< John 20 >

1 The morow after the saboth daye came Mary Magdalene erly when it was yet darcke vnto ye sepulcre and sawe the stone taken awaye from ye toumbe.
Mapema siku ya kwanza ya juma, kungali bado giza, Mariamu Magdalena alikuja kaburini; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
2 Then she ranne and came to Simon Peter and to the other disciple whome Iesus loved and sayde vnto them. They have taken awaye the Lorde out of the toumbe and we cannot tell where they have layde him.
Kwa hiyo akakimbia mbio kwenda kwa Simon Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, kisha akawaambia, “wamemchukua Bwana kaburini, nasi hatujui kule walikomlaza.”
3 Peter went forth and that other disciple and came vnto the sepulcre.
Kisha Petro na yule mwanafunzi mwingine wakatoka, kuelekea kaburini.
4 They ranne bothe to gether and that other disciple dyd out runne Peter and came fyrst to the sepulcre.
Wote walipiga mbio kwa pamoja; yule mwanafunzi mwingine alikimbia kwa kasi zaidi ya Petro nakufika kaburini wa kwanza.
5 And he stouped doune and sawe the lynnen clothes lyinge yet wet he not in.
Akasimama na kisha kuangalia kaburini; akaiona ile sanda ya kitani imelala, lakini hakuingia ndani.
6 Then came Simon Peter folowynge him and went into ye sepulcre and sawe the lynnen clothes lye
Kisha Simon Petro naye akafika akaingia ndani ya Kaburi. Akaiona ile sanda ya kitani imelala pale
7 and the napkyn that was aboute his heed not lyinge with the lynnen clothe but wrapped togeder in a place by it selfe.
na ile leso iliyokuwa kichwani pake haikuwa imelala pamoja na zile sanda za kitani bali ilikuwa imelala pembeni peke yake.
8 Then went in also that other disciple which came fyrst to the sepulcre and he sawe and beleved.
Ndipo yule mwanafunzi mwingine naye alipoingia ndani ya kaburi; akaona na kuamini.
9 For as yet they knew not the scriptures that he shuld ryse agayne from deeth.
Kwa kuwa hadi wakati huo walikuwa bado hawajayajua maandiko kwamba ilimlazimu Yesu afufuke tena katika wafu.
10 And the disciples wet awaye agayne vnto their awne home.
Kisha wanafunzi wakaenda tena nyumbani kwao.
11 Mary stode with out at the sepulcre wepynge. And as she wept she bowed her selfe into the sepulcre
Hata hivyo, Mariamu alikuwa amesimama kaburini akilia, alivyokuwa akiendelea kulia alisimama kisha akatazama kaburini.
12 and sawe two angels in whyte sittyng the one at the heed and the other at the fete where they had layde the body of Iesus.
Akaona malaika wawili wenye sura nyeupe wamekaa mmoja kichwani na mwingine miguuni mahali ambapo Yesu alikuwa amelala.
13 And they sayde vnto her: woman why wepest thou? She sayde vnto the: For they have taken awaye my lorde and I wote not where they have layde him.
Nao wakamwambia, “Mwanamke, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Ni kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, nami sijui walikomweka.”
14 When she had thus sayde she turned her selfe backe and sawe Iesus stondynge and knewe not that it was Iesus.
Alipokwisha sema hayo, aligeuka na kumwona Yesu akiwa amesimama. Lakini hakutambua kama huyo alikuwa Yesu.
15 Iesus sayde vnto her: woman why wepest thou? Whom sekest thou? She supposynge that he had bene the gardener sayde vnto him. Syr yf thou have borne him hece tell me where thou hast layde him that I maye fet him.
Naye Yesu akamwambia, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Naye huku akidhani kuwa ni mtunza bustani akamwambia, “Bwana, kama ni wewe uliyemchukua, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Iesus sayde vnto her: Mary. She turned her selfe and sayde vnto him: Rabboni which is to saye master.
Yesu akamwambia, “Mariamu.” Naye akageuka mwenyewe na kumwambia kwa Kiaramu, “Raboni,” yaani hii ni kusema, “Mwalimu.”
