< 1 Corinthians 3 >

1 And I coulde not speake vnto you brethre as vnto spretuall: but as vnto carnall even as it were vnto babes in Christ.
Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2 I gave you mylke to drinke and not meate. For ye then were not stronge no nether yet are.
Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3 For ye are yet carnall. As longe verely as ther is amoge you envyige stryfe and dissencio: are ye not carnall and walke after ye manner of me?
Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4 As loge as one sayth I holde of Paul and another I am of Apollo are ye not carnall?
Mmoja wenu anaposema, “Mimi ni wa Paulo”, na mwingine, “Mimi ni wa Apolo”, je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5 What is Paul? What thinge is Apollo? Only miministers are they by who ye beleved even as the Lorde gave every ma grace.
Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6 I have planted: Apollo watred: but god gave increace.
Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7 So then nether is he that planteth eny thinge nether he yt watreth: but god which gave the increace.
Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8 He that planteth and he that watreth are nether better then the other. Every man yet shall receave his rewarde accordynge to his laboure.
Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9 We are goddis labourers ye are goddis husbandrye ye are goddis byldynge.
Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10 Accordynge to the grace of god geven vnto me as a wyse bylder have I layde the foundacio And another bylt thero But let every ma take hede how he bildeth apo.
Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11 For other foundacion can no man laye then yt which is layde which is Iesus Christ.
Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12 Yf eny man bilde on this foundacion golde silver precious stones tymber haye or stoble:
Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13 every mannes worke shall appere. For the daye shall declare it and it shalbe shewed in fyre. And ye fyre shall trye euery mannes worke what it is.
Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14 Yf eny mannes worke yt he hath bylt apon byde he shall receave a rewarde.
Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15 If eny manes worke burne he shall suffre losse: but he shalbe safe him selfe: neverthelesse yet as it were thorow fyre.
lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16 Are ye not ware that ye are the temple of god and how that the sprete of god dwelleth in you?
Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17 Yf eny man defyle the temple of god him shall god destroye. For the temple of god is holy which temple ye are.
Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18 Let no man deceave him silfe. Yf eny man seme wyse amonge you let him be a fole in this worlde that he maye be wyse. (aiōn g165)
Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. (aiōn g165)
19 For ye wisdome of this worlde is folysshnes with god. For it is writte: he compaseth the wyse in their craftynes.
Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: “Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao.”
20 And agayne God knoweth the thoughtes of the wyse that they be vayne.
Na tena: “Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai.”
21 Therfore let no ma reioyce in men. For all thinges are youres
Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22 whether it be Paul other Apollo other Cephas: whether it be ye worlde other lyfe other deeth whether they be present thinges or thinges to come: all are youres
Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23 and ye are Christes and Christ is goddis.
Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.

< 1 Corinthians 3 >