< Romans 5 >

1 Because therfore that we are iustified by fayth we are at peace with god thorow oure Lorde Iesue Christ:
Kwa kuwa tumehesabiwa haki kwa njia ya imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
2 by who we have awaye in thorow fayth vnto this grace wherin we stonde aud reioyce in hope of the prayse that shalbe geven of God.
Kupitia yeye sisi pia tuna fursa kwa njia ya imani katika neema hii ambayo ndani yake tunasimama. Tunafurahi katika ujasiri atupao Mungu kwa ajili ya baadaye, ujasiri ambao tutashiriki katika utukufu wa Mungu.
3 Nether do we so only: but also we reioyce in tribulacion. For we know that tribulacion bringeth pacience
Siyo hili tu, lakini pia tunafurahi katika mateso yetu. Tunajua kwamba mateso huzaa uvumilivu.
4 pacience bringeth experience experience bringeth hope.
Uvumilivu huzaa kukubalika, na kukubalika huzaa ujasiri kwa ajili ya baadaye.
5 And hope maketh not ashamed for the love of God is sheed abrod in oure hertes by the holy goost which is geven vnto vs.
Ujasiri huu haukatishi tamaa, kwa sababu upendo wa Mungu umemwagwa katika mioyo yetu kupitia Roho Mtakatifu, ambaye alitolewa kwetu.
6 For when we were yet weake accordynge to ye tyme: Christ dyed for vs which were vngodly.
Kwa tulipokuwa tungali tu dhaifu, kwa wakati muafaka Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.
7 Yet scace will eny man dye for a rightewes man. Paraventure for a good ma durst a man dye.
Kwa kuwa itakuwa vigumu mmoja kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki. Hii ni kwamba, pengine mtu angethubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
8 But God setteth out his love that he hath to vs seinge that whyll we were yet synners Christ dyed for vs.
Lakini Mungu amehakikisha upendo wake mwenyewe kwetu, kwa sababu wakati tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
9 Moche more then now (seynge we are iustifyed in his bloud) shall we be saved from wrath thorow him.
Kisha zaidi ya yote, sasa kwa kuwa tumehesabiwa haki kwa damu yake, tutaokolewa kwa hiyo kutoka katika gadhabu ya Mungu.
10 For yf when we were enemyes we were reconciled to God by the deeth of his sonne: moche more seinge we are reconciled we shal be preservid by his lyfe.
Kwa kuwa, ikiwa wakati tulipokuwa maadui, tulipatanishwa na Mungu kwa njia ya kifo cha mwanae, zaidi sana, baada ya kuwa tumekwisha patanishwa, tutaokolewa kwa maisha yake.
11 Not only so but we also ioye in God by the meanes of oure Lorde Iesus Christ by whom we have receavyd the attonment.
Siyo hivi tu, bali pia tunafurahi katika Mungu kupitia Bwana Yesu Kristo, kupitia yeye ambaye sasa tumepokea upatanisho huu.
12 Wherfore as by one ma synne entred into the worlde and deeth by the meanes of synne. And so deeth went over all men in somoche that all men synned.
Kwa hiyo basi, kama kupitia mtu mmoja dhambi iliingia duniani, kwa njia hii kifo kiliingia kwa njia ya dhambi. Na kifo kikasambaa kwa watu wote, kwa sababu wote walifanya dhambi.
13 For even vnto the tyme of the lawe was synne in the worlde: but synne was not regarded as longe as ther was no lawe:
Kwa kuwa hadi sheria, dhambi ilikuwa duniani, lakini dhambi haihesabiki wakati hakuna sheria.
14 neverthelesse deeth rayned fro Adam to Moses eve over them also that synned not wt lyke transgression as dyd Adam: which is ye similitude of him that is to come.
Hata hivyo, kifo kilitawala kutoka Adamu hadi Musa, hata juu ya wale ambao hawakufanya dhambi kama kutotii kwa Adamu, ambaye ni mfano wa yeye ambaye angekuja.
15 But the gyfte is not lyke as the synne. For yf thorow the synne of one many be deed: moche more plenteous vpon many was the grace of God and gyfte by grace: which grace was geven by one man Iesus Christ.
Lakini hata hivyo, zawadi ya bure si kama kosa. Kwa kuwa ikiwa kwa kosa la mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu na zawadi kwa neema ya mtu mmoja, Yesu Kristo, imezidi kuongezeka kwa wengi.
16 And ye gifte is not over one synne as deeth cam thorow one synne of one yt synned. For damnacion cam of one synne vnto condemnacion: but the gyft cam to iustify fro many synnes.
Kwa kuwa zawadi si kama matokeo ya yule ambaye alifanya dhambi. Kwa kuwa kwa upande mwingine, hukumu ya adhabu ilikuja kwa sababu ya kosa la mtu mmoja. Lakini kwa upande mwingine, kipawa cha bure kinachotoka katika kuhesabiwa haki kilikuja baada ya makosa mengi.
17 For yf by the synne of one deeth raigned by the meanes of one moche more shall they which receave aboundance of grace and of the gyfte of rightewesnes raygne in lyfe by the meanes of one (that is to saye) Iesus Christ.
Kwa maana, ikiwa kwa kosa la mmoja, kifo kilitawala kupitia mmoja, zaidi sana wale ambao watapokea neema nyingi pamoja na kipawa cha haki watatawala kupitia maisha ya mmoja, Yesu Kristo.
18 Lykewyse then as by the synne of one condemnacion cam on all men: eve so by the iustifyinge of one cometh the rightewesnes that bringeth lyfe vpo all men.
Hivyo basi, kama kupitia kosa moja watu wote walikuja kwenye hukumu, ingawa kupitia tendo moja la haki kulikuja kuhesabiwa haki ya maisha kwa watu wote.
19 For as by one manes disobediece many be cam synners: so by ye obediece of one shall many be made righteous.
Kwa kuwa kama kupitia kutotii kwa mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, hivyo kupitia utii wa mmoja wengi watafanywa wenye haki.
20 But ye lawe in the meane tyme entred in yt synne shuld encreace. Neverthelater where aboundaunce of synne was there was more plenteousnes of grace.
Lakini sheria iliingia pamoja, ili kwamba kosa liweze kuenea. Lakini mahali ambapo dhambi ilizidi kuwa nyingi, neema iliongezeka hata zaidi.
21 That as synne had raigned vnto deeth even so might grace raygne thorow rightewesnes vnto eternall lyfe by the helpe of Iesu Christ. (aiōnios g166)
Hii ilitokea ili kwamba, kama dhambi ilivyotawala katika kifo, ndivyo hata neema inaweza kutawala kupitia haki kwa ajili ya maisha ya milele kupitia Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)

< Romans 5 >