17 Iesus sayde vnto her touche me not for I am not yet ascended to my father. But goo to my brethren and saye vnto them I ascende vnto my father and youre father to: my god and youre god.
Yesu akamwambia, “Usiniguse, kwani bado sijapaa kwenda kwa baba; bali uende kwa ndugu zangu ukawaambie kuwa nitapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
18 Mary Magdalene came and tolde the disciples yt she had sene the lorde and yt he had spoken soche thinges vnto her.
Mariamu Magdalena akaja kuwaambia wanafunzi, “Nimemwona Bwana,” na kwamba amemwambia mambo haya.
19 The same daye at nyght which was the morowe after ye saboth daye when the dores were shut where the disciples were assembled to geder for feare of the Iewes came Iesus and stode in the myddes and sayd to the: peace be with you.
Na ilipokuwa jioni, siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, na milango ikiwa imefungwa mahali wanafunzi walipokuwapo kwa kuwahofia Wayahudi, Yesu alikuja na kusimama katikati yao na kuwaambia, “Amani iwe kwenu.”
20 And when he had so sayde he shewed vnto them his hondes and his syde. Then were the disciples glad when they sawe the Lorde.
Alipokwisha sema haya akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Nao wanafunzi walipomwona Bwana walifurahi.
21 Then sayde Iesus to them agayne: peace be with you. As my father sent me even so sende I you.
Kisha Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi. Kama vile Baba alivyonituma mimi, vivyo hivyo nami nawatuma ninyi.”
22 And when he had sayde that he brethed on them and sayde vnto the: Receave ye holy goost.
Yesu alipokwisha sema hayo, akawavuvia akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Whosoevers synnes ye remyt they are remitted vnto the. And whosoevers synnes ye retayne they are retayned.
Yeyote mmsameheye dhambi, wamesamehewa; na wale mtakaowafungia watafungiwa.”
24 But Thomas one of ye twelve called Didymus was not with the when Iesus came.
Thomaso, mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Didimas, hakuwa na wanafunzi wenzake Yesu alipokuja.
25 The other disciples sayd vnto him: we have sene ye lorde. And he sayde vnto the: except I se in his hondes the prent of the nayles and put my fynger in the holes of the nayles and thrust my honde into his syde I will not beleve.
Wale wanafunzi wengine waka mwambia baadaye, “Tumemwona Bwana.” Naye akawambia, “Kama sitaona alama za misumari katika mikono yake, na kuweka vidole vyangu kwenye hizo alama, na pia kuweka mkono wangu kwenye ubavu wake sitaamini.”
26 And after. viii. dayes agayne his disciples were with in and Thomas with them. Then came Iesus when the dores were shut and stode in the myddes and sayde: peace be with you.
Baada ya siku nane wanafunzi walikuwa chumbani tena, naye Thomaso alikuwa pamoja nao. Wakati milango ilipokuwa imefungwa Yesu alisimama katikati yao. na akasema, “Amani na iwe nanyi.”
27 After that sayde he to Thomas: bringe thy fynger hether and se my hondes and bringe thy honde and thrust it into my syde and be not faythlesse but belevynge.
Kisha akamwambia Thomaso, leta kidole chako na uone mikono yangu; leta hapa mikono yako na uweke kwenye ubavu wangu; wala usiwe asiyeamini bali aaminiye.”
28 Thomas answered and sayde vnto him: my Lorde and my God.
Naye Thomaso akajibu na kumwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu.”
29 Iesus sayde vnto him. Thomas because thou hast sene me therfore thou belevest: Happy are they that have not sene and yet beleve.
Yesu akamwambia, Kwa kuwa umeniona, umeamini. Wamebarikiwa wao wanaoamini, pasipokuona.”
30 And many other signes dyd Iesus in the presence of his disciples which are not written in this boke.
Kisha Yesu alifanya ishara nyingi mbele ya wanafunzi, ambazo hazijawahi kuandikwa katika kitabu hiki;
31 These are written that ye myght beleve that Iesus is Christ the sonne of God and that in belevynge ye myght have lyfe thorowe his name.
bali hizi zimeandikwa ili kwamba muweze kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu, na kwamba muaminipo muwe na uzima katika jina lake.

< John 20 >