< Acts 9 >

1 And Saul yet brethynge oute threatnynges and slaughter agaynst ye disciples of the lorde went vnto ye hye preste
Wakati huo Saulo alikuwa akizidisha vitisho vikali vya kuwaua wafuasi wa Bwana. Alikwenda kwa Kuhani Mkuu,
2 and desyred of him letters to Damasco to ye synagoges: that yf he founde eny of this waye whether they were men or wemen he myght bringe them bounde vnto Ierusalem.
akaomba apatiwe barua za utambulisho kwa masunagogi ya Kiyahudi kule Damasko, ili akikuta huko wanaume au wanawake wanaofuata Njia ya Bwana, awakamate na kuwaleta Yerusalemu.
3 But as he went on his iorney it fortuned yt he drue nye to Damasco and sodenly ther shyned rounde about him a lyght fro heven.
Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka angani ulimwangazia pande zote.
4 And he fell to ye erth and hearde a voyce sayinge to him: Saul Saul why persecutest thou me?
Akaanguka chini na kusikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?”
5 And he sayde what arte thou lorde? And the lorde sayd I am Iesus whom thou persecutest it shalbe harde for ye to kycke agaynst ye pricke.
Naye Saulo akauliza, “Ni nani wewe Bwana?” Na ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
6 And he bothe tremblynge and astonyed sayde: Lorde what wilt thou have me to do? And ye Lorde sayde vnto him: aryse and goo into the cite and it shalbe tolde the what thou shalt do.
Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”
7 The men which iornayed with him stode amased for they herde a voyce but sawe no man.
Wale watu waliokuwa wanasafiri pamoja na Saulo walisimama pale, wakiwa hawana la kusema; walisikia ile sauti lakini hawakumwona mtu.
8 And Saul arose from the erth and opened his eyes but sawe no man. Then ledde they him by the honde and brought him into Damasco.
Saulo aliinuka, na alipofumbua macho yake hakuweza kuona chochote; hivyo wale watu wakamwongoza kwa kumshika mkono mpaka mjini Damasko.
9 And he was. iii. dayes with out syght and nether ate nor dranke.
Saulo alikaa siku tatu bila kuona, na wakati huo hakula au kunywa chochote.
10 And ther was a certayne disciple at Damasco named Ananias and to him sayde the lorde in a vision: Ananias. And the he sayde: beholde I am here lorde.
Basi, huko Damasko kulikuwa na mfuasi mmoja aitwaye Anania. Bwana akamwambia katika maono, “Anania!” Anania akaitika, “Niko hapa, Bwana.”
11 And the lorde sayde to him: aryse and goo into the strete which is called strayght and seke in the housse of Iudas after one called Saul of Tharsus. For beholde he prayeth
Naye Bwana akamwambia, “Jitayarishe uende kwenye barabara inayoitwa Barabara ya Moja kwa Moja, na katika nyumba ya Yuda umtake mtu mmoja kutoka Tarso aitwaye Saulo. Sasa anasali;
12 and hath sene in a vision a man named Ananias comynge in to him and puttynge his hondes on him that he myght receave his syght.
na katika maono ameona mtu aitwaye Anania akiingia ndani na kumwekea mikono ili apate kuona tena.”
13 Then Ananias answered: Lorde I have hearde by many of this man how moche evell he hath done to thy sainctes at Ierusalem
Lakini Anania akajibu, “Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kutoka kwa watu wengi; nimesikia juu ya mabaya aliyowatendea watu wako huko Yerusalemu.
14 and here he hath auctorite of the hye prestes to bynde all that call on thy name.
Na amekuja hapa akiwa na mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu kuwatia nguvuni wote wanaoomba kwa jina lako.”
15 The lorde sayde vnto him: Goo thy wayes: for he is a chosen vessell vnto me to beare my name before the gentyls and kynges and the chyldren of Israel.
Lakini Bwana akamwambia, “Nenda tu, kwa maana nimemchagua awe chombo changu, alitangaze jina langu kwa mataifa na wafalme wao na kwa watu wa Israeli.
