< Matthew 27 >

1 When the mornynge was come all ye chefe prestes and the elders of ye people helde a counsayle agenst Iesu to put him to deeth
Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
2 and brought him bounde and delivered him vnto Poncius Pilate the debite.
Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
3 Then when Iudas which betrayed him sawe that he was condempned he repented him sylfe and brought ageyne the. xxx. plattes of sylver to ye chefe prestes and elders
Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
4 sayinge: I have synned betrayinge the innocent bloud. And they sayde: what is that to vs? Se thou to that.
Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
5 And he cast doune the sylver plattes in the temple and departed and went and hounge him sylfe.
Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
6 And the chefe prestes toke the sylver plattes and sayd: it is not lawfull for to put them in to the treasury because it is the pryce of bloud.
Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
7 And they toke counsell and bought with them a potters felde to bury strangers in.
Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8 Wherfore that felde is called the felde of bloud vntyll this daye.
Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
9 Then was fulfylled that which was spoken by Ieremy the Prophet sayinge: and they toke. xxx. sylver plattes the prise of him that was valued whom they bought of the chyldren of Israel
Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
10 and they gave them for the potters felde as the Lorde appoynted me.
wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
11 Iesus stode before the debite: and the debite axed him sayinge: Arte thou the kynge of ye Iues? Iesus sayd vnto him: Thou sayest
Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
12 and when he was accused of ye chefe prestes and elders he answered nothinge.
Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
13 Then sayd Pilate vnto him: hearest thou not how many thinges they laye ageynste ye?
Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
14 And he answered him to never a worde: in so moche that the debite marveylled greatlie.
Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
15 At that feest the debite was wonte to deliver vnto ye people a presoner whom they wolde desyer.
Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
16 He had then a notable presoner called Barrabas.
Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
17 And when they were gadered together Pilate sayde vnto the: whether wyll ye that I geve losse vnto you Barrabas or Iesus which is called Christ?
Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
18 For he knewe well that for envie they had delivred him.
Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
19 When he was set doune to geve iudgemet his wyfe sent to him sayinge: have thou nothinge to do with that iuste man. For I have suffered many thinges this daye in a dreame about him.
Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
20 But the chefe preestes and the elders had parswaded the people that they shulde axe Barrabas and shulde destroye Iesus.
Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
21 Then the debite answered and sayde vnto them: whether of the twayne wyll ye that I let loosse vnto you? And they sayde Barrabas.
Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
22 Pilate sayde vnto them: what shall I do then with Iesus which is called Christ? They all sayde to him: let him be crucified.
Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
23 Then sayde the debite: what evyll hath he done? And they cryed the more sayinge: let him be crucified.
Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
24 When Pilate sawe that he prevayled nothinge but that moare busines was made he toke water and wasshed his hondes before ye people sayinge: I am innocent of the bloud of this iuste person and that ye shall se.
Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
25 Then answered all the people and sayde: his bloud be on vs and on oure chyldren.
Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
26 Then let he Barrabas loose vnto them and scourged Iesus and delivered him to be crucified.
Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
27 Then the soudeours of the debite toke Iesus vnto the comen hall and gaddered vnto him all the company.
Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
28 And they stripped him and put on him a purpyll roobe
Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
29 and platted a croune of thornes and put vpon his heed and a rede in his ryght honde: and bowed their knees before him and mocked him saying: hayle kinge of the Iewes:
Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
30 and spitted vpon him and toke the rede and smoote him on the heed.
Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
31 And when they had mocked him they toke the robe of him ageyne and put his awne reymet on him and leed him awaye to crucify him.
Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
32 And as they came out they fonnde a man of Cyren named Simon: him they compelled to beare his crosse.
Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
33 And whe they cam vnto ye place called Golgotha (that is to saye a place of deed mens sculles)
Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
34 they gave him veneger to drinke mengled with gall. And when he had tasted therof he wolde not drinke.
wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
35 When they had crucified him they parted his garmentes and did cast lottes: to fulfyll that was spoken by the prophet. They deuyded my garmetes amonge them: and apon my vesture did cast loottes.
Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
36 And they sate and watched him there.
Wakaketi, wakawa wanamchunga.
37 And they set vp over his heed the cause of his deeth written. This is Iesus the kynge of the Iewes.
Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
38 And ther were two theves crucified with him one on ye right honde and another on the lyfte.
Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
39 They that passed by revyled him waggynge ther heeddes
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
40 and sayinge: Thou that destroyest the temple of God and byldest it in thre dayes save thy sylfe. If thou be ye sonne of God come doune from the crosse.
“Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
41 Lykwyse also the hye prestes mockinge him with the scribes aud elders sayde:
Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
42 He saved other him sylfe he can not save. If he be ye kynge of Israel: let him now come doune from the crosse and we will beleve him.
“Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
43 He trusted in God let him deliver him now yf he will have him: for he sayde I am the sonne of God.
Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
44 That same also the theves which were crucified with him cast in his tethe.
Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
45 From the sixte houre was there dercknes over all the londe vnto the nynth houre.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
46 And about ye nynth houre Iesus cryed with a loude voyce sayinge: Eli Eli lama asbathani. That is to saye my God my God why hast thou forsaken me?
Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
47 Some of them that stode there when they herde that sayde: This man calleth for Helyas.
Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
48 And streyght waye one of them ranne and toke a sponge and filled it full of veneger and put it on a rede and gave him to drinke.
Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
49 Other sayde let be: let vs se whyther Helyas will come and deliver him.
Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
50 Iesus cryed agayne with a lowde voyce and yelded vp the goost.
Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
51 And beholde the vayle of the temple dyd rent in twayne from ye toppe to the bottome and the erth dyd quake and the stones dyd rent
Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52 and graves dyd open: and the bodies of many sainctes which slept arose
makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
53 and came out of ye graves after his resurreccion and came into the holy cite and appered vnto many.
nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
54 When the Centurion and they that were with him watchinge Iesus sawe ye erth quake and those thinges which hapened they feared greatly sayinge. Of a surete this was the sonne of God.
Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
55 And many wemen were there beholdinge him a farre of which folowed Iesus fro Galile ministringe vnto him.
Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
56 Amonge which was Mary Magdalen and Mary the mother of Iames and Ioses and ye mother of zebedes chyldren.
Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
57 When the even was come there came a ryche man of Aramathia named Ioseph which same also was Iesus disciple.
Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58 He went to Pilate and begged the body of Iesus. Then Pilate commaunded the body to be delivered.
Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
59 And Ioseph toke the body and wrapped it in a clene lynnyn clooth
Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
60 and put it in his newe tombe which he had hewen out even in the roke and rolled a greate stone to the dore of ye sepulcre and departed.
akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
61 And there was Mary Magdalene and the other Mary sittynge over ageynste the sepulcre.
Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
62 The nexte daye that foloweth good frydaye the hye prestes and pharises got them selves to Pilate
Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
63 and sayde: Syr we remember yt this deceaver sayde whyll he was yet alyve After thre dayes I will aryse agayne.
Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64 Commaunde therfore that the sepulcre be made sure vntyll ye thyrd daye lest paraventure his disciples come and steale him awaye and saye vnto the people he is rysen from deeth and the laste erroure be worsse then the fyrst.
Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
65 Pilate sayde vnto them. Take watche men: Go and make it as sure as ye can.
Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
66 And they went and made the sepulcre sure with watche men and sealed the stone.
Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.

< Matthew 27 >