< Romans 10 >

1 Brethren my hertes desyre and prayer to God for Israel is that they might be saved.
Ndugu, nia ya moyo wangu na ombi langu kwa Mungu ni kwa ajili yao, kwa ajili ya wokovu wao.
2 For I beare them recorde that they have a fervet mynde to God warde but not accordinge to knowledge.
Kwa kuwa nawashuhudia kwamba wanajuhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si kwa ajili ya ufahamu.
3 For they are ignoraut of the rightewesnes which is alowed before God and goo about to stablisshe their awne rightewesnes and therfore are not obedient vnto the rightewesnes which is of valew before God.
Kwa kuwa hawajui haki ya Mungu, na wanatafuta kujenga haki yao wenyewe. Hawakuwa watiifu kwa haki ya Mungu.
4 For Christ is the ende of the lawe to iustifie all that beleve.
Kwa kuwa Kristo ndiye utimilifu wa sheria kwa ajili ya haki ya kila mtu aaminiye.
5 Moses describeth the rightewesnes which cometh of ye lawe howe that the man which doth the thinges of the lawe shall lyve therin.
Kwa kuwa Musa anaandika kuhusu haki ambayo huja kutokana na sheria: “Mtu ambaye hutenda haki ya sheria ataishi kwa haki hii.”
6 But ye rightewesnes which cometh of fayth speaketh on this wyse. Saye not in thyne hert who shall ascende into heven? (that is nothinge els then to fetch Christ doune)
Lakini haki ambayo inatokana na imani husema hivi, “Usiseme moyoni mwako, 'Nani atapaa kwenda mbinguni?' (Hii ni kumleta Kristo chini).
7 Other who shall descende into the depe? (that is nothinge els but to fetch vp Christ from deeth) (Abyssos g12)
Na usiseme, 'Nani atashuka katika shimo?”' (Hii ni, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu). (Abyssos g12)
8 But what sayth the scripture? The worde is nye the even in thy mouth and in thyn herte. This worde is the worde of fayth which we preache.
Lakini inasema nini? “Neno liko karibu na wewe, katika kinywa chako na katika moyo wako.” Hilo ni neno la imani, ambalo tunatangaza.
9 For yf thou shalt knowledge wt thy mouth that Iesus is the lorde and shalt beleve with thyn hert that God raysed him up from deeth thou shalt be safe.
Kwa kuwa kama kwa kinywa chako unamkiri Yesu ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
10 For the belefe of the hert iustifieth: and to knowledge with the mouth maketh a man safe.
Kwa kuwa kwa moyo mtu huamini na kupata haki, na kwa kinywa hukiri na kupata wokovu.
11 For the scripture sayth: whosoever beleveth on him shall not be ashamed.
Kwa kuwa andiko lasema, “Kila amwaminiye hata aibika.”
12 Ther is no difference bitwene the Iewe and the gentyll. For one is Lorde of all which is ryche vnto all that call on him.
kwa kuwa hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani. Kwa kuwa Bwana yule yule ni Bwana wa wote, na ni tajiri kwa wote wamwitao.
13 For whosoever shall call on the name of the lorde shalbe safe.
Kwa kuwa kila mtu ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka.
14 But how shall they call on him on who they beleved not? how shall they beleve on him of whom they have not herde? how shall they heare with out a preacher?
Kwa jinsi gani wanaweza kumwita yeye ambaye hawajamwamini? Na jinsi gani wanaweza kuamini katika yeye ambaye hawajamsikia? Na watasikiaje pasipo muhubiri?
15 And how shall they preach except they be sent? As it is written: how beautifull are the fete of them which bringe glad tydynges of peace and bringe glad tydynges of good thinges.
Na jinsi gani wanaweza kuhubiri, isipokuwa wametumwa? - Kama ilivyoandikwa, “Jinsi gani ni mizuri miguu ya wale ambao wanatangaza habari za furaha za mambo mema!”
16 But they have not all obeyed to ye gospell. For Esaias sayth: Lorde who shall beleve oure sayinges?
Lakini wote hawakusikiliza injili. Kwa kuwa Isaya hunena, “Bwana, ni nani aliyesikia ujumbe wetu?”
17 So then fayth cometh by hearynge and hearynge cometh by the worde of God.
Hivyo imani huja kutokana na kusikia, na kusikia kwa neno la Kristo.
18 But I axe: have they not herde? No dout their sounde went out into all londes: and their wordes in to the endes of the worlde.
Lakini nasema, “Je hawakusikia?” Ndiyo, kwa hakika sana. “Sauti yao imekwisha toka nje katika nchi yote, na maneno yao kwenda miisho ya dunia.”
19 But I demaunde whether Israel dyd knowe or not? Fyrst Moses sayth: I will provoke you for to envy by the that are no people and by a folisshe nacion I will anger you.
Zaidi ya yote, Ninasema, “Je Israel hakujua?” Kwanza Musa hunena, “Nitawachokoza kuwatia wivu kwa watu ambao si taifa. Kwa njia ya taifa lisilo na uelewa, nitawachochea hadi mkasirike.”
20 Esaias after that is bolde and sayth. I am founde of the that sought me not and have appered to them that axed not after me.
Na Isaya ni jasiri sana na husema, “Nilipatikana na wale ambao hawakunitafuta. Nilionekana kwa wale ambao hawakunihitaji.”
21 And agaynst Israel he sayth: All daye longe have I stretched forth my hondes vnto a people yt beleveth not but speaketh agaynst me.
Lakini kwa Israel husema, “Siku zote nilinyoosha mikono yangu kwa wasiotii na kwa watu wagumu.”

< Romans 10 >