16 For I will shewe him how great thinges he must suffre for my names sake.
Mimi mwenyewe nitamwonyesha mengi yatakayomlazimu kuteswa kwa ajili ya jina langu.”
17 Ananias went his waye and entryd into ye housse and put his hondes on him and sayde: brother Saul the lorde that apperyd vnto the in the waye as thou camst hath sent me that thou myghtest receave thy syght and be filled with the holy goost.
Basi, Anania akaenda, akaingia katika hiyo nyumba. Kisha akaweka mikono yake juu ya Saulo, akasema, “Ndugu Saulo, Bwana ambaye ndiye Yesu mwenyewe aliyekutokea ulipokuwa njiani kuja hapa, amenituma ili upate kuona tena na kujazwa Roho Mtakatifu.”
18 And immediatly ther fell from his eyes as it had bene scales and he receaved syght and arose and was baptised
Mara vitu kama magamba vikaanguka kutoka macho ya Saulo, akaweza kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
19 and receaved meate and was comforted. Then was Saul a certayne daye wt the disciples which were at Damasco.
Na baada ya kula chakula, nguvu zake zikamrudia. Saulo alikaa siku chache pamoja na wafuasi huko Damasko.
20 And streyght waye he preached Christ in the synagoges how that he was the sonne of God.
Mara alianza kuhubiri katika masunagogi kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
21 All that hearde him were amased and sayde: is not this he that spoyled the which called on this name in Ierusalem and came hyther for ye entent that he shuld bringe the bounde vnto the hye prestes?
Watu wote waliomsikia walishangaa, wakasema, “Je, mtu huyu si yuleyule aliyewaua wale waliokuwa wanaomba kwa jina hili kule Yerusalemu? Tena alikuja hapa akiwa na madhumuni ya kuwatia nguvuni watu hao na kuwapeleka kwa makuhani!”
22 But Saul encreased in stregth and confounded the Iewes which dwelte at Damasco affirminge that this was very Christ.
Saulo alizidi kupata nguvu, na kwa jinsi alivyothibitisha wazi kwamba Yesu ndiye Kristo, Wayahudi wa huko Damasko walivurugika kabisa.
23 And after a good whyle ye Iewes toke counsell to gether to kyll him.
Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi walikusanyika na kufanya mpango wa kumwua Saulo.
24 But their layinge awayte was knowen of Saul. And they watched at the gates daye and nyght to kyll him.
Lakini Saulo alipata habari ya mpango huo. Usiku na mchana walilinda milango ya kuingia mjini ili wapate kumwua.
25 Then ye disciples toke him by night and put him thorow the wall and let him doune in a basket.
Lakini wakati wa usiku wanafunzi wake walimchukua, wakamteremsha chini ndani ya kapu kubwa kwa kupitia nafasi iliyokuwako ukutani.
26 And when Saul was come to Ierusalem he assayde to cople him silfe with ye discyples and they were all afrayde of hym and beleued not that he was a disciple.
Saulo alipofika Yerusalemu alijaribu kujiunga na wale wanafunzi. Lakini wote walimwogopa, na hawakuweza kuamini kwamba yeye amekuwa mfuasi.
27 But Bernabas toke hym and brought hym to ye apostles and declared to the how he had sene ye Lorde in ye waye and had spoke wyth hym: and how he had done boldely at damasco in the name of Iesu.
Hapo, Barnaba alikuja akamchukua Saulo, akampeleka kwa mitume na kuwaeleza jinsi Saulo alivyomwona Bwana njiani na jinsi Bwana alivyoongea naye. Aliwaambia pia jinsi Saulo alivyokuwa amehubiri bila uoga kule Damasko.
28 And he had his conuersacion with them at Ierusalem
Basi, Saulo alikaa pamoja nao, akatembelea Yerusalemu yote akihubiri neno la Bwana bila hofu.
29 and quit hym silfe boldly in the name of the lorde Iesu. And he spake and disputed wyth the grekes: and they went aboute to slee hym.
Pia aliongea na kubishana na Wayahudi wasemao Kigiriki, lakini wao walijaribu kumwua.
