< Matthew 23 >

1 Then spake Iesus to the people and to his disciples
Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
2 sayinge. The Scribes and the Pharises sit in Moses seate.
“Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
3 All therfore whatsoever they byd you observe that observe and do: but after their workes do not:
Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
4 For they saye and do not. Ye and they bynde hevy burthes and grevous to be borne and ley the on menes shulders: but they themsylfes will not heave at them with one of their fyngers.
Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
5 All their workes they do for to be sene of me. They set abroade their philateries and make large borders on there garmetes
Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
6 and love to sit vppermooste at feastes and to have the chefe seates in the synagoges
Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
7 and gretinges in the marketes and to be called of men Rabi.
Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
8 But ye shall not suffre youre selves to be called Rabi. For one is youre master that is to wyt Christ and all ye are brethre.
Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
9 And call no man youre father vpon the erth for there is but one youre father and he is in heven.
Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
10 Be not called masters for there is but one youre master and he is Christ.
Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
11 He that is greatest amoge you shalbe youre seruaunte.
Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
12 But whosoever exalteth himsilfe shalbe brought lowe. And he yt hubleth himsilfe shalbe exalted.
Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
13 Wo be vnto you Scribes and Pharises ypocrites for ye shutte vp the kyngdome of heve before men: ye youre selves goo not in nether suffre ye them that come to enter in.
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
14 Wo be vnto you Scribes and Pharises ypocrites: ye devoure widdowes houses and that vnder a coloure of praying longe prayers: wherfore ye shall receave greater damnacion.
Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
15 Wo be vnto you Scribes and Pharises ypocrites which compasse see and londe to bringe one in to youre belefe: and when he ys brought ye make him two folde more the chylde of hell then ye youre selves are. (Geenna g1067)
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe. (Geenna g1067)
16 Wo be vnto you blynd gides which saye whosoever sweare by the teple it is no thinge: but whosoever sweare by the golde of the temple he offendeth.
“Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
17 Ye foles and blinde? whether is greater the golde or the teple that sanctifieth ye golde.
Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18 And whosoever sweareth by the aulter it is nothinge: but whosoever sweareth by ye offeringe yt lyeth on ye aultre offendeth.
Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
19 Ye foles and blinde: whether is greater ye offeringe or ye aultre which sanctifieth ye offeringe?
Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
20 Whosoever therfore sweareth by ye aultre sweareth by it and by all yt there on is.
Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
21 And whosoever sweareth by the teple sweareth by it and by hym yt dwelleth therin.
Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
22 And he that sweareth by heve swereth by the seate of God and by hym that sytteth theron.
Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
23 Wo be to you Scribes and Pharises ypocrites which tythe mynt annyse and comen and leave the waygthtyer mattres of ye lawe vndone: iudgemet mercy and fayth. These ought ye to have done and not to have left the othre vndone.
Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
24 Ye blinde gydes which strayne out a gnat and swalowe a cammyll.
Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
25 Wo be to you scribes and pharises ypocrites which make clene ye vtter syde of the cuppe and of the platter: but within they are full of brybery and excesse.
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
26 Thou blinde Pharise clense fyrst the outsyde of the cup and platter that the ynneside of them maye be clene also.
Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
27 Wo be to you Scribe and Pharises ypocrite for ye are lyke vnto paynted tombes which appere beautyfull outwarde: but are wt in full of deed bones and of all fylthynes.
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
28 So are ye for outwarde ye appere righteous vnto me when within ye are full of ypocrisie and iniquite.
Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29 Wo be vnto you Scribes and Pharises ypocrites: ye bylde the tombes of the Prophetes and garnisshe the sepulchres of the righteous
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
30 and saye: Yf we had bene in the dayes of oure fathers we wolde not have bene parteners with them in the bloud of the Prophetes.
Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
31 So then ye be witnesses vnto youre selfes that ye are the chyldren of them which killed the prophetes.
Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
32 Fulfill ye lyke wyse the measure of youre fathers.
Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
33 Yee serpentes and generacion of vipers how shuld ye scape ye dapnacio of hell? (Geenna g1067)
Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu? (Geenna g1067)
34 Wherfore beholde I sende vnto you prophetes wyse men and scribes and of the ye shall kyll and crucifie: and of the ye shall scourge in youre synagoges and persecute from cyte to cyte
Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
35 that vpon you maye come all the righteous bloude that was sheed vpon the erth fro the bloud of righteous Abell vnto ye bloud of zacharias the sonne of Barachias who ye slewe betwene the teple and ye altre.
Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
36 Verely I say vnto you all these thinges shall light vpon this generacion.
Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
37 Hierusalem hierusalem which kyllest prophetes and stonest the which are sent to the: how often wolde I have gadered thy chyldren to gether as the henne gadreth her chickes vnder her winges but ye wolde not:
“Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
38 Beholde youre habitacio shalbe lefte vnto you desolate.
Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
39 For I saye to you ye shall not se me heceforthe tyll that ye saye: blessed is he that cometh in the name of ye Lorde.
Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”

< Matthew 23 >