< Acts 24 >

1 After. v. dayes Ananias the hye preste descended with elders and with a certayne Oratour named Tartullus and enformed the ruelar of Paul.
Baada ya siku tano, Anania kuhani mkuu, baadhi ya wazee na msemaji mmoja aitwaye Tertulo, wakaenda pale. Watu hawa wameleta mashtaka dhidi ya Paulo kwa gavana.
2 When Paul was called forth Tartullus beganne to accuse him saying: Seynge yt we live in great quyetnes by the meanes of the and that many good thinges are done vnto this nacion thorow thy providence:
Paulo alipo simama mbele ya gavana, Tertulo akaanza kumshitaki na kusema kwa gavana, “kwa sababu yako tuna amani kuu; na kwa maono yako yanaleta mageuzi mazuri katika taifa letu;
3 that alowe we ever and in all places most myghty Felix with all thankes.
basi kwa shukurani yote tunapokea kila kitu ukifanyacho, Wasalam mheshimiwa Feliki.
4 Notwithstondinge that I be not tedeous vnto the I praye the that thou woldest heare vs of thy curtesy a feawe wordes.
Lakini nisikuchoshe zaidi, nakusihi unisikilize maneno machache kwa fadhili zako.
5 We have founde this ma a pestilent felowe and a mover of debate vnto all the Iewes thorowe out the worlde and a mayntayner of ye secte of the Nazarites
Kwa maana tumempata mtu huyu mkorofi, na anasababisha Wayahudi wote kuasi duniani. Tena ni kiongozi wa madhehebu ya Wanazorayo. (Zingatia: Sehemu ya maneno ya mstari huu 24: 6
6 and hath also enforsed to pollute the temple. Whom we toke and wolde have iudged acordinge to oure lawe:
Na tena alijaribu kulitia hekalu unajisi hivyo tukamkamata., haumo kwenye nakala bora za kale). (Zingatia: Mstari huu
7 but the hye captayne Lisias came vpon vs and with great violence toke him awaye out of oure hodes
Lisiasi, afisa, alikuja na akamchukua kwa nguvu mikononi mwetu., haumo kwenye nakala bora za maandiko ya kale).
8 comaundinge his accusars to come vnto the. Of who thou mayst (yf thou wilt enquyre) knowe the certayne of all these thinges where of we accuse him.
Ukimwuliza Paulo kuhusu mambo haya, hata utaweza kujifunza ni kitu gani tumemshtakia.”
9 The Iewes lyke wyse affermed sayinge that it was even so.
Wayahudi nao wakamshtaki Paulo, wakisema kwamba haya mambo yalikuwa kweli.
10 Then Paul (after that the rular him selfe had beckened vnto him that he shuld speake) answered: I shall with a moare quyet minde answere for my selfe for as moche as I vnderstonde yt thou hast bene of many yeares a iudge vnto this people
Liwali alipompungia mkono ili Paulo aongee, Paulo alijibu, “Ninajua ya kwamba kwa miaka mingi umekua mwamuzi wa taifa hili, na nina furaha kujieleza mwenyewe kwako.
11 because that thou mayst knowe yt there are yet. xii. dayes sence I went vp to Ierusalem for to praye
Waweza kuhakikisha kuwa hazijapita siku zaidi ya kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda kuabudu Yerusalemu.
12 and that they nether founde me in the teple disputinge with eny man other raysinge vp the people nether in the Synagoges nor in the cite.
Na waliponikuta katika hekalu, sikubishana na mtu yeyote, na sikufanya fujo katika mkutano, wala katika masinagogi wala ndani ya mji;
13 Nether can they prove ye thinges wher of they accuse me.
na wala hawawezi kuhakikisha kwako mashitaka wanayoyashitaki dhidi yangu.
14 But this I confesse vnto ye that after that waye (which they call heresy) so worshippe I the God of my fathers belevinge all thinges which are writte in the lawe and ye Prophetes
Ila nakiri hili kwako, ya kwamba kwa njia ile ambayo wanaiita dhehebu, kwa njia iyo hiyo ninamtumikia Mungu wa baba zetu. Mimi ni mwaminifu kwa yote yaliyoko kwenye sheria na maandiko ya manabii.
