< Luke 1 >

1 Since many have undertaken to set in order a narrative concerning those matters which have been fulfilled amongst us,
Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2 even as those who from the beginning were eyewitnesses and servants of the word delivered them to us,
Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3 it seemed good to me also, having traced the course of all things accurately from the first, to write to you in order, most excellent Theophilus;
Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4 that you might know the certainty concerning the things in which you were instructed.
ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judea, a certain priest named Zechariah, of the priestly division of Abijah. He had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elisheva.
Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6 They were both righteous before God, walking blamelessly in all the commandments and ordinances of the Lord.
Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7 But they had no child, because Elisheva was barren, and they both were well advanced in years.
Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now while he executed the priest’s office before God in the order of his division
Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9 according to the custom of the priest’s office, his lot was to enter into the temple of the Lord and burn incense.
Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10 The whole multitude of the people were praying outside at the hour of incense.
Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11 An angel of the Lord appeared to him, standing on the right side of the altar of incense.
Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12 Zechariah was troubled when he saw him, and fear fell upon him.
Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 But the angel said to him, “Don’t be afraid, Zechariah, because your request has been heard. Your wife, Elisheva, will bear you a son, and you shall call his name Yochanan.
Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14 You will have joy and gladness, and many will rejoice at his birth.
Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he will be great in the sight of the Lord, and he will drink no wine nor strong drink. He will be filled with the Holy Spirit, even from his mother’s womb.
Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 He will turn many of the children of Israel to the Lord their God.
Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 He will go before him in the spirit and power of Elijah, ‘to turn the hearts of the fathers to the children,’ and the disobedient to the wisdom of the just; to prepare a people prepared for the Lord.”
Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18 Zechariah said to the angel, “How can I be sure of this? For I am an old man, and my wife is well advanced in years.”
Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
19 The angel answered him, “I am Gabriel, who stands in the presence of God. I was sent to speak to you and to bring you this good news.
Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20 Behold, you will be silent and not able to speak until the day that these things will happen, because you didn’t believe my words, which will be fulfilled in their proper time.”
Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21 The people were waiting for Zechariah, and they marvelled that he delayed in the temple.
Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22 When he came out, he could not speak to them. They perceived that he had seen a vision in the temple. He continued making signs to them, and remained mute.
Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23 When the days of his service were fulfilled, he departed to his house.
Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24 After these days Elisheva his wife conceived, and she hid herself five months, saying,
Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25 “Thus has the Lord done to me in the days in which he looked at me, to take away my reproach amongst men.”
“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
26 Now in the sixth month, the angel Gabriel was sent from God to a city of Galilee named Nazareth,
Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27 to a virgin pledged to be married to a man whose name was Joseph, of David’s house. The virgin’s name was Miriam.
kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28 Having come in, the angel said to her, “Rejoice, you highly favoured one! The Lord is with you. Blessed are you amongst women!”
Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
29 But when she saw him, she was greatly troubled at the saying, and considered what kind of salutation this might be.
Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 The angel said to her, “Don’t be afraid, Miriam, for you have found favour with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 Behold, you will conceive in your womb and give birth to a son, and shall name him ‘Yeshua.’
Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32 He will be great and will be called the Son of the Most High. The Lord God will give him the throne of his father David,
Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33 and he will reign over the house of Jacob forever. There will be no end to his Kingdom.” (aiōn g165)
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 Miriam said to the angel, “How can this be, seeing I am a virgin?”
Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
35 The angel answered her, “The Holy Spirit will come on you, and the power of the Most High will overshadow you. Therefore also the holy one who is born from you will be called the Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36 Behold, Elisheva your relative also has conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who was called barren.
Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37 For nothing spoken by God is impossible.”
Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Miriam said, “Behold, the servant of the Lord; let it be done to me according to your word.” Then the angel departed from her.
Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
39 Miriam arose in those days and went into the hill country with haste, into a city of Judah,
Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40 and entered into the house of Zechariah and greeted Elisheva.
Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41 When Elisheva heard Miriam’s greeting, the baby leapt in her womb; and Elisheva was filled with the Holy Spirit.
Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42 She called out with a loud voice and said, “Blessed are you amongst women, and blessed is the fruit of your womb!
akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43 Why am I so favoured, that the mother of my Lord should come to me?
Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For behold, when the voice of your greeting came into my ears, the baby leapt in my womb for joy!
Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 Blessed is she who believed, for there will be a fulfilment of the things which have been spoken to her from the Lord!”
Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46 Miriam said, “My soul magnifies the Lord.
Naye Maria akasema,
47 My spirit has rejoiced in God my Saviour,
“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48 for he has looked at the humble state of his servant. For behold, from now on, all generations will call me blessed.
Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49 For he who is mighty has done great things for me. Holy is his name.
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50 His mercy is for generations and generations on those who fear him.
Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51 He has shown strength with his arm. He has scattered the proud in the imagination of their hearts.
Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 He has put down princes from their thrones, and has exalted the lowly.
amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53 He has filled the hungry with good things. He has sent the rich away empty.
Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54 He has given help to Israel, his servant, that he might remember mercy,
Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55 as he spoke to our fathers, to Abraham and his offspring forever.” (aiōn g165)
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
56 Miriam stayed with her about three months, and then returned to her house.
Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57 Now the time that Elisheva should give birth was fulfilled, and she gave birth to a son.
Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58 Her neighbours and her relatives heard that the Lord had magnified his mercy towards her, and they rejoiced with her.
Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59 On the eighth day, they came to circumcise the child; and they would have called him Zechariah, after the name of his father.
Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60 His mother answered, “Not so; but he will be called Yochanan.”
Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61 They said to her, “There is no one amongst your relatives who is called by this name.”
Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62 They made signs to his father, what he would have him called.
Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63 He asked for a writing tablet, and wrote, “His name is Yochanan.” They all marvelled.
Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64 His mouth was opened immediately and his tongue freed, and he spoke, blessing God.
Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 Fear came on all who lived around them, and all these sayings were talked about throughout all the hill country of Judea.
Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66 All who heard them laid them up in their heart, saying, “What then will this child be?” The hand of the Lord was with him.
Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67 His father Zechariah was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68 “Blessed be the Lord, the God of Israel, for he has visited and redeemed his people;
“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69 and has raised up a horn of salvation for us in the house of his servant David
Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70 (as he spoke by the mouth of his holy prophets who have been from of old), (aiōn g165)
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
71 salvation from our enemies and from the hand of all who hate us;
kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 to show mercy towards our fathers, to remember his holy covenant,
Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73 the oath which he swore to Abraham our father,
Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74 to grant to us that we, being delivered out of the hand of our enemies, should serve him without fear,
tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75 in holiness and righteousness before him all the days of our life.
kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76 And you, child, will be called a prophet of the Most High; for you will go before the face of the Lord to prepare his ways,
Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77 to give knowledge of salvation to his people by the remission of their sins,
kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78 because of the tender mercy of our God, by which the dawn from on high will visit us,
Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79 to shine on those who sit in darkness and the shadow of death; to guide our feet into the way of peace.”
na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80 The child was growing and becoming strong in spirit, and was in the desert until the day of his public appearance to Israel.
Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.

< Luke 1 >