30 But when the brethren knew of that they brought hym to cesarea and sent hym forth to Tharsus.
Wale ndugu walipogundua jambo hilo walimchukua Saulo, wakampeleka Kaisarea, wakamwacha aende zake Tarso.
31 Then had ye congregacios rest thorowoute all Iewry and galile and Samary and were edified and walked in the feare of the lorde and multiplied by the comforte of the holy gost.
Wakati huo kanisa likawa na amani popote katika Yudea, Galilaya, na Samaria. Lilijengwa na kukua katika kumcha Bwana, na kuongezeka likitiwa moyo na Roho Mtakatifu.
32 And it chaunsed yt as Peter walked throughoute all quarters he ca to ye saynctes which dwelt at Lydda
Petro alipokuwa anasafirisafiri kila mahali alifika pia kwa watu wa Mungu waliokuwa wanaishi Luda.
33 and there he foude a certayne ma namyd Eneas whych had kepte hys bed viii. yere sicke of the palsie.
Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Enea ambaye kwa muda wa miaka minane alikuwa amelala kitandani kwa sababu alikuwa amepooza.
34 Then sayde Peter vnto hym: Eneas Iesus Christ make ye whole. Aryse and make thy beed. And he arose immedyatly.
Basi, Petro akamwambia, “Enea, Yesu Kristo anakuponya. Amka utandike kitanda chako.” Enea akaamka mara.
35 And all that dwelt at lydda and assaron sawe hym and tourned to the lorde.
Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Enea, na wote wakamgeukia Bwana.
36 Ther was at Ioppe a certayne woma (whiche was a disciple named Tabitha which by interpretacion is called dorcas) the same was full of good workes and almes dedes which she did.
Kulikuwa na mfuasi mmoja mwanamke mjini Yopa aitwaye Tabitha (kwa Kigiriki ni Dorka, maana yake, Paa). Huyo mwanamke alikuwa akitenda mema na kuwasaidia maskini daima.
37 And it chaunsed in those dayes that she was sicke and dyed. When they had wesshed her and layd her in a chamber:
Wakati huo ikawa kwamba aliugua, akafa. Watu wakauosha mwili wake, wakauzika katika chumba ghorofani.
38 Because Lydda was nye to Ioppa and the disciples had hearde that Peter was there they sent vnto hym desyrynge him that he wolde not be greved to come vnto them.
Yopa si mbali sana na Luda; kwa hiyo wafuasi waliposikia kwamba Petro alikuwa Luda, wakawatuma watu wawili kwake na ujumbe: “Njoo kwetu haraka iwezekanavyo.”
39 Peter arose and came with them and when he was come they brought him in to ye chamber. And all ye wydowes stode roude aboute hym wepynge and shewynge the cotes and garmentes which Dorcas made whill she was with the.
Basi, Petro akaenda pamoja nao. Alipofika alipelekwa ghorofani katika kile chumba. Huko wajane wengi walimzunguka Petro wakilia na kumwonyesha makoti na nguo ambazo Dorka alikuwa akitengeneza wakati alipokuwa hai.
40 And Peter put the all forth and kneled doune and prayde and turned him to ye body and sayde: Tabitha aryse. And she opened her eyes and whe she sawe Peter she sat vp.
Petro aliwatoa nje wote, akapiga magoti, akasali. Kisha akamgeukia yule maiti, akasema, “Tabitha, amka” Naye akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi.
41 And he gave her ye honde and lyft her up and called the sainctes and wydowes and shewed her alyve.
Petro akamsaidia kusimama, halafu akawaita wale watu wa Mungu na wale wajane, akamkabidhi kwao akiwa mzima.
42 And it was knowne throwout all Ioppa and many beleved on the Lorde.
Habari ya tukio hili ilienea kila mahali huko Yopa, na watu wengi wakamwamini Bwana.
43 And it fortuned that he taryed many dayes in Ioppa with one Simon a tanner.
Petro alikaa siku kadhaa huko Yopa, akiishi kwa mtu mmoja mtengenezaji wa ngozi aitwaye Simoni.

< Acts 9 >