15 and have hope towardes God that ye same resurreccion from deeth (which they them selves loke for also) shalbe both of iust and vniust.
Nina ujasiri ule ule kwa Mungu ambao hata hao nao wanaungojea, kuja kwa ufufuo wa wafu, kwa wote wenye haki na wasio na haki pia;
16 And therfore stody I to have a cleare consciece towarde God and toward man also.
na kwa hili, ninafanya kazi ili niwe na dhamira isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu kupitia mambo yote.
17 But after many yeres I came and brought almes to my people and offeringes
Sasa Baada ya miaka mingi nimekuja kuleta msaada kwa taifa langu na zawadi ya fedha.
18 in the which they founde me purified in the teple nether with multitude nor yet wt vnquyetnes How beit there were certayne Iewes out of Asia
Nilipofanya hivi, Wayahudi fulani wa Asia wakanikuta ndani ya sherehe ya utakaso ndani ya hekalu, bila kundi la watu wala ghasia.
19 which ought to be here present before the and accuse me yf they had ought agaynst me:
Watu hawa ambao imewapasa kuwapo mbele yako sasa hivi na waseme kile walichonacho juu yangu kama wana neno lo lote.
20 or els let these same here saye if they have founde eny evyll doinge in me whill I stonde here in ye counsell:
Au watu hawa wenyewe na waseme ni kosa gani waliloliona kwangu niliposimama mbele za baraza la kiyahudi;
21 except it be for this one voyce yt I cryed stondinge amoge the of the resurreccion fro deeth am I iudged of you this daye.
isipokuwa kwa ajili ya kitu kimoja nilichokisema kwa sauti niliposimama katikati yao, ' ni kwa sababu ya ufufuo wa wafu ninyi mnanihukumu.”'
22 When Felix hearde these thinges he deferde them for he knewe very well of yt waye and sayde: when Lisias the captayne is come I will know the vtmost of youre matters.
Feliki alikuwa ametaarifiwa vizuri kuhusu njia, na akauahirisha mkutano. Akasema, “Lisia jemedari atakapokuja chini kutoka Yerusalemu nitatoa maamuzi dhidi ya mashitaka yenu.”
23 And he commaunded an vndercaptayne to kepe Paul and that he shuld have rest and that he shuld forbyd none of his aquayntauce to minister vnto him or to come vnto him.
Ndipo akamwamuru akida amlinde Paulo, ila awe na nafasi na hata asiwepo mtu wakuwakataza marafiki zake wasimsaidie wala wasimtembelee.
24 And after a certayne dayes ca Felix and his wyfe Drusilla which was a Iewas and called forth Paul and hearde him of the fayth which is toward Christ.
Baada ya siku kadhaa, Feliki akarudi na Drusila mkewe aliyekuwa Myahudi, akatuma kumwita Paulo na akasikiliza toka kwake habari za imani ndani ya Kristo Yesu.
25 And as he preached of righteousnes temperauce and iudgement to come Felix trembled and answered: thou hast done ynough at this tyme departe when I have a conveniet tyme I will sende for the.
Ila Paulo alipokuwa akijadiliana naye kuhusu haki, kuwa na kiasi na hukumu itakayokuja, Feliki akapata hofu akajibu, “nenda mbali kwa sasa, ila nikipata muda tena, nitakuita.”
26 He hoped also that money shuld have bene geven him of Paul that he myght lowse him: wherfore he called him ye oftener and comened with him.
Muda uo huo, alitegemea kwamba Paulo atampa fedha kwa hiyo alimwita mara nyingi akaongea naye.
27 But after two yeare Festus Porcius came into Felix roume. And Felix willinge to shewe ye Iewes a pleasure lefte Paul in preson bounde.
Ila miaka miwili ilipopita, Porkio Festo akawa Liwali baada ya Feliki, ila Feliki alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, hivyo akamwacha Paulo chini ya uangalizi.

< Acts 24 >