< John 8 >

1 And Iesus went vnto mounte Olivete
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Yesu alienda mlima wa Mizeituni.
2 and erly in ye mornynge came agayne into ye temple and all the people came vnto him and he sate doune and taught them.
Mapema asubuhi akaja tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; akakaa na kuwafundisha.
3 And the scribes and ye pharises brought vnto him a woman taken in advoutry and set hyr in the myddes
Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha kuzini. Wakamweka katikati.
4 and sayde vnto him: Master this woman was taken in advoutry even as the dede was a doyng.
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Ndipo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, mwanamke huyu amekamatwa katika uzinzi, katika kitendo kabisa.
5 Moses in the lawe comaunded vs yt suche shuld be stoned. What sayest thou therfore?
Sasa, katika sheria, Musa ametuamuru kuwaponda mawe watu kama hawa, unasemaje juu yake?
6 And this they sayde to tempt him: that they myght have wherof to accuse him. Iesus stouped doune and with his fynger wrote on the grounde.
Walisema haya ili kumtega ili kwamba wapate jambo la kumshitaki, lakini Yesu akainama chini akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
7 And whyll they continued axynge him he lyfte him selfe vp and sayde vnto them: let him yt is amoge you wt out synne cast the fyrst stone at her.
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Walipoendelea kumwuliza, alisimama na kuwaambia, “Yeye asiyekuwa na dhambi miongoni mwenu, awe wa kwanza kumponda mawe.”
8 And agayne he stouped doune and wrote on ye grounde.
Akainama tena chini, akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
9 And assone as they hearde that they went out one by one the eldest fyrst. And Iesus was lefte a lone and the woman stondynge in ye myddes.
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Waliposikia hayo, waliondoka mmoja baada ya mwingine, kuanzia aliye mzee. Mwishowe Yesu aliachwa peke yake, pamoja na mwanamke aliyekuwa katikati yao.
10 When Iesus had lyfte vp him selfe agayne and sawe no man but the woman he sayde vnto hyr. Woman where are those thyne accusars? Hath no man condempned the?
Yesu alisimama na kumwambia, “Mwanamke, waliokushitaki wako wapi? Hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
11 She sayde: No man Lorde. And Iesus sayde: Nether do I condempne the. Goo and synne no moare.
Akasema, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda njia yako; kuanzia sasa na kuendelea usitende dhambi tena.”
12 Then spake Iesus agayne vnto them sayinge: I am the light of the worlde. He that foloweth me shall not walke in darcknes: but shall have the light of lyfe.
Tena Yesu akazungumza na watu akisema, “Mimi ni nuru ya ulimwengu; yeye anifuataye hatatembea gizani bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 The pharises sayde vnto him: thou bearest recorde of thy sylfe thy recorde is not true.
Mafarisayo wakamwambia, “Unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako siyo wa kweli.”
14 Iesus answered and sayde vnto them: Though I beare recorde of my selfe yet my recorde is true: for I knowe whece I came and whyther I goo. But ye cannot tell whece I come and whyther I goo.
Yesu alijibu akawaambia, “Hata kama nitajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli. Ninajua mahali nilikotoka na kule ninakoenda, lakini ninyi hamjui mahali ninapotoka au kule ninakoenda.
15 Ye iudge after ye flesshe. I iudge no man
Nyinyi mnahukumu kimwili; mimi simhukumu yeyote.
16 though I iudge yet is my iudgmet true. For I am not alone: but I and the father that sent me.
Mimi hata nikihukumu, hukumu yangu ni kweli kwa sababu siko peke yangu, bali niko pamoja na baba aliyenituma.
17 It is also written in youre lawe that the testimony of two men is true.
Ndiyo, na katika sheria yenu imeandikwa kwamba ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
18 I am one yt beare witnes of my selfe and the father that sent me beareth witnes of me.
Mimi ndiye ninayejishuhudia, na Baba aliyenituma ananishuhudia.”
19 Then sayde they vnto him: where is thy father? Iesus answered: ye nether knowe me nor yet my father. Yf ye had knowen me ye shuld have knowen my father also.
Wakamwambia, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu, “mimi hamnijui wala Baba yangu hammjui; mngelikuwa mnanijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
20 These wordes spake Iesus in the tresury as he taught in the temple and no man layde hondes on him for his tyme was not yet come.
Alisema maneno haya akiwa karibu na hazina alipokuwa akifundisha hekaluni, na hakuna hata mmoja aliyemkamata kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
21 Then sayde Iesus agayne vnto them. I goo my waye and ye shall seke me and shall dye in youre synnes. Whyther I goo thyther can ye not come.
