< John 11 >

1 A certayne man was sicke named Lazarus of Bethania the toune of Mary and her sister Martha.
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Alitokea Bethania, kijiji cha Mariamu na dada yake Martha.
2 It was that Mary which annoynted Iesus with oyntment and wyped his fete with her heere whose brother Lazarus was sicke
Alikuwa ni Mariamu yule yule aliyempaka Bwana Marhamu na kumfuta miguu yake kwa nywele zake, ambaye ndugu yake Lazaro alikuwa ni mgonjwa.
3 and his sisters sent vnto him sayinge. Lorde behold he whom thou lovest is sicke.
Ndipo dada hawa walituma ujumbe kwa Yesu na kusema, “Bwana, angalia yule umpendaye anaumwa.”
4 When Iesus hearde yt he sayd: this infirmite is not vnto deth but for ye laude of God that the sonne of God myght be praysed by the reason of it.
Yesu aliposikia alisema, “Ugonjwa huu si wa mauti, lakini, badala yake ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu ili kwamba Mwana wa Mungu apate kutukuzwa katika huo Ugonjwa.”
5 Iesus loved Martha and her sister and Lazarus.
Yesu alimpenda Martha na dada yake na Lazaro.
6 After he hearde that he was sicke then aboode he two dayes still in the same place where he was.
Aliposikia kuwa Lazaro ni mgonjwa, Yesu alikaa siku mbili zaidi mahali alipokuwa.
7 Then after that sayd he to his disciples: let us goo into Iewry agayne.
Ndipo baada ya hili aliwaambia wanafunzi wake, “Twendeni Uyahudi tena.”
8 His disciples sayde vnto him. Master the Iewes lately sought meanes to stone the and wilt thou goo thyther agayne?
Wanafunzi wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wakijaribu kukuponda mawe, na wewe unataka kurudi huko tena?”
9 Iesus answered: are ther not twelve houres in ye daye? Yf a man walke in ye daye he stombleth not because he seith the lyght of this worlde.
Yesu akawajibu, “Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu anapotembea mchana hawezi kujikwaa, kwa sababu anaona kwa nuru ya mchana.
10 But yf a ma walke in ye nyght he stombleth because ther is no lyght in him.
Hata hivyo, ikiwa atatembea usiku, atajikwaa kwa sababu nuru haiko ndani yake.”
11 This sayde he and after yt he sayde vnto the: oure frende Lazarus slepeth but I goo to wake him out of slepe.
Yesu akasema mambo haya, na baada ya mambo haya, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini ninakwenda ili kwamba nipate kumuamsha kutoka usingizini.”
12 Then sayde his disciples: Lorde yf he slepe he shall do well ynough.
Ndipo wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala, ataamka.
13 How be it Iesus spake of his deeth: but they thought yt he had spoke of ye naturall slepe.
Wakati huu Yesu alikuwa akizungumza habari za kifo cha Lazaro, lakini wao walidhani anazungumza juu ya kulala usingizi.
14 Then sayde Iesus vnto the playnly Lazarus is deed
Ndipo Yesu akazungumza nao wazi wazi, “Lazaro amekufa.
15 and I am glad for youre sakes yt I was not there because ye maye beleve. Neverthelesse let vs go vnto him.
Nina furaha kwa ajili yenu, kwamba sikuwepo kule ili kwamba mpate kuamini. Twendeni kwake.”
16 Then sayde Thomas which is called Dydimus vnto ye disciples: let vs also goo that we maye dye wt him
Basi Tomaso, aliyeitwa Pacha, aliwaambia wanafunzi wenzake, “Nasi twendeni pia tukafe pamoja na Yesu.”
17 Then went Iesus and founde that he had lyne in his grave foure dayes already.
Wakati Yesu alipokuja, alikuta kwamba Lazaro tayari amekwishakuwa kaburini siku nne.
18 Bethanie was nye vnto Ierusalem aboute. xv. furlonges of
Nayo Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu kama kilomita arobaini na tano hivi.
19 and many of the Iewes were come to Martha and Mary to comforte them over their brother.
Wengi kati ya Wayahudi wakaja kwa Martha na Mariamu kuwafariji kwa ajili ya ndugu yao.
20 Martha assone as she hearde yt Iesus was comynge went and met him: but Mary sate still in the housse.
Ndipo Martha aliposikia kuwa Yesu anakuja, alienda kukutana naye, lakini Mariamu aliendelea kukaa nyumbani.
21 Then sayde Martha vnto Iesus: Lorde yf thou haddest bene here my brother had not bene deed:
Ndipo Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, kaka yangu asingelikufa.
