< Matthew 17 >

1 And after. vi. dayes Iesus toke Peter and Iames and Ihon his brother and brought them vp into an hye mountayne out of the waye
Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu.
2 and was transfygured before them: and his face did shyne as the sunne and his clothes were as whyte as the light.
Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3 And beholde ther appered vnto the Moses and Helyas talkinge with him.
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
4 Then answered Peter and sayde to Iesus: master here is good beinge for vs. If thou wylt leet vs make here. iii. tabernacles one for the and one for Moses and one for Helyas.
Hapo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.”
5 Whyll he yet spake beholde a bright cloude shadowed them. And beholde there came a voyce out of ye cloude sayinge: this is my deare sonne in whom I delite heare him.
Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni.”
6 And when the disciples hearde that they fell on their faces and were soore afrayed.
Wanafunzi waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
7 And Iesus came and touched them and sayde: aryse and be not afrayed.
Yesu akawaendea, akawagusa, akasema, “Simameni, msiogope!”
8 And when they looked vp they saw no man saue Iesus onely.
Walipoinua macho yao hawakumwona mtu, ila Yesu peke yake.
9 And as they came doune from the mountayne Iesus charged them sayinge: se yt ye shewe the vision to no man vntyll the sonne of man be rysen ageyne from deeth.
Basi, walipokuwa wanashuka mlimani, Yesu akawaonya: “Msimwambie mtu mambo mliyoyaona mpaka Mwana wa Mtu atakapofufuliwa kutoka wafu.”
10 And his disciples axed of him sayinge: Why then saye the scribes yt Helyas muste fyrst come?
Kisha wanafunzi wakamwuliza, “Mbona walimu wa Sheria wanasema ati ni lazima kwanza Eliya aje?”
11 Iesus answered and sayd vnto them: Helyas shall fyrst come and restore all thinges.
Yesu akawajibu, “Kweli, Eliya atakuja kutayarisha mambo yote.
12 And I saye vnto you yt Helyas is come alredy and they knewe him not: but have done vnto him whatsoever they lusted. In lyke wyse shall also the sonne of man suffre of the.
Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja nao hawakumtambua, bali walimtendea jinsi walivyotaka. Mwana wa Mtu atateswa vivyo hivyo mikononi mwao.”
13 Then ye disciples perceaved that he spake vnto them of Ihon baptist.
Hapo hao wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohane mbatizaji.
14 And when they were come to ye people ther cam to him a certayne man and kneled doune to him and sayde:
Walipojiunga tena na ule umati wa watu, mtu mmoja alimwendea Yesu, akampigia magoti,
15 Master have mercy on my sonne for he is franticke: and is sore vexed. And oft tymes he falleth into the fyre and oft into ye water
akasema, “Mheshimiwa, mwonee huruma mwanangu kwa kuwa ana kifafa, tena anateseka sana; mara nyingi yeye huanguka motoni na majini.
16 And I brought him to thy disciples and they coulde not heale him.
Nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumponya.”
17 Iesus answered and sayde: O generacion faythles and croked: how longe shall I be with you? how longe shall I suffre you? bring him hidder to me.
Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia ninyi mpaka lini? Mleteni hapa huyo mtoto.”
18 And Iesus rebuked the devyll and he ca out of him. And ye child was healed even yt same houre.
Basi, Yesu akamkemea huyo pepo, naye akamtoka, na yule mtoto akapona wakati huohuo.
19 Then came the disciples to Iesus secretly and sayde: Why could not we cast him out?
Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha, wakamwuliza, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo?”
20 Iesus sayd vnto the: Because of youre vnbelefe For I saye veryly vnto you: yf ye had faythe as a grayne of musterd seed ye shuld saye vnto this moutayne remove hence to yonder place and he shuld remove: nether shuld eny thinge be vnpossible for you to do.
Yesu akawajibu, “Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, hata iwe ndogo kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: Toka hapa uende pale, nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu.”
21 How be it this kynde goeth not oute but by prayer and fastinge.
“Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga.”
22 As they passed the tyme in Galile Iesus sayde vnto them: the sonne of man shalbe betrayed into the hondes of men
Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, “Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.
23 and they shall kill him and the thyrd daye he shall ryse agayne. And they sorowed greatly.
Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa.” Wanafunzi wakahuzunika mno.
24 And when they were come to Capernau they yt were wont to gadre poll money came to Peter and sayde: Doth youre master paye tribute?
Walipofika Kafarnaumu watu wenye kukusanya fedha ya zaka ya Hekalu walimwendea Petro, wakamwuliza, “Je, mwalimu wenu hulipa fedha ya zaka?”
25 He sayd: ye. And when he was come into the house Iesus spake fyrst to him saying What thinkest thou Simon? of whome do ye kynges of the erth take tribute or poll money? of their chyldren or of straungers?
Petro akajibu, “Naam, hulipa.” Basi, Petro alipoingia ndani ya nyumba, kabla hata hajasema neno, Yesu akamwuliza, “Simoni, wewe unaonaje? Wafalme wa dunia hukusanya ushuru au kodi kutoka kwa kina nani? Kutoka kwa wananchi ama kutoka kwa wageni?”
26 Peter sayde vnto him: of straungers. Then sayd Iesus vnto him agayne: Then are the chyldren fre.
Petro akajibu, “Kutoka kwa wageni.” Yesu akamwambia, “Haya basi, wananchi hawahusiki.
27 Neverthelesse lest we shuld offende the: goo to ye see and cast in thyne angle and take the fysshe yt fyrst cometh vp: and when thou hast opened his mouthe thou shalt fynde a pece of twentie pence: yt take and paye for me and the.
Lakini kusudi tusiwakwaze, nenda ziwani ukatupe ndoana; chukua samaki wa kwanza atakayenaswa, fungua kinywa chake, na ndani utakuta fedha taslimu ya zaka. Ichukue ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako.”

< Matthew 17 >