< Romans 3 >

1 What preferment then hath the Iewe? other what a vauntageth circumcision?
Kisha ni faida gani aliyo nayo Myahudi? Na faida ya tohara ni nini?
2 Surely very moche. Fyrst vnto them was committed the worde of God
Ni vyema sana kwa kila njia. Awali ya yote, Wayahudi walikabidhiwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
3 What then though some of them did not beleve? shall their vnbeleve make the promes of god with out effecte?
Lakini, itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kuwa batili?
4 God forbid. Let god be true and all men lyars as it is written: That thou myghtest be iustifyed in thy sayinge and shuldest overcome when thou arte iudged.
La hasha. Badala yake, acha Mungu aonekane kuwa kweli, hata kama kila mtu ni mwongo. Kama ilivyokuwa imeandikwa, “Ya kwamba uweze kuonekana kuwa mwenye haki katika maneno yako, na uweze kushinda uingiapo katika hukumu.”
5 Yf oure vnrightewesnes make the rightewesnes of God more excellent: what shall we saye? Is God vnrighteous which taketh vengeauce? I speake after the maner of me.
Lakini ikiwa uovu wetu unaonesha haki ya Mungu, tuseme nini? Mungu si dhalimu atoapo ghadhabu yake, je yupo hivyo? Naongea kutokana na mantiki ya kibinadamu.
6 God forbid. For how then shall God iudge the worlde?
La hasha! Ni jinsi gani basi Mungu atauhukumu ulimwengu?
7 Yf the veritie of God appere moare excellent thorow my lye vnto his prayse why am I hence forth iudged as a synner?
Lakini ikiwa kweli ya Mungu kupitia uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado nahukumiwa kama mwenye dhambi?
8 and saye not rather (as men evyll speake of vs and as some affirme that we saye) let vs do evyll that good maye come therof. Whose damnacion is iuste.
Kwa nini tusiseme, kama tulivyosingiziwa na kama wengine wanavyothibitisha kwamba tunasema, “Tufanye uovu, ili mema yaje”? Hukumu juu yao ni ya haki.
9 What saye we then? Are we better then they? No in no wyse. For we have all ready proved how that both Iewes and Gentils are all vnder synne
Ni nini basi? Tunajitetea wenyewe? Hapana kabisa. Kwa kuwa sisi tayari tumewatuhumu Wayahudi na Wayunani wote pamoja, ya kuwa wapo chini ya dhambi.
10 as it is writte: There is none righteous no not one:
Hii ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hata mmoja.
11 There is none that vnderstondith there is none yt seketh after God
Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
12 they are all gone out of ye waye they are all made vnprofytable ther is none that doeth good no not one.
Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
13 Their throte is an open sepulchre with their tounges they have disceaved: the poyson of Aspes is vnder their lippes.
Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
14 Whose mouthes are full of coursynge and bitternes.
Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
15 Their fete are swyfte to sheed bloud.
Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
16 Destruccion and wretchednes are in their wayes.
Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
17 And the waye of peace they have not knowen.
Watu hawa hawajajua njia ya amani.
18 There is no feare of God before their eyes.
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao.”
19 Ye and we knowe that whatsoever ye lawe sayth he sayth it to them which are vnder the lawe. That all mouthes maye be stopped and all the worlde be subdued to god
Sasa tunajua kwamba chochote sheria isemacho, husema na wale walio chini ya sheria. Hii ni ili kwamba kila kinywa kifungwe, na hivyo kwamba ulimwengu wote uweze kuwajibika kwa Mungu.
20 because that by ye dedes of the lawe shall no flesshe be iustified in the sight of God. For by the lawe commeth the knowledge of synne.
Hii ni kwa sababu hakuna mwili utakaohesabiwa haki kwa matendo ya sheria mbele za macho yake. Kwa kuwa kupitia Sheria huja ufahamu wa dhambi.
21 Now verely is ye rigtewesnes that cometh of God declared without the fulfillinge of ye lawe havinge witnes yet of ye lawe and of the Prophetes.
Lakini sasa pasipo sheria, haki ya Mungu imejulikana. Ilishuhudiwa kwa sheria na Manabii,
22 The rightewesnes no dout which is good before God cometh by ye fayth of Iesus Christ vnto all and vpon all that beleve. Ther is no differece:
hiyo ni, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo kwa wale wote wanaoamini. Maana hakuna tofauti.
23 for all have synned and lacke the prayse yt is of valoure before God:
Kwa kuwa wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
24 but are iustified frely by his grace through the redemcion that is in Christ Iesu
Wamehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 whom God hath made a seate of mercy thorow faith in his bloud to shewe ye rightewesnes which before him is of valoure in yt he forgeveth ye synnes yt are passed which God dyd suffre
Kwa maana Mungu alimtoa Kristo Yesu awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alimtoa Kristo kama ushahidi wa haki yake, kwa sababu ya kuziachilia dhambi zilizopita
26 to shewe at this tyme ye rightewesnes yt is alowed of him yt he myght be couted iuste and a iustifiar of him which belevith on Iesus.
katika uvumilivu wake. Haya yote yalitokea ili kuonesha haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kujithibitisha mwenyewe kuwa haki, na kuonesha kwamba humhesabia haki mtu yeyote kwa sababu ya imani katika Yesu.
27 Where is then thy reioysinge? It is excluded. By what lawe? by ye lawe of workes? Naye: but by the lawe of fayth.
Kuwapi basi kujisifu? Kumetengwa. Kwa misingi ipi? Misingi ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani.
28 For we suppose that a man is iustified by fayth without the dedes of ye lawe.
Hivyo tunahitimisha kwamba mtu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
29 Is he the God of the Iewes only? Is he not also the God of the Gentyls? Yes eve of the Gentyles also.
Au Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Ndiyo, wa mataifa pia.
30 For it is God only which iustifieth circumcision which is of fayth and vncircumcision thorow fayth.
Ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja, atawahesabia haki walio wa tohara kwa imani, na wasiotahiriwa kwa njia ya imani.
31 Do we then destroye the lawe thorow fayth? God forbid. But we rather mayntayne the lawe.
Je sisi twaibatilisha sheria kwa imani? La hasha! Kinyume cha hayo, sisi twaithibitisha sheria.

< Romans 3 >