22 but neverthelesse I knowe that whatsoever thou axest of God God will geve it the.
Hata sasa, najua ya kuwa lolote utakaloomba kutoka kwa Mungu, atakupatia.”
23 Iesus sayde vnto her: Thy brother shall ryse agayne.
Yesu akamwambia, kaka yako atafufuka tena.”
24 Martha sayde vnto him: I knowe that he shall ryse agayne in the resurreccion at the last daye.
Martha akamwambia, najua kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
25 Iesus sayde vnto her: I am the resurreccion and the lyfe: He that beleveth on me ye though he were deed yet shall he lyve.
Yesu akamwambia, “Mimi ni ufufuo na uzima; yeye aniaminiye, ingawa atakufa, hata hivyo atakuwa anaishi;
26 And whosoever lyveth and belevest on me shall never dye. Beleveth thou this? (aiōn g165)
na yeye aishiye na kuniamini mimi hatakufa. Unaamini hili?” (aiōn g165)
27 She sayde vnto him: ye Lorde I beleve that thou arte Christ the sonne of god which shuld come into the worlde.
Akamwambia, “Ndiyo, Bwana naamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye katika ulimwengu.”
28 And assone as she had so sayde she went her waye and called Marie her sister secretly sayinge: The master is come and calleth for the
Alipokwisha kusema hili, alienda zake na kumwita dada yake Mariamu faraghani. Akasema, “Mwalimu yuko hapa na anakuita.”
29 And she assone as she hearde that arose quickly and came vnto him.
Mariamu aliposikia haya, aliinuka kwa haraka na kwenda kwa Yesu.
30 Iesus was not yet come into the toune: but was in the place where Martha met him.
Naye Yesu alikuwa hajaja bado ndani ya kijiji, bali alikuwa bado mahali alipokutana na Martha.
31 The Iewes then which were with her in the housse and comforted her when they sawe Mary that she rose vp hastely and went out folowed her saying: She goeth vnto the grave to wepe there.
Ndipo Wayahudi waliokuwa na Mariamu katika nyumba na wale waliokuwa wakimfariji, walipomuona akiinuka haraka na kutoka nje, walimfuata; walidhani kuwa anaenda kaburini ili akalie huko.
32 Then when Mary was come where Iesus was and sawe him she fell doune at his fete sayinge vnto him: Lorde yf thou haddest bene here my brother had not bene deed.
Ndipo Mariamu, alipofika pale Yesu alipokuwa alimuona na, alianguka chini ya miguu yake na kumwambia, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, ndugu yangu asingelikufa.”
33 When Iesus sawe her wepe and ye Iewes also wepe which came wt her he groned in ye sprete and was troubled in him selfe
Yesu alipomuona analia, na Wayahudi waliokuja pamoja naye walikuwa wakilia pia, aliomboleza katika roho na kufadhaika;
34 and sayde: Where have ye layed him? They sayde vnto him: Lorde come and se.
akasema, “Mmemlaza wapi? wakamwambia, Bwana, njoo utazame.”
35 And Iesus wept.
Yesu akalia.
36 Then sayde the Iewes: Beholde howe he loved him.
Ndipo Wayahudi wakasema, “Angalia alivyompenda Lazaro!”
37 And some of the sayde: coulde not he which openned the eyes of the blynde have made also that this man shuld not have dyed?
Lakini wengine kati yao wakasema, “Siyo huyu, mtu aliyeyafumbua macho ya yule aliyekuwa kipofu, hakuweza kumfanya huyu mtu asife?”
38 Iesus agayne groned in him selfe and came to the grave. It was a caue and a stone layde on it.
Ndipo Yesu, hali akiomboleza nafsini mwake tena, alienda kwenye kaburi. Sasa lilikuwa pango, na jiwe limewekwa juu yake.
39 And Iesus sayd: take ye awaye the stone. Martha the sister of him that was deed sayd vnto him: Lorde by this tyme he stinketh. For he hath bene deed foure dayes:
Yesu akasema, “Liondoweni jiwe.” Martha, dada yake na Lazaro, yeye aliyekufa, akamwambia Yesu, “Bwana, kwa muda huu, mwili utakuwa umeoza, kwa sababu amekwishakuwa maiti kwa siku nne.”
40 Iesus sayde vnto her: Sayde I not vnto the yt if thou didest beleve thou shuldest se ye glory of God.
Yesu akamwambia, “Mimi sikukuwaambia ya kwamba, kama ukiamini, utauona utukufu wa Mungu?”
