< Mark 15 >

1 And anone in ye dawnynge the hye prestes helde counsell wt ye elders and ye scribes and ye whoole cogregacion and bounde Iesus and ledde him awaye and delivered him to Pilate.
Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2 And Pilate axed him: arte thou the kynge of the Iewes? And he answered and sayde vnto him: thou sayest it.
Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 And the hye prestes accused him of many thinges.
Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4 Wherfore Pilate axed him agayne sayinge: Answerest thou nothinge? Beholde how many thinges they lay vnto thy charge.
Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
5 Iesus yet answered never aworde so that Pilate merveled.
Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6 At that feast Pilate was wont to delivre at their pleasure a presoner: whomsoever they wolde desyre.
Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7 And ther was one named Barrabas which laye bounde with the that made insurreccion and in the insurreccion comitted murther.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8 And ye people called vnto him and began to desyre accordinge as he had ever done vnto them.
Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9 Pylate answered them and sayd: Will ye that I lowse vnto you the kynge of the Iewes?
Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he knewe that the hye Prestes had delyvered him of envy.
Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11 But the hye prestes had moved the people that he shuld rather delyvre Barrabas vnto them.
Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12 And Pylate answered agayne and sayd vnto the: What will ye then that I do wt him whom ye call ye kynge of ye Iewes?
Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 And they cryed agayne: crucifie him.
Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
14 Pylate sayde vnto them: What evell hath he done? And they cryed ye moore fervently: crucifie him.
Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
15 And so Pylate willinge to content the people lowsed them Barrabas and delyvered Iesus when he had scourged him for to be crucified.
Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16 And the souddeers ledde him awaye into ye commen hall and called togedder the whoole multitude
Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 and they clothed him with purple and they platted a croune of thornes and crouned him with all
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18 and beganne to salute him. Hayle kynge of the Iewes.
Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
19 And they smoote him on the heed wt a rede and spat apon him and kneled doune and worsheped him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20 And when they had moocked him they toke the purple of him and put his awne cloothes on him and ledde him oute to crucifie him.
Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21 And they compelled one that passed by called Symon of Cyrene (which cam oute of the felde and was father of Alexander and Rufus) to beare his crosse.
Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22 And they brought him to a place named Golgotha (which is by interpretacion the place of deed mens scoulles)
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
23 and they gave him to drinke wyne myngled with myrte but he receaved it not.
Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24 And when they had crucified him they parted his garmentes castinge loottes for them what every man shulde have.
Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25 And it was aboute ye thyrde houre and they crucified him.
Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 And the tytle of his cause was wrytten: The kynge of the Iewes.
Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 And they crucified with him two theves: the one on the ryght honde and the other on his lyfte.
Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
28 And the scripture was fulfilled which sayeth: he was counted amonge the wicked.
Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
29 And they that went by rayled on him: waggynge their heedes and sayinge: A wretche that destroyest the temple and byldest it in thre dayes:
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30 save thy sylfe and come doune from the crosse.
Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
31 Lyke wyse also mocked him ye hye preestes amonge them selves with the scribes and sayde: He saved other men him sylfe he cannot save.
Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32 Let Christ the kynge of Israel now descende from the crosse that we maye se and beleve. And they that were crucified with him checked him also.
Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33 And when the sixte houre was come darknes aroose over all the erth vntyll ye nynthe houre.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34 And at the nynthe houre Iesus cryed with a loude voyce sayinge: Eloi Eloi lamaasbathani which is yf it be interpreted: my God my God why hast thou forsaken me?
Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
35 And some of them that stode by when they hearde yt sayde: beholde he calleth for Helyas
Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
36 And one ran and filled a sponge full of veneger and put it on a rede and gave him to drinke sayinge: let him alone let vs se whether Helyas will come and take him doune.
Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
37 But Iesus cryed with aloude voyce and gave vp the gooste.
Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38 And the vayle of the temple dyd rent in two peces from the toppe to the boottome.
Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 And when the Centurion which stode before him sawe that he so cryed and gave vp the gooste he sayd: truly this man was the sonne of God.
Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 Ther were also wemen a good waye of beholdinge him: amonge whom was Mary Magdalen and Mary the mother of Iames the lytle and of Ioses and Mary Salome
Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41 which also when he was in Galile folowed him and ministred vnto him and many other wemen which came vp with him to Hierusalem.
Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42 And now when nyght was come (because it was ye even that goeth before ye saboth)
Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43 Ioseph of Arimathia a noble councelour which also loked for ye kyngdome of God came and went in booldly vnto Pylate and begged ye boddy of Iesu.
Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44 And Pylate merveled that he was alredy deed and called vnto him ye Centurion and axed of him whether he had bene eny whyle deed.
Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45 And when he knewe the trueth of the Centurion he gave ye body to Ioseph.
Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46 And he bought a lynnen cloothe and toke him doune and wrapped him in ye lynnen cloothe and layde him in a tombe yt was hewen oute of ye rocke and rolled a stone vnto the doze of the sepulcre.
Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47 And Mary Magdalen and Mary Ioses beheld where he was layde.
Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.

< Mark 15 >