+ Revelation 1 >

1 The reuelacion of Iesus Christe which god gave vnto him for to shewe vnto his servauntes thinges which muste shortly come to passe. And he sent and shewed by his angell vnto his servaunt Ihon
Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
2 which bare recorde of the worde of god and of the testimony of Iesus Christe and of all thinges yt he sawe.
naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
3 Happy is he that redith and they that heare the wordes of the prophesy and kepe thoo thinges which are written therin. For the tyme is at honde.
Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
4 Ihon to the. vii. congregacios in Asia. Grace be with you and peace from him which is and which was and which is to come and from the. vii. spretes which are present before his trone
Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5 and from Iesus Christ which is a faythfull witnes and fyrst begotte of the deed: and Lorde over the kinges of the erth. Vnto him that loved vs and wesshed vs fro synnes in his awne bloud
na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
6 and made vs kinges and Prestes vnto God his father be glory and dominion for ever more. Amen. (aiōn g165)
akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
7 Beholde he commeth with cloudes and all eyes shall se him: and they also which peersed him. And all kinredes of ye erth shall wayle. Even so. Amen.
Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
8 I am Alpha and Omega the begynninge and the endinge sayth the Lorde almyghty which is and which was and which is to come.
“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
9 I Ihon youre brother and companyon in tribulacion and in the kyngdom and pacience which is in Iesu Christe was in the yle of Pathmos for the worde of god and for ye witnessynge of Iesu Christe.
Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
10 I was in the sprete on a sondaye and herde behynde me a gret voyce as it had bene of a trompe
Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
11 sayinge: I am Alpha and Omega the fyrst and the laste. That thou seist write in a boke and sende it vnto the congregacions which are in Asia vnto Ephesus and vnto Smyrna and vnto Pargamos and vnto Thiatira and vnto Sardis and vnto Philadelphia and vnto Laodicia.
Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
12 And I turned backe to se the voyce that spake to me. And when I was turned: I sawe. vii golde candelstyckes
Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
13 and in the myddes of the cadelstyckes one lyke vnto ye sone of ma clothed with a lynnen garmet doune to the ground and gyrd aboute the pappes with a golden gyrdle
na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
14 His heed and his heares were whyte as whyte woll and as snowe: and his eyes were as a flame of fyre:
Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
15 and his fete lyke vnto brasse as though they brent in a fornace: and his voyce as the sounde of many waters.
miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
16 And he had in his right honde vii. starres. And out of his mouth wet a sharpe twoo edged swearde. And his face shone eve as the sonne in his strength.
Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
17 And when I sawe him I fell at his fete even as deed. And he layde hys ryght honde apon me sayinge vnto me: feare not. I am the fyrst and the laste
Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
18 and am alyve and was deed. And beholde I am alyve for ever more and have the kayes of hell and of deeth. (aiōn g165, Hadēs g86)
Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 wryte therfore the thynges which thou haste sene and the thynges which are and the thynges which shalbe fulfylled hereafter:
Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
20 and ye mystery of the vii. starres which thou sawest in my ryght honde and the vii. golden candelstyckes. The vii. stares are the messengers of the vii. congregacios: And the vii. candlestyckes which thou sawest are the vii. congregacions.
Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.

+ Revelation 1 >