< Luke 4 >

1 Iesus then full of the holy goost returnyd fro Iordan and was caryed of ye sprete into wildernes
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 and was. xl. dayes tempted of the devyll. And in thoose dayes ate he no thinge. And when they were ended he afterward hongred.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 And the devyll sayde vnto him: yf thou be the sonne of God comaunde this stone yt it be breed.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 And Iesus answered hym sayinge: It is writte: man shall not live by breed only but by every worde of God.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And ye devyll toke him vp into an hye moutayne and shewed him all the kyngdoms of the worlde eve in ye twincklinge of an eye.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 And ye devyll sayde vnto him: all this power will I geve ye every whit and the glory of the: for yt is delyvered to me and to whosoever I will I geve it.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 Yf thou therfore wilt worshippe me they shalbe all thyne.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Iesus answered him and sayde: hence from me Sathan. For it is written: Thou shalt honour the Lorde thy God and him only serve.
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 And he caryed him to Ierusalem and set him on a pynacle of the temple and sayd vnto him: Yf thou be the sonne of God cast thy silfe doune from hens.
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 For it is written he shall geve his angels charge over the to kepe the
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 and with there hondis they shall stey the vp that thou dasshe not thy fote agaynst a stone.
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Iesus answered and sayde to him it is sayd: thou shalt not tempte the Lorde thy God.
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Assone as the devyll had ended all his temptacions he departed from him for a season.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 And Iesus retourned by the power of ye sprete in to Galile and there went a fame of him thorowe oute all the regio roude aboute.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 And he taught in their synagoges and was commended of all men.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 And he came to Nazareth where he was noursed and as hys custome was went in to the synagoge on the Saboth dayes and stode vp for to rede.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 And ther was delyvered vnto him ye boke of ye Prophete Esaias. And when he had opened the boke he founde the place where it was written.
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 The sprete of the lorde vpon me because he hath annoynted me: to preache ye gospell to ye poore he hath sent me: and to heale the broken harted: to preache delyverauce to the captive and sight to the blinde and frely to set at lyberte them that are brused
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 and to preache the acceptable yeare of the Lorde.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 And he cloosed the booke and gave it agayne to the minister and sate doune. And the eyes of all that were in the synagoge were fastened on him.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 And he began to saye vnto them. This daye is this scripture fulfilled in youre eares.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 And all bare him witnes and wondred at the gracious wordes which proceded oute of his mouth and sayde: Is not this Iosephs sonne?
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 And he sayde vnto them: Ye maye very well saye vnto me this proverbe: Phisicion heale thy silfe. Whatsoever we have heard done in Capernaum do the same here lyke wyse in thyne awne countre.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 And he sayde verely I saye vnto you: No Prophet is accepted in his awne countre.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 But I tell you of a truth many wyddowes were in Israell in the dayes of Helias when hevyn was shet thre yeres and syxe monethes when greate fammisshemet was throughoute all the londe
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 and vnto none of them was Helias sent save in to Sarephta besydes Sidon vnto a woma that was a widow.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 And many lepers were in Israel in the tyme of Heliseus the Prophete: and yet none of them was healed savinge Naaman of Siria.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 And as many as were in ye sinagoge when they herde that were filled with wrath:
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 and roose vp and thrust him oute of the cite and ledde him eve vnto the edge of the hill wher on their cite was bilte to cast him doune hedlynge.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 But he went his waye eve thorow the myddes of them:
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 and came in to Capernaum a cyte of Galile and there taught the on the Saboth dayes.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 And they were astonyed at his doctrine: for his preachige was wt power.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 And in the synagoge ther was a ma which had a sprete of an vncleane devell and cryed with aloude voyce
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 sayinge: let me alone what hast thou to do with vs thou Iesus of Nazareth? Arte thou come to destroye vs? I knowe the what thou arte eve the holy of God.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 And Iesus rebuked him sayinge: holde thy peace and come oute of him. And the devyll threwe him in the myddes of them and came oute of him and hurt him not.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 And feare came on them all and they spake amonge them selves sayinge: what maner a thinge is this? For with auctorite and power he commaundeth the foule spretes and they come out?
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 And ye fame of him spreed abroode thorowoute all places of the countre round aboute.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 And he roose vp and came oute of ye sinagoge and entred in to Simons housse. And Simos motherelawe was take with a greate fever and they made intercession to him for her.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 And he stode over her and rebuked the fever: and it leeft her. And immediatly she arose and ministred vnto them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 When the sonne was doune all they that had sicke take with divers deseases brought them vnto him: and he layde his hondes on every one of them and healed them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 And devils also cam out of many of them crying and saying: thou arte Christ the sonne of God. And he rebuked them and suffered them not to speake: for they knewe that he was Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Assone as it was daye he departed and went awaye into a desert place and ye people sought him and came to him and kept him that he shuld not departe from the.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 And he sayde vnto the: I muste to other cities also preache the kyngdome of God: for therfore am I sent.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And he preached in the synagoges of Galile.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luke 4 >