Basi akawaambia tena, “Ninaenda zangu; mtanitafuta na mtakufa katika dhambi zenu. Kule niendako, hamuwezi kuja.”
22 Then sayde the Iewes: will he kyll him selfe because he sayth: whyther I goo thyther can ye not come?
Wayahudi wakasema, “Atajiua mwenyewe, yeye ambaye alisema, 'kule niendako hamuwezi kuja'?”
23 And he sayde vnto the: ye are fro beneth I am from above. Ye are of this worlde I am not of this worlde.
Yesu akawaambia, “Mnatoka chini; mimi natoka juu. Ninyi ni wa Ulimwengu huu; mimi si wa ulimwengu huu.
24 I sayde therfore vnto you that ye shall dye in youre synnes. For except ye beleve that I am he ye shall dye in youre synnes.
Kwa hiyo, naliwaambieni kuwa mtakufa katika dhambi zenu. Vinginevyo muamini kuwa MIMI NDIYE, mtakufa katika dhambi zenu”.
25 Then sayde they vnto him who arte thou? And Iesus sayde vnto them: Even ye very same thinge yt I saye vnto you.
Kwa hiyo wakamwambia, “Wewe ni nani?” Yesu akawaambia, Yale niliyowaambia tangu mwanzo.
26 I have many thinges to saye and to iudge of you. But he yt sent me is true. And I speake in ye worlde those thinges which I have hearde of him.
Ninayo mambo mengi ya kuzungumza na kuhukumu juu yenu. Hata hivyo, yeye aliyenituma ni wa kweli; na mambo niliyoyasikia kutoka kwake, mambo haya nayasema kwa Ulimwengu.”
27 They understode not that he spake of his father.
Hawakumuelewa kwamba alikuwa akiongea nao kuhusu Baba.
28 Then sayde Iesus vnto them: when ye have lyft vp an hye the sonne of man then shall ye knowe that I am he and that I do nothinge of my selfe: but as my father hath taught me even so I speake:
Yesu akasema, “Mtakapomwinua juu Mwana wa Mtu, ndipo mtakapojua kuwa MIMI NDIYE, na kwamba sifanyi lolote kwa nafsi yangu. Kama Baba alivyonifundisha, ninazungumza mambo haya.
29 and he that sent me is with me. The father hath not lefte me alone for I do alwayes those thinges that please him.
Yeye aliyenituma yuko pamoja nami, na yeye hajaniacha peke yangu, kwani kila mara nafanya yale yanayompendeza.”
30 As he spake these wordes many beleved on him.
Wakati Yesu akisema mambo haya, wengi walimwamini.
31 Then sayde Iesus to those Iewes which beleved on him. If ye cotinue in my wordes then are ye my very disciples
Yesu akasema kwa wale Wayahudi waliomwamini, “Ikiwa mtakaa katika neno langu, ndipo mtakuwa wanafunzi wangu kweli,
32 and shall knowe the trueth: and the trueth shall make you free.
nanyi mtaijua kweli, na kweli itawaweka huru.”
33 They answered him: We be Abrahams seede and were never bonde to eny man: why sayest thou then ye shalbe made fre.
Walimjibu, “Sisi ni uzao wa Ibrahimu na kamwe hatujawahi kwa chini ya utumwa wa yeyote; utasemaje, “Tutawekwa huru?”
34 Iesus answered them: verely verely I saye vnto you that whosoever committeth synne is the servaunt of synne.
Yesu aliwajibu, “Amini, amini, nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 And the servaunt abydeth not in the housse for ever: But ye sonne abydeth ever. (aiōn g165)
Mtumwa hakai nyumbani wakati wote; mwana hudumu siku zote. (aiōn g165)
36 If the sonne therfore shall make you fre then are ye fre in dede.
Kwa hiyo, ikiwa Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kabisa.”
37 I knowe that ye are Abrahams seed: But ye seke meanes to kyll me because my sayinges have no place in you.
Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Ibrahimu; mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halina nafasi ndani yenu.
38 I speake that I have sene with my father: and ye do that which ye have sene with youre father.
Ninasema mambo ambayo nimeyaona pamoja na Baba yangu, na ninyi vile vile mnafanya mambo ambayo mliyasikia kutoka kwa baba yenu.”
39 They answered and sayde vnto him: Abraham is oure father. Iesus sayde vnto them. If ye were Abrahams chyldren ye wolde do the dedes of Abraham.
Walijibu na kumwambia, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, Kama mngelikuwa watoto wa Ibrahimu, mngefanya kazi za Ibrahimu.
40 But now ye goo about io kyll me a man that have tolde you the truthe which I have herde of god: this dyd not Abraham.
Hata sasa mnatafuta kuniua, mtu aliyewaambia ukweli kwamba nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya hivi.
