< Acts 3 >

1 Peter and Iohn went up togedder into the teple at the nynthe houre of prayer.
Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
2 And ther was a certayne man halt from his mothers wobe who they brought and layde at the gate of the temple called beutifull to axe almes of them that entred into the temple.
Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
3 Which same when he sawe Peter and Iohn that they wolde in to the teple desyred to receave an almes.
Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
4 And Peter fastened his eyes on him with Iohn and sayde: looke on vs.
Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
5 And he gaue hede vnto the trustinge to receave somthinge of them.
Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 Then sayd Peter: Silver and golde have I none suche as I have geve I the. In the name of Iesu Christ of Nazareth ryse vp and walke.
Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
7 And he toke him by the right honde and lifte him vp. And immediatly his fete and ancle bones receaved strenght.
Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
8 And he sprage stode and also walked and entred with them into the temple walkinge and leapinge and laudynge God.
Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
9 And all the people sawe him walke and laude God.
Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
10 And they knewe him that it was he which sate and begged at the beutifull gate of the temple. And they wondred and were sore astonnyed at that which had happened vnto him.
Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
11 And as ye halt which was healed helde Peter and Iohn all the people ranne amased vnto them in Salomons porche.
Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
12 When Peter sawe that he answered vnto the people. Ye men of Israel why marvayle ye at this or why looke ye so stedfastly on vs as though by oure awne power or holynes we had made this man goo?
Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
13 The God of Abraham Isaac and Iacob the God of oure fathers hath glorified his sonne Iesus whom ye delyvered and denyed in the presence of Pylate whe he had iudged him to be lowsed.
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
14 But ye denyed the holy and iust and desyred a mortherar to be geven you
Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
15 and kylled the Lorde of lyfe whom God hath raysed from deeth of the which we are wytnesses.
Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
16 And his name thorow the fayth of his name hath made this man sound whom ye se and knowe. And the fayth which is by him hath geven to him this health in the presence of you all.
Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
17 And now brethre I wote well that thorow ignorauce ye did it as dyd also youre heddes.
“Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
18 But those thinges which God before had shewed by the mouth of all his Prophetes how yt Christ shuld suffre he hath thus wyse fulfilled.
Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
19 Repent ye therfore and turne yt youre synnes maye be done awaye when the tyme of refresshinge commeth which we shall have of the presence of the Lorde
Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
20 and when God shall sende him which before was preached vnto you that is to wit Iesus Christ
Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
21 which must receave heave vntyll the tyme yt all thinges which God hath spoken by the mouth of all his holy Prophetes sence the worlde began be restored agayne. (aiōn g165)
Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
22 For Moses sayd vnto the fathers: A Prophet shall the Lorde youre God rayse vp vnto you even of youre brethren lyke vnto me: him shall ye heare in all thinges whatsoever he shall saye vnto you.
Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
23 For the tyme will come yt every soule which shall not heare that same Prophet shalbe destroyed from amonge the people.
Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
24 Also all the Prophetes from Samuel and thence forth as many as have spoken have in lykwyse tolde of these dayes.
Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
25 Ye are the chyldren of the Prophetes and of the covenaunt which God hath made vnto oure fathers sayinge to Abraham: Eve in thy seede shall all the kinredes of the erth be blessed.
Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
26 Fyrst vnto you hath God raysed vp his sonne Iesus and him he hath sent to blysse you that every one of you shuld turne from youre wickednes.
Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”

< Acts 3 >