41 Then they toke awaye ye stone from ye place where the deed was layde. And Iesus lyfte vp his eyes and sayde: Father I thanke the because that thou hast hearde me.
Kwa hiyo wakaliondoa jiwe. Yesu akainua macho yake juu na kusema, “Baba, nakushukuru kwa kuwa unanisikiliza.
42 I wot that thou hearest me all wayes: but because of the people that stonde by I sayde it yt they maye beleve that thou hast sent me.
Nilijua kwamba unanisikia mara zote, lakini ni kwa sababu ya kusanyiko ambalo limesimama kunizunguka kwamba nimesema haya, ili kwamba wapate kuamini kuwa wewe umenituma.”
43 And when he thus had spoken he cryed wt a loud voyce. Lazarus come forthe.
Baada ya kusema haya, alilia kwa sauti kubwa, “Lazaro, toka nje!”
44 And he that was deed came forth bounde hand and fote with grave bondes and his face was bounde with a napkin. Iesus sayde vnto the: loowse him and let him goo.
Mfu alitoka nje amefungwa mikono na miguu kwa sanda za kuzikia, na uso wake ulifungwa na kitambaa.” Yesu akawaambia, “Mfungueni mkamwache aende.”
45 Then many of the Iewes which came to Mary and had sene the thinges which Iesus dyd beleved on him.
Ndipo Wayahudi wengi waliokuja kwa Mariamu na kuona Yesu alichofanya, walimwamini;
46 But some of them went their wayes to the Pharises and tolde them what Iesus had done.
lakini baadhi yao walienda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo aliyoyafanya Yesu.
47 Then gadered the hye prestes and the Pharises a counsell and sayde: what do we? This ma doeth many miracles.
Ndipo wakuu wa Makuhani na Mafarisayo wakakusanyika pamoja katika baraza na kusema, “Tutafanya nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi.
48 Yf we let him scape thus all men will beleve on him and ye Romaynes shall come and take awaye oure countre and the people.
Ikiwa tutamwacha hivi peke yake, wote watamwamini; Warumi watakuja na kuchukua vyote mahali petu na taifa letu.”
49 And one of them named Cayphas which was the hieprest yt same yeare sayde vnto them: Ye perceave nothinge at all
Hata hivyo, mtu mmoja kati yao, Kayafa, aliyekuwa kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Hamjui chochote kabisa.
50 nor yet consider that it is expedient for vs that one man dye for the people and not that all the people perisshe.
Hamfikirii kwamba yafaa kwa ajili yenu kwamba mtu mmoja yapasa kufa kwa ajili ya watu kuliko taifa lote kuangamia.”
51 This spake he not of him selfe but beinge hye preste that same yeare he prophesied that Iesus shulde dye for the people
Haya hakuyasema kwa sababu yake mwenyewe, badala yake, kwa kuwa alikuwa kuhani mkuu mwaka ule, alitabiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa;
52 and not for the people only but that he shuld gader to geder in one the chyldren of God which were scattered abroode.
na si kwa taifa peke yake, bali Yesu apate vile vile kuwakusanya watoto wa Mungu ambao wametawanyika sehemu mbali mbali.
53 From that daye forth they held a counsell to geder for to put him to deeth.
Kwa hiyo kuanzia siku hiyo na kuendelea wakapanga namna ya kumwua Yesu.
54 Iesus therfore walked no more opely amoge the Iewes: but wet his waye thence vnto a coutre nye to a wildernes into a cite called Ephraim and there hauted with his disciples.
Yesu hakutembea tena wazi wazi kati ya Wayahudi, bali aliondoka hapo na kwenda nchi iliyo karibu na jangwa katika mji uitwao Efraimu. Hapo alikaa na wanafunzi.
55 And the Iewes ester was nye at hand and many went out of the countre vp to Ierusalem before the ester to purify them selves.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu, na wengi wakapanda kwenda Yerusalemu nje ya mji kabla ya Pasaka ili wapate kujitakasa wenyewe.
56 Then sought they for Iesus and spake bitwene the selves as they stode in the teple: What thinke ye seynge he cometh not to the feast.
Walikuwa wakimtafuta Yesu, na kuzungumza kila mmoja walipokuwa wamesimama hekaluni, “Mnafikiri nini? Kwamba hatakuja katika sikukuu?”
57 The hye prestes and Pharises had geven a comaundemet that yf eny man knew where he were he shuld shewe it that they myght take him.
Wakati huu wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba ikiwa mmoja atajua Yesu alipo, anapaswa kutoa taarifa ili kwamba wapate kumkamata.

< John 11 >