< Luke 3 >

1 In the fiftenthe yeare of the raygne of Tiberius the Emperoure Pontius Pylate beinge leftenaut of Iurie and Herode beinge Tetrach of Galile and his brother Philip Tetrach in Iturea and in the region of Traconites and Lysanias the Tetrach of Abyline
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 when Anna and Cayphas were the hye prestes: the worde of God came vnto Iohn ye sonne of zacharias in the wildernes.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 And he came in to all the coostes aboute Iordan preachynge the baptyme of repentaunce for the remission of synnes
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 at it is written in the boke of the sayinges of Esaias ye Prophet which sayeth: The voyce of a cryar in wyldernes prepare the waye of the Lorde make hys pathes strayght.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 Every valley shalbe fylled and every moutayne and hyll shalbe brought lowe. And crocked thinges shalbe made streight: and the rough wayes shalbe made smoth:
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 and all flesshe shall se the saveour sent of God.
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 Then sayde he to the people that were come to be baptysed of him: O generacion of vipers who hath taught you to flye from the wrath to come?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 Bringe forth due frutes of repentaunce and begynne not to saye in youre selves we have Abraham to oure father. For I saye vnto you: God is able of these stones to reyse vp chyldren vnto Abraham.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 Now also ys the axe leyd vnto the rote of the trees: so yt every tree which bringeth not forth good frute shalbe hewe doune and caste in to ye fyre.
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 And the people axed him sayinge: What shall we do then?
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 He answered and sayde vnto them: He that hath two coottes let him parte with him that hath none: and he that hath meate let him do lyke wyse.
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Then came ther Publicans to be baptised and sayde vnto him: Master what shall we do?
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 And he sayde vnto the: requyre no more then that which ys appoynted vnto you.
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 The soudyoures lyke wyse demaunded of hym sayinge: and what shall we do? And he sayde to them: Do violence to noo ma: nether trouble eny man wrongfully: but be content with youre wages.
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 As the people were in a doute and all men disputed in their hertes of Iohn whether he were very Christ:
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 Ihon answered and sayde to them all: I baptyse you wt water but a stronger then I cometh after me whose shue latchet I am not worthy to vnlouse: he will baptise you with the holy goost and with fyre:
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 which hath his fanne in his hond and will pourge his floore and will gader the corne into his barne: but the chaffe wyll he bourne with fyre that never shalbe quenched.
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 And many other thinges in his exhortacion preached he vnto the people.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 Then Herode the Tetrach (when he was rebuked of him for Herodias his brother Philippes wyfe and for all the evyls which Herod had done)
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 added this above all and leyd Iohn in preson.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 And yt fortuned as all the people receaved baptyme (and when Iesus was baptised and dyd praye) that heave was opened
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 and the holy goost came doune in a bodely shape lyke a dove vpo him and a voyce came fro heve sayinge: Thou arte my dere sonne in the do I delyte.
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 And Iesus him silfe was about thirty yere of age when he begane beinge as men supposed the sonne of Ioseph. which Ioseph was the sonne of Heli
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 which was the sonne of Mathat which was the sonne of Levi: which was the sonne of Melchi: which was the sonne of Ianna: which was the sonne of Ioseph:
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 which was the sonne of Matatthias: which was the sonne of Amos: which was the sonne of Nahum: which was the sonne of Esli: which was the sonne of Nagge:
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 which was the sonne of Maath: which was the sonne of Matathias: which was the sonne of Semei: which was the sonne of Ioseph: which was the sonne of Iuda:
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 which was the sonne of Iohanna: which was the sonne of Rhesya: which was the sonne of zorobabel: which was the sonne of Salathiel: which was the sonne of Neri:
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 which was the sonne of Melchi: which was the sonne of Addi: which was the sonne of Cosam: which was the sonne of Helmadam: which was the sonne of Her:
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 which was the sonne of Ieso: which was the sonne of Helieser: which was the sonne of Ioram: which was the sonne of Mattha: which was the sonne of Levi:
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 which was the sonne of Simeon: which was the sonne of Iuda: which was the sonne of Ioseph: which was the sonne of Ionam: which was the sonne of Heliachim:
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 which was the sonne of Melea: which was the sonne of Menam: which was the sonne of Mathathan: which was the sonne of Nathan: which was the sonne of David:
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 which was the sonne of Iesse: which was the sonne of Obed: which was the sonne of Boos: which was the sonne of Salmon: which was the sonne of Naason:
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 which was the sonne of Aminadab: which was the sonne of Aram: which was the sonne of Esrom: which was the sonne of Phares: which was the sonne of Iuda:
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 which was the sonne of Iacob: which was the sonne of Ysaac: which was the sonne of Abraham: which was the sonne of Tharra: which was the sonne of Nachor:
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 which was the sonne of Saruch: which was the sonne of Ragau: which was the sonne of Phalec: which was the sonne of Heber: which was the sonne of Sala:
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 which was the sonne of Cainan: which was the sonne of Arphaxat: which was the sonne of Sem: which was the sonne of Noe: which was the sonne of Lameth:
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 which was the sonne of Mathusala: which was the sonne of Enoch: which was the sonne of Iareth: which was the sonne of Malalehel. which was the sonne of Cainan:
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 which was the sonne of Enos: which was the sonne of Seth: which was the sonne of Adam: which was the sonne of God.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luke 3 >