< Mark 1 >

1 The beginning of the Good News of Yeshua the Messiah, the Son of God.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 As it is written in the Prophets, “Behold, I send my messenger before your face, who will prepare your way before you:
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 the voice of one crying in the wilderness, ‘Make ready the way of the Lord! Make his paths straight!’”
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 Yochanan came immersing in the wilderness and proclaiming the immersion of repentance for forgiveness of sins.
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 All the country of Judea and all those of Jerusalem went out to him. They were immersed by him in the Jordan river, confessing their sins.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 Yochanan was clothed with camel’s hair and a leather belt around his waist. He ate locusts and wild honey.
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 He preached, saying, “After me comes he who is mightier than I, the strap of whose sandals I am not worthy to stoop down and loosen.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 I immersed you in water, but he will immerse you in the Holy Spirit.”
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 In those days, Yeshua came from Nazareth of Galilee, and was immersed by Yochanan in the Jordan.
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 Immediately coming up from the water, he saw the heavens parting and the Spirit descending on him like a dove.
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 A voice came out of the sky, “You are my beloved Son, in whom I am well pleased.”
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 Immediately the Spirit drove him out into the wilderness.
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 He was there in the wilderness forty days, tempted by Satan. He was with the wild animals; and the angels were serving him.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 Now after Yochanan was taken into custody, Yeshua came into Galilee, proclaiming the Good News of God’s Kingdom,
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 and saying, “The time is fulfilled, and God’s Kingdom is at hand! Repent, and believe in the Good News.”
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 Passing along by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew, the brother of Simon, casting a net into the sea, for they were fishermen.
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 Yeshua said to them, “Come after me, and I will make you into fishers for men.”
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 Immediately they left their nets, and followed him.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Going on a little further from there, he saw Jacob the son of Zebedee, and Yochanan his brother, who were also in the boat mending the nets.
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Immediately he called them, and they left their father, Zebedee, in the boat with the hired servants, and went after him.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 They went into Capernaum, and immediately on the Sabbath day he entered into the synagogue and taught.
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 They were astonished at his teaching, for he taught them as having authority, and not as the scribes.
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 Immediately there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he cried out,
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 saying, “Ha! What do we have to do with you, Yeshua, you Nazarene? Have you come to destroy us? I know who you are: the Holy One of God!”
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 Yeshua rebuked him, saying, “Be quiet, and come out of him!”
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 The unclean spirit, convulsing him and crying with a loud voice, came out of him.
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 They were all amazed, so that they questioned amongst themselves, saying, “What is this? A new teaching? For with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him!”
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 The report of him went out immediately everywhere into all the region of Galilee and its surrounding area.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 Immediately, when they had come out of the synagogue, they came into the house of Simon and Andrew, with Jacob and Yochanan.
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 Now Simon’s wife’s mother lay sick with a fever, and immediately they told him about her.
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 He came and took her by the hand and raised her up. The fever left her immediately, and she served them.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 At evening, when the sun had set, they brought to him all who were sick and those who were possessed by demons.
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 All the city was gathered together at the door.
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 He healed many who were sick with various diseases and cast out many demons. He didn’t allow the demons to speak, because they knew him.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 Early in the morning, while it was still dark, he rose up and went out, and departed into a deserted place, and prayed there.
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 Simon and those who were with him searched for him.
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 They found him and told him, “Everyone is looking for you.”
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 He said to them, “Let’s go elsewhere into the next towns, that I may proclaim there also, because I came out for this reason.”
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 He went into their synagogues throughout all Galilee, proclaiming and casting out demons.
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 A leper came to him, begging him, kneeling down to him, and saying to him, “If you want to, you can make me clean.”
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 Being moved with compassion, he stretched out his hand, and touched him, and said to him, “I want to. Be made clean.”
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 When he had said this, immediately the leprosy departed from him and he was made clean.
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 He strictly warned him and immediately sent him out,
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 and said to him, “See that you say nothing to anybody, but go show yourself to the priest and offer for your cleansing the things which Moses commanded, for a testimony to them.”
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 But he went out, and began to proclaim it much, and to spread about the matter, so that Yeshua could no more openly enter into a city, but was outside in desert places. People came to him from everywhere.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.

< Mark 1 >