41 Ye do the dedes of youre father. Then sayde they vnto him: we were not borne of fornicacion. We have one father which is God.
Mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia, “Hatukuzaliwa katika uzinzi, tunaye Baba mmoja, Mungu.”
42 Iesus sayde vnto them: yf God were youre father then wolde ye love me. For I proceaded forthe and come from God. Nether came I of my selfe but he sent me.
Yesu akawaambia, “Ikiwa Mungu ni Baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nimetoka kwa Mungu; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye alinituma.
43 Why do ye not knowe my speache? Even because ye cannot abyde the hearynge of my wordes.
Kwa nini hamyaelewi maneno yangu? Kwa sababu hamuwezi kuvumilia kuyasikia maneno yangu.
44 Ye are of youre father the devyll and the lustes of youre father ye will folowe. He was a murtherer from the beginnynge and aboode not in the trueth because ther is no trueth in him. When he speaketh a lye then speaketh he of his awne. For he is a lyar and the father therof.
Ninyi ni wa baba yenu, shetani, na mnataka kuzitenda tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo na hawezi kusimama katika kweli kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anapoongea uongo, anaongea kutoka kwenye asili yake kwa sababu ni mwongo na baba wa uongo.
45 And because I tell you ye trueth therfore ye beleve me not.
Hata sasa, kwa sababu ninasema iliyo kweli, hamniamini.
46 Which of you can rebuke me of synne? If I saye ye trueth why do not ye beleve me?
Ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi? ikiwa ninasema iliyo kweli, kwa nini hamniamini?
47 He that is of God heareth goddes wordes Ye therfore heare them not because ye are not of God.
Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; ninyi hamyasikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
48 Then answered the Iewes and sayde vnto him: Saye we not well that thou arte a Samaritane and hast the devyll?
Wayahudi wakamjibu na kumwambia, hatujasema kweli kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?”
49 Iesus answered: I have not the devyll: but I honour my father and ye have dishonoured me.
Yesu akajibu, sina pepo; lakini namheshimu Baba yangu, nanyi hamniheshimu.
50 I seke not myne awne prayse: but ther is one that seketh and iudgeth.
Sitafuti utukufu wangu; kuna mmoja atafutaye na kuhukumu.
51 Verely verely I saye vnto you yf a man kepe my sayinges he shall never se deeth. (aiōn g165)
Amini, amini, nawaambia, iwapo yeyote atalishika neno langu, hataona mauti kamwe.” (aiōn g165)
52 Then sayde the Iewes to him: Now knowe we that thou hast the devyll. Abraha is deed and also the Prophetes: and yet thou sayest yf a man kepe my sayinge he shall never tast of deeth. (aiōn g165)
Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kuwa una pepo. Abrahamu na mabii walikufa; lakini unasema, 'Ikiwa mtu atalishika neno langu, hataonja mauti'. (aiōn g165)
53 Arte thou greater then oure father Abraham which is deed? and the Prophetes are deed. Whome makest thou thy selfe?
Wewe si mkuu kuliko baba yetu Abrahamu aliyekufa, sivyo? Manabii pia walikufa. Wewe wajifanya kuwa nani?”
54 Iesus answered: Yf I honoure my selfe myne honoure is nothinge worth. It is my father that honoureth me which ye saye is youre God
Yesu akajibu, “Ikiwa nitajitukuza mwenyewe, utukufu wangu ni bure; ni Baba yangu anayenitukuza - yule mnayemsema kuwa ni Mungu wenu.
55 and ye have not knowen him: but I knowe him. And yf I shuld saye I knowe him not I shuld be a lyar lyke vnto you. But I knowe him and kepe his sayinge.
Ninyi hamjamjua yeye, lakini mimi namjua yeye. Ikiwa nitasema, 'simjui,' nitakuwa kama nyinyi, muongo. Hata hivyo, ninamjua na maneno yake nimeyashika.
56 Youre father Abraham was glad to se my daye and he sawe it and reioysed.
Baba yenu Abrahamu alishangilia atakavyoiona siku yangu; aliiona na alifurahi.”
57 Then sayde the Iewes vnto him: thou arte not yet. l. yere olde and hast thou sene Abraham?
Wayahudi wakamwambia,”Haujafikisha umri wa miaka hamsini bado, nawe umemuona Ibrahimu?”
58 Iesus sayd vnto them: Verely verely I saye vnto you: yer Abraham was I am.
Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, MIMI NIKO.”
59 Then toke they vp stones to caste at him. But Iesus hid him selfe and went out of ye temple.
Ndipo waliokota mawe wapate kumpiga, lakini Yesu alijificha na akatoka nje ya hekalu.

< John 8 >