< Matthew 19 >

1 And it came to passe when Iesus had fynisshed those sayinges he gat him from Galile and came into the coostes of Iewry beyonde Iordan
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, alitoka Galilaya, akaenda katika mkoa wa Yudea, ng'ambo ya mto Yordani.
2 and moche people folowed him and he healed them theare.
Watu wengi walimfuata huko, naye akawaponya.
3 Then came vnto him the pharises temtinge him and sayinge to him: Ys it lawfull for a man to put awaye his wyfe for all maner of causes?
Mafarisayo kadhaa walimjia, wakamwuliza kwa kumtega, “Je, ni halali mume kumpa talaka mkewe kwa kisa chochote?”
4 He answered and sayd vnto them: Have ye not redde how that he which made man at the beginninge made them man and woman
Yesu akawajibu, “Je, hamkusoma katika Maandiko Matakatifu kwamba Mungu aliyemuumba mtu tangu mwanzo alimfanya mwanamume na mwanamke,
5 and sayde: for this thinge shall a ma leve father and mother and cleve vnto his wyfe and they twayne shalbe one flesshe.
na akasema: Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?
6 Wherfore now are they not twayne but one flesshe. Let not man therfore put a sunder that which God hath cuppled to gedder.
Kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikitenganishe.”
7 The sayde they to him: why did Moses comaunde to geve a testimoniall of divorsemet and to put hyr awaye?
Lakini wao wakamwuliza, “Kwa nini basi, Mose alituagiza mwanamke apewe hati ya talaka na kuachwa?”
8 He sayde vnto them: Moses because of the hardnes of youre hertes suffred you to put awaye youre wyfes: But from ye beginnynge it was not so.
Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
9 I saye therfore vnto you whosoever putteth awaye his wyfe (except it be for fornicacion) and maryeth another breaketh wedlocke. And whosoever maryeth her which is divorsed doeth commyt advoutry.
Lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo. Basi nawaambieni, yeyote atakayemwacha mke wake isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, akaoa mke mwingine, anazini.”
10 Then sayde his disciples to him: yf the mater be so betwene man and wyfe then is it not good to mary.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Ikiwa mambo ya mume na mkewe ni hivyo, ni afadhali kutooa kabisa.”
11 He sayde vnto them: all me can not awaye with that sayinge save they to whom it is geve.
Yesu akawaambia, “Si wote wanaoweza kulipokea fundisho hili, isipokuwa tu wale waliojaliwa na Mungu.
12 Ther are chaste which were so borne out of their mothers belly. And ther are chaste which be made of men. And ther be chaste which have made them selves chaste for the kyngdome of heves sake. He that can take it let him take it.
Maana kuna sababu kadhaa za kutoweza kuoa: wengine ni kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine kwa sababu wamefanywa hivyo na watu, na wengine wameamua kutooa kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee.”
13 Then were brought to him yonge chyldre that he shuld put his hondes on them and praye And the disciples rebuked them.
Kisha watu wakamletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono na kuwaombea. Lakini wanafunzi wakawakemea.
14 But Iesus sayde: suffre the chyldren and forbid them not to come to me: for of suche is the kyngdome of heven.
Yesu akasema, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie; maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu walio kama watoto hawa.”
15 And when he had put his hondes on them he departed thence.
Basi, akawawekea mikono, kisha akaondoka mahali hapo.
16 And beholde one came and sayde vnto him: good master what good thinge shall I do that I maye have eternall lyfe? (aiōnios g166)
Mtu mmoja alimjia Yesu, akamwuliza, “Mwalimu, nifanye kitu gani chema ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
17 He sayde vnto him: why callest thou me good? there is none good but one and that is God. But yf thou wylt entre in to lyfe kepe the commaundementes.
Yesu akamwambia, “Mbona unaniuliza kuhusu jambo jema? Kuna mmoja tu aliye mwema. Ukitaka kuingia katika uzima, shika amri.”
18 The other sayde to him Which? And Iesus sayde: breake no wedloke kill not steale not: beare not falce witnes:
Yule mtu akamwuliza, “Amri zipi?” Yesu akasema, “Usiue, usizini, usiibe, usitoe ushahidi wa uongo,
19 honoure father and mother: and love thyne neighbour as thy sylfe.
waheshimu baba yako na mama yako; na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
20 And the younge man sayde vnto him: I have observed all these thingis from my youth what lacke I yet?
Huyo kijana akamwambia, “Hayo yote nimeyazingatia tangu utoto wangu; sasa nifanye nini zaidi?”
21 And Iesus sayde vnto him yf thou wylt be perfecte goo and sell that thou hast and geve it to the povre and thou shalt have treasure in heven and come and folowe me.
Yesu akamwambia, “Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako uwape maskini hiyo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.”
22 When ye younge ma hearde yt sayinge he wet awaye mourninge. For he had greate possessions.
Huyo kijana aliposikia hayo, alienda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi.
23 Then Iesus sayde vnto his disciples: Verely I saye vnto you: yt is harde for a ryche ma to enter into ye kyngdome of heaven.
Hapo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kweli nawaambieni, itakuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.
24 And moreover I saye vnto you: it is easier for a camell to go through the eye of a nedle then for a ryche man to enter into the kyngdome of God.
Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.”
25 When his disciples hearde that they were excedingly amased sayinge: who then can be saved?
Wale wanafunzi waliposikia hivyo walishangaa, wakamwuliza, “Ni nani basi, awezaye kuokoka?”
26 Iesus behelde the and sayde vnto them: with men this is vnpossible but with God all thinges are possible.
Yesu akawatazama, akasema, “Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
27 Then answered Peter and sayde to him: Beholde we have forsaken all and folowed the what shall we have?
Kisha Petro akasema, “Na sisi je? Tumeacha yote tukakufuata; tutapata nini basi?”
28 Iesus sayde vnto them: verely I saye to you: when the sonne of man shall syt in ye seate of his maieste ye which folowe me in ye seconde generacion shall syt also vpon. xii. seates and iudge ye. xii. tribes of Israel.
Yesu akawaambia, “Nawaambieni kweli, Mwana wa Mtu atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake katika ulimwengu mpya, ninyi mlionifuata mtaketi katika viti kumi na viwili mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
29 And whosoever forsaketh housses or brethren or systers other father or mother or wyfe or chyldren or landes for my names sake ye same shall receave an hundred folde and shall inheret everlastynge lyfe. (aiōnios g166)
Na kila aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi, na kupata uzima wa milele. (aiōnios g166)
30 Many that are fyrste shalbe laste and the laste shalbe fyrste.
Lakini walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.

< Matthew 19 >