29 the chaumbre therof, and the frount therof, and the porche therof bi the same mesuris; and he mat the wyndows therof, and the porche therof in cumpas; fifti cubitis of lengthe, and fyue and twenti cubitis of breede.
Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
30 And he mat the halle bi cumpas, the lengthe of fyue and twenti cubitis, and the breede therof of fyue cubitis.
(Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
31 And the porche therof was to the outermere halle, and the palm trees therof in the frount; and eiyte degrees weren, bi whiche me stiede thorouy it.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
32 And he ledde me in to the ynnere halle, bi the eest weie; and he mat the yate by the formere mesures;
Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
33 the chaumbre therof, and the frount therof, and the porchis therof, as aboue; and he mat the wyndows therof, and the porchis therof in cumpas; the lengthe of fifti cubitis, and the breede of fyue and twenti cubitis; and the porche therof,
Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
34 that is, of the outermore halle; and palme trees grauun in the frount therof, on this side and on that side; and in eiyte degrees was the stiyng therof.
Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
35 And he ledde me in to the yate that bihelde to the north; and he mat bi the formere mesuris;
Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
36 the chaumbre therof, and the frount therof, and the porche therof, and the wyndows therof bi cumpas; the lengthe of fifti cubitis, and the breede of fyue and twenti cubitis.
kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
37 The porche therof bihelde to the outermore halle; and the grauyng of palm trees was in the frount therof, on this side and on that side; and in eiyte degrees was the stiyng therof.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
38 And bi alle tresories a dore was in the frountis of yatis; and there thei waischiden brent sacrifice.
Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
39 And in the porche of the yate weren twei boordis on this side, and twei boordis on that side, that brent sacrifice be offrid on tho, `bothe for synne and for trespasse.
Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
40 And at the outermore side, which stieth to the dore of the yate that goith to the north, weren twei boordis; and at `the tother side, bifor the porche of the yate, weren twei boordis.
Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
41 Foure boordis on this side, and foure boordis on that side; bi the sidis of the yate weren eiyte boordis, on whiche thei offriden.
Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
42 Forsothe foure boordis to brent sacrifice weren bildid of square stoonys, in the lengthe of o cubit and an half, and in the breed of o cubit and an half, and in the hiythe of o cubit; on whiche boordis thei schulen sette vessels, in whiche brent sacrifice and slayn sacrifice is offrid.
Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
43 And the brenkis of tho boordis ben of oon handibreede, and ben bowid ayen with ynne bi cumpas; forsothe on the boordis weren fleischis of offryng.
Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
44 And with out the ynnere yate weren tresories of chauntours, in the ynnere halle, that was in the side of the yate biholdynge to the north; and the faces of tho weren ayens the south weie; oon of the side of the eest yate, that bihelde to the weie of the north.
Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
45 And he seide to me, This treserie, that biholdith the south weie, is of the prestis that waken in the kepyngis of the temple,
Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
46 Sotheli the tresorye that biholdith to the weie of the north, schal be of the preestis that waken to the seruice of the auter; these ben the sones of Sadoch, whiche of the sones of Leuy neiyen to the Lord, for to mynystre to hym.
nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
47 And he mat the halle, the lengthe of an hundrid cubitis, and the breede of an hundrid cubitis, bi square, and the auter bifore the face of the temple.
Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
48 And he ledde me in to the porche of the temple; and he mat the porche bi fyue cubitis on this side, and bi fyue cubitis on that side; and he mat the breede of the yate, of thre cubitis on this side, and of thre cubitis on that side.
Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
49 But he mat the lengthe of the porche of twenti cubitis, and the breede of eleuene cubitis, and bi eiyte degrees me stiede to it; and pileris weren in the frountis, oon on this side, and `another on that side.
Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.

< Ezekiel 40 >