< Revelation 2 >

1 Unto the messenger of the congregacion of Ephesus wryte: These thynges sayth he that holdeth the vii. starres in his right honde and walketh in the myddes of the vii. golden candlestyckes
“Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
2 I knowe thy workes and thy labour and thy pacience and howe thou cannest not forbeare the which are evyll: and examinedst them which saye they are Apostles and are not: and hast founde them lyars
Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
3 and dydest wasshe thy self. And hast pacience: and for my names sake hast labored and hast not faynted.
Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
4 Neverthelesse I have sumwhat agaynst the for thou haste lefte thy fyrst love.
Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
5 Remember therfore from whence thou art fallen and repent and do the fyrst workes. Or elles I wyll come vnto the shortly and will remove thy candlestyke out of his place excepte thou repent.
Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
6 But this thou haste because thou hatest ye dedes of the Nicolaitans which dedes I also hate.
Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
7 Lett him yt hath eares heare what ye sprete sayth vnto the congregacions. To him that overcometh will I geve to eate of the tree of lyfe which is in the myddes of ye paradice of god.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
8 And vnto the angell of the congregacion of Smyrna wryte: These thynges sayth he that is fyrst and the laste which was deed and is alive.
“Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
9 I knowe thy workes and tribulacion and poverte but thou art ryche: And I knowe the blaspemy of them whiche call them selves Iewes and are not: but are the congregacio of sathan.
Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
10 Feare none of thoo thynges which thou shalt soffre. Beholde the devyll shall caste of you into preson to tempte you and ye shall have tribulacion. x. dayes. Be faythfull vnto the deeth and I will geve the a croune of lyfe.
Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
11 Let him that hath ears heare what the sprete sayth to the congregacions: He that overcometh shall not be hurte of the seconde deeth.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
12 And to the messenger of the congregacion in Pergamos wryte: This sayth he which hath ye sharpe swearde with two edges.
“Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
13 I knowe thy workes and where thow dwellest evyn where Sathans seat ys and thou kepest my name and hast not denyed my fayth. And in my dayes Antipas was a faythfull witnes of myne which was slayne amonge you where sathan dwelleth.
Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
14 But I have a fewe thynges agaynst the: yt thou hast there they that mayntayne the doctryne of Balam which taught in balake to put occasion of syn before the chylderne of Israhell that they shulde eate of meate dedicat vnto ydoles and to commyt fornicacion.
Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
15 Even so hast thou them that mayntayne the doctryne of the Nicolaytans which thynge I hate.
Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
16 But be converted or elles I will come vnto the shortly and will fyght agaynste the with thes wearde of my mouth
Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
17 Lett him that hath eares heare what the sprete sayth vnto the congregacios: To him that overcommeth will I geve to eate manna that is hyd and will geve him a whyte stone and in the stone a newe name wrytten which no ma knoweth savinge he that receaveth it.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
18 And vnto the messenger of the congregacion of Theatira write: This sayth the sonne of god which hath his eyes lyke vnto a flame of fyre whose fete are like brasse:
“Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
19 I knowe thy workes and thy love service and fayth and thy paciece and thy dedes which are mo at the last then at the fyrste.
Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
20 Notwitstondinge I have a feawe thynges agaynst the that thou sofferest that woman Iesabell which called her sylfe a prophetes to teache and to deceave my servauntes to make them commyt fornicacion and to eate meates offered vppe vnto ydoles.
Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
21 And I gave her space to repent of her fornicacion and she repented not.
Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
22 Beholde I will caste her into a beed and them yt commyt fornicacion wt her into gret adversite excepte they tourne fro their deades.
Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
23 And I will kyll her children with deeth. And all the congregacions shall knowe that I am he which searcheth ye reynes and hertes. And I will geve vnto evere one of you accordynge vnto youre workes.
Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
24 Vnto you I saye and vnto other of them of Thiatyra as many as have not this lerninge and which have not knowen the depnes of Satha (as they saye) I will put apo you none other burthe
“Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
25 but yt which ye have alreddy. Holde fast tyll I come
Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
26 and whosoever overcometh and kepeth my workes vnto the ende to hym will I geve power over nacios
“Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
27 and he shall rule them with a rodde of yron: and as the vessels of a potter shall he breake them to shevers. Eve as I receaved of my father
Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
28 eue so will I geve him ye mornynge starre.
Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
29 Let him yt hath eares heare what the sprete sayth to the congregacions.
“Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!

< Revelation 2 >