< Matthew 20 >

1 “For the Kingdom of Heaven is like a man who was the master of a household, who went out early in the morning to hire labourers for his vineyard.
“Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2 When he had agreed with the labourers for a denarius a day, he sent them into his vineyard.
Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3 He went out about the third hour, and saw others standing idle in the marketplace.
Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4 He said to them, ‘You also go into the vineyard, and whatever is right I will give you.’ So they went their way.
Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5 Again he went out about the sixth and the ninth hour, and did likewise.
Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6 About the eleventh hour he went out and found others standing idle. He said to them, ‘Why do you stand here all day idle?’
Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7 “They said to him, ‘Because no one has hired us.’ “He said to them, ‘You also go into the vineyard, and you will receive whatever is right.’
Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8 “When evening had come, the lord of the vineyard said to his manager, ‘Call the labourers and pay them their wages, beginning from the last to the first.’
“Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9 “When those who were hired at about the eleventh hour came, they each received a denarius.
Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10 When the first came, they supposed that they would receive more; and they likewise each received a denarius.
Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11 When they received it, they murmured against the master of the household,
Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12 saying, ‘These last have spent one hour, and you have made them equal to us who have borne the burden of the day and the scorching heat!’
Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13 “But he answered one of them, ‘Friend, I am doing you no wrong. Didn’t you agree with me for a denarius?
“Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14 Take that which is yours, and go your way. It is my desire to give to this last just as much as to you.
Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15 Isn’t it lawful for me to do what I want to with what I own? Or is your eye evil, because I am good?’
Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
16 So the last will be first, and the first last. For many are called, but few are chosen.”
Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
17 As Yeshua was going up to Jerusalem, he took the twelve disciples aside, and on the way he said to them,
Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
18 “Behold, we are going up to Jerusalem, and the Son of Man will be delivered to the chief priests and scribes, and they will condemn him to death,
“Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19 and will hand him over to the Gentiles to mock, to scourge, and to crucify; and the third day he will be raised up.”
Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
20 Then the mother of the sons of Zebedee came to him with her sons, kneeling and asking a certain thing of him.
Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21 He said to her, “What do you want?” She said to him, “Command that these, my two sons, may sit, one on your right hand and one on your left hand, in your Kingdom.”
Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
22 But Yeshua answered, “You don’t know what you are asking. Are you able to drink the cup that I am about to drink, and be immersed with the immersion that I am immersed with?” They said to him, “We are able.”
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
23 He said to them, “You will indeed drink my cup, and be immersed with the immersion that I am immersed with; but to sit on my right hand and on my left hand is not mine to give, but it is for whom it has been prepared by my Father.”
Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
24 When the ten heard it, they were indignant with the two brothers.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25 But Yeshua summoned them, and said, “You know that the rulers of the nations lord it over them, and their great ones exercise authority over them.
Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26 It shall not be so amongst you; but whoever desires to become great amongst you shall be your servant.
Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27 Whoever desires to be first amongst you shall be your bondservant,
na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28 even as the Son of Man came not to be served, but to serve, and to give his life as a ransom for many.”
Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
29 As they went out from Jericho, a great multitude followed him.
Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30 Behold, two blind men sitting by the road, when they heard that Yeshua was passing by, cried out, “Lord, have mercy on us, you son of David!”
Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
31 The multitude rebuked them, telling them that they should be quiet, but they cried out even more, “Lord, have mercy on us, you son of David!”
Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
32 Yeshua stood still and called them, and asked, “What do you want me to do for you?”
Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
33 They told him, “Lord, that our eyes may be opened.”
Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
34 Yeshua, being moved with compassion, touched their eyes; and immediately their eyes received their sight, and they followed him.
Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.

< Matthew 20 >