< Ezekiel 32 >

1 And it was don in the tweluethe yeer, in the tweluethe monethe, in the firste dai of the monethe, the word of the Lord was maad to me,
Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema:
2 and he seide, Thou, sone of man, take weilyng on Farao, kyng of Egipt, and thou schalt seie to hym, Thou were maad lijk to a lioun of hethene men, and to a dragoun whiche is in the see. And thou wyndewist with horn in thi floodis, and thou disturblidist watris with thi feet, and defoulidist the floodis of tho.
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama joka kubwa baharini, unayevuruga maji kwa miguu yako na kuchafua vijito.
3 Therfor the Lord God seith these thingis, Y schal spredde abrood my net on thee in the multitude of many puples, and Y schal drawe thee out in my net;
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
4 and Y schal caste forth thee in to erthe. On the face of the feeld Y schal caste thee awei, and Y schal make alle the volatils of heuene to dwelle on thee, and Y schal fille of thee the beestis of al erthe.
Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
5 And Y schal yyue thi fleischis on hillis, and Y schal fille thi litle hillis with thi root;
Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
6 and Y schal moiste the erthe with the stynk of thi blood on mounteyns, and valeis schulen be fillid of thee.
Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
7 And whanne thou schalt be quenchid, Y schal hile heuenes, and Y schal make blak the sterris therof; Y schal kyuere the sunne with a clowde, and the moone schal not yyue hir liyt.
Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
8 Y schal make alle the liyt yyueris of heuene to mourne on thee, and Y schal yyue derknessis on thi lond, seith the Lord God; whanne thi woundid men schulen falle doun in the myddis of erthe, seith the Lord God.
Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mwenyezi.
9 And Y schal terre to wraththe the herte of many puplis, whanne Y schal bringe in thi sorewe among folkis, on londis whiche thou knowist not.
Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo haujapata kuzijua.
10 And Y schal make many puplis to wondre on thee, and the kyngis of hem schulen drede with ful greet hidousnesse on thee, for alle thi wickidnessis whiche thou wrouytist, whanne my swerd schal bigynne to flee on the faces of hem. And alle men schulen be astonyed sudenli, for her lijf, in the dai of her fallyng.
Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
11 For the Lord God seith these thingis, The swerd of the king of Babiloyne schal come to thee;
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
12 in swerdis of stronge men Y schal caste doun thi multitude, alle these folkis ben not able to be ouercomun. And thei schulen waste the pride of Egipt, and the multitude therof schal be distried.
Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka kwa panga za watu mashujaa, taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote ya wajeuri yatashindwa.
13 And Y schal leese alle the beestis therof, that weren on ful many watris; and the foot of a man schal no more troble tho watris, nether the clee of beestis schal troble tho.
Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi, hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
14 Thanne Y schal yelde the watris of hem clenneste, and Y schal brynge the floodis of hem as oile, seith the Lord God,
Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mwenyezi.
15 whanne Y schal yyue desolat the lond of Egipt. Forsothe the lond schal be forsakun of his fulnesse, whanne Y schal smyte alle the dwellers therof; and thei schulen wite, that Y am the Lord.
Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo ndani yake, nitakapowapiga wote waishio humo, ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
16 It is a weiling, and the douytris of hethene men schulen biweile hym; thei schulen biweile hym on Egipt, and thei schulen biweile hym on the multitude therof, seith the Lord God.
“Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”
17 And it was don in the tweluethe yeer, in the fiftenthe dai of the monethe, the word of the Lord was maad to me,
Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
18 and he seide, Sone of man, synge thou a song of weilyng on the multitude of Egipt, and drawe thou doun it the same, and the douytris of stronge hethene men to the laste lond, with hem that yeden doun in to the lake.
“Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. (questioned)
19 In as myche as thou art fairere, go doun, and slepe with vncircumcidid men.
Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
20 In the myddis of slayn men thei schulen falle doun bi swerd; a swerd is youun, and thei drowen it to, and alle the puplis therof.
Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote.
21 The myytieste of stronge men schulen speke to hym, fro the myddis of helle, whiche with her helperis yeden doun, and slepten vncircumcidid, and slayn bi swerd. (Sheol h7585)
Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol h7585)
22 There is Assur, and al his multitude; the sepulcris of hem ben in the cumpas of hym, alle slayn men, and that fellen doun bi swerd,
“Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
23 whose sepulcris ben youun in the laste thingis of the lake. And the multitude of hym is maad bi the cumpas of his sepulcre, alle slayn men, and fallynge doun bi swerd, whiche yauen sum tyme her ferdfulnesse in the lond of lyuynge men.
Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
24 There is Helam, and al the multitude therof bi the cumpas of his sepulcre; alle these weren slayn, and fallynge doun bi swerd, that yeden doun vncircumcidid to the laste lond; whiche settiden her drede in the lond of lyuynge men, and baren her schenschipe with hem that goon doun in to the lake.
“Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. (questioned)
25 In the myddis of slayn men thei puttiden his bed in alle the puplis of hym; his sepulcre is in the cumpas of hym. Alle these weren vncircumcidid and slayn bi swerd, for thei yauen drede in the lond of lyuynge men, and baren her schenschipe with hem that gon doun in to the lake; thei ben set in the myddis of slayn men.
Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
26 There ben Mosoch and Tubal, and al the multitude therof; the sepulcris therof ben in the cumpasse therof. Alle these men vncircumcidid weren slayn, and fallynge doun bi swerd, for thei yauen her drede in the lond of lyuynge men.
“Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
27 And thei schulen not slepe with stronge men, and fallynge doun, and vncircumcidid, that yeden doun in to helle with her armuris, and puttiden her swerdis vndur her heedis. And the wickidnessis of hem weren in the boonys of hem, for thei weren maad the drede of stronge men in the lond of lyuynge men. (Sheol h7585)
Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
28 And thou therfor schalt be al to-foulid in the myddis of vncircumcidid men, and schalt slepe with hem that ben slayn bi swerd.
“Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
29 There is Idumee, and the kingis therof, and alle duykis therof, that ben youun with her oost, with men slayn bi swerd, and which slepten with vncircumcidid men, and with hem that yeden doun in to the lake.
“Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.
30 There ben alle princes of the north, and alle hunteris, that weren led forth with slayn men, that ben dredinge and schent in her strengthe, which slepten vncircumcidid with men slayn bi swerd, and baren her schenschipe with hem that yeden doun in to the lake.
“Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.
31 Farao siy hem, and was coumfortid on al his multitude that was slayn bi swerd. And Farao and al his oost, seith the Lord God, baren her schenschipe with hem that yeden doun in to the lake;
“Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
32 for he yaf his drede in the lond of lyuynge men. And Farao and al his multitude slepte in the myddis of vncircumcidid men, with men slayn bi swerd, seith the Lord God.
Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 32 >