< Mark 5 >

1 And they cam over to the other syde of ye see in to the coutre of ye Gaderenites.
Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2 And when he was come out of ye shippe there met him out of the graves a man possessyd of an vncleane sprete
Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3 which had his abydinge amoge the graves. And no man coulde bynde him: no not with cheynes
Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4 because that when he was often bounde wt fetters and cheynes he plucked ye chaynes asundre and brake the fetters in peaces. Nether coulde eny man tame him.
Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5 And alwayes bothe nyght and daye he cryed in ye moutaynes and in ye graves and bet himsilfe wt stones.
Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6 When he had spied Iesus afarre of he rane and worshipped him
Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7 and cryed wt a lowde voyce and sayde: what have I to do wt the Iesus ye sonne of the moost hyest God? I requyre ye in the name of God yt thou tormet me not.
akisema kwa sauti kubwa, “Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!”
8 For he had sayd vnto hym: come out of the man thou fowle sprete.
(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.”)
9 And he axed him: what is thy name? And he answered sayinge: my name is Legion for we are many.
Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Naye akajibu, “Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi.”
10 And he prayd him instantly that he wolde not sende the awaye out of the countre.
Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11 And ther was there nye vnto ye moutayns a greate heerd of swyne fedinge
Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12 and all the devyls besought him sayinge: sende vs into the heerde of swyne yt we maye enter in to them.
Basi, hao pepo wakamsihi, “Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie.”
13 And anone Iesus gave them leave. And the vnclene spretes wet out and entred into ye swyne. And the heerd starteled and ran hedling into the see. They were about. ii. M. swyne and they were drouned in the see.
Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14 And the swyne heerdes fleed and tolde it in ye cyte and in the countre. And they came out for to se what had hapened:
Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15 and came to Iesus and sawe hym that was vexed wt the fende and had the legio syt both clothed and in his right mynde and were afrayed.
Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16 And they that sawe it tolde them how it had happened vnto him that was possessed with the devyll: and also of the swyne.
Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17 And they begane to praye him that he wolde departe fro their coostes.
Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18 And when he was come in to the shyppe he that had ye devyll prayed him that he myght be with him.
Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19 Howbeit Iesus wolde not suffre him but sayde vnto him: goo home in to thyne awne housse and to thy frendes and shewe the what great thinges ye Lorde hath done vnto the and how he had copassion on the.
Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma.”
20 And he departed and begane to publisshe in ye ten cyties what greate thinges Iesus had done vnto him and all me dyd merveyle.
Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21 And when Iesus was come over agayne by shyp vnto the other syde moche people gadered vnto him and he was nye vnto the see.
Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22 And beholde ther came one of the rulers of ye Synagoge whose name was Iairus: and when he sawe him he fell doune at his fete
Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23 and besought hym greatly sayinge: my doughter lyith at poynt of deeth I wolde thou woldest come and laye thy honde on her that she myght be safe and live.
akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi.”
24 And he wet with him and moche people folowed him and thronged him.
Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25 And ther was a certen woman which was diseased of an yssue of bloude. xii. yeres
Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26 and had suffred many thinges of many phisicios and had spet all yt she had and felte none amendmet at all but wexed worsse and worsse.
Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27 When she had herde of Iesus: she came into the preace behynde him and touched his garmet.
Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28 For she thought: yf I maye but touche his clothes I shall be whole.
Alifanya hivyo, maana alijisemea, “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
29 And streyght waye her foutayne of bloude was dryed vp aud she felt in her body that she was healed of the plage.
Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30 And Iesus immediatly felt in him silfe ye vertue that wet out of him and tourned him roude aboute in the preace and sayde: who touched my clothes?
Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, “Nani aliyegusa mavazi yangu?”
31 And his disciples sayde vnto him: seist thou ye people thrust the and yet axest who dyd touche me?
Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?”
32 And he loked roud about for to se her that had done that thinge.
Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33 The woman feared and trembled (for she knew what was done with in her) and she came and fell doune before him and tolde him ye truth of everythinge.
Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34 And he sayde to her: Doughter thy fayth hath made the whoale: goo in peace and be whole of thy plage.
Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
35 Whyll he yet spake ther came fro the ruler of ye synagoges housse certayne which sayde: thy doughter is deed: why diseasest thou ye master eny further?
Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
36 Assone as Iesus herde that worde spoke he sayde vnto the ruler of ye synagoge: be not afrayed only beleve.
Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, “Usiogope, amini tu.”
37 And he suffred no man to folowe him moo then Peter and Iames and Ihon the brother of Iames.
Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38 And he came vnto the housse of the ruler of ye synagoge and sawe ye wondrynge and them that wepte and wayled greatly
Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39 and went in and sayde vnto them: why make ye this adoo and wepe? The mayde is not deed but slepith.
Akaingia ndani, akawaambia, “Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu.”
40 And they lawght him to scorne. Then he put them all out and toke ye father and the mother of ye mayden and them that were with him and entred in where the mayden laye
Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41 and toke the mayden by the honde and sayde vnto hyr: Tabitha cumi: which is by interpretacion: mayde I saye vnto the aryse.
Kisha akamshika mkono, akamwambia, “Talitha, kumi,” maana yake, “Msichana, nakwambia, amka!”
42 And streyght the mayden arose and went on her fete. For she was of the age of twelve yeres. And they were astonied at it out of measure.
Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43 And he charged the straytely that no man shuld knowe of it and comaunded to geve her meate.
Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.

< Mark 5 >