< 1 Corinthians 15 >

1 Brethren as pertayninge to the gospell which I preached vnto you which ye have also accepted and in the which ye continue
Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2 by which also ye are saved: I do you to wit after what maner I preached vnto you yf ye kepe it except ye have beleved in vayne.
Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3 For fyrst of all I delivered vnto you that which I receaved: how that Christ dyed for oure synnes agreinge to the scriptures:
Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4 and that he was buried and that he arose agayne the thyrd daye accordinge to the scriptures:
kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5 and that he he was sene of Cephas then of the twelve.
kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6 After that he was sene of moo the five hodred brethren at once: of which many remayne vnto this daye and many are fallen aslepe.
Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7 After that appered he to Iames then to all the Apostles.
Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8 And last of all he was sene of me as of one that was borne out of due tyme.
Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9 For I am the lest of all the Apostles which am not worthy to be called an Apostle because I persecuted the congregacion of God.
Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10 But by the grace of God I am that I am. And his grace which is in me was not in vayne: but I labored moare aboundauntly then they all not I but the grace of God which is with me.
Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11 Whether it were I or they so we preache and so have ye beleved.
Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12 If Christ be preached how that he rose fro deeth: how saye some that are amoge you that ther is no resurreccion from deeth?
Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13 If ther be no rysynge agayne from deeth: then is Christ not rysen.
Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14 If Christ be not rysen then is oure preachinge vayne and youre faith is also in vayne.
na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15 Ye and we are founde falce witnesses of God. For we have testifyed of God how that he raysyd vp Christ whom he raysyd not vp yf it be so that the deed ryse not vp agayne.
Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua—kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16 For yf the deed ryse not agayne then is Christ not rysen agayne.
Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17 If it be so yt Christ rose not then is youre fayth in vayne and yet are ye in youre synnes.
Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18 And therto they which are fallen a slepe in Christ are perished.
Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19 If in this lyfe only we beleve on christ then are we of all men the miserablest.
Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20 But now is Christ rysen from deeth and is become the fyrst frutes of them that slept.
Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21 For by a man came deeth and by a man came resurreccion fro deeth.
Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22 For as by Adam all dye: eve so by Christ shall all be made alive
Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23 and every man in his awne order. The fyrst is Christ then they yt are Christis at his commynge.
Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24 Then cometh the ende when he hath delivered vp ye kyngdome to God ye father when he hath put doune all rule auctorite and power.
Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25 For he must raygne tyll he have put all his enemyes vnder his fete.
Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26 The last enemye that shalbe destroyed is deeth.
Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27 For he hath put all thinges vnder his fete. But when he sayth all thinges are put vnder him it is manyfest that he is excepted which dyd put all thinges vnder him.
Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28 When all thinges are subdued vnto him: then shall the sonne also him selfe be subiecte vnto him that put all thinges vnder him yt God maye be all in all thinges.
Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29 Ether els what do they which are baptised over ye deed yf the deed ryse not at all? Why are they then baptised over the deed?
Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30 Ye and why stonde we in ieoperdy every houre?
Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31 By oure reioysinge which I have in Christ Iesu oure Lorde I dye dayly.
Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32 That I have fought with beastes at Ephesus after the maner of men what avautageth it me yf the deed ryse not agayne? Let vs eate and drynke to morowe we shall dye.
Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”
33 Be not deceaved: malicious speakinges corrupte good maners.
Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34 Awake truely out of slepe and synne not. For some have not the knowlege of God. I speake this vnto youre rebuke.
Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35 But some ma will saye: how aryse ye deed? with what bodyes come they in?
Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?”
36 Thou fole that which thou sowest is not quickened except it dye.
Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37 And what sowest thow? Thow sowest not that body that shalbe: but bare corne (I meane ether of wheet or of some other)
Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38 and God geveth it a body at his pleasure to every seed a severall body.
Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39 All flesshe is not one manner of flesshe: but ther is one maner flesshe of men another maner flesshe of beastes another maner flesshe of fysshes and another of byrdes.
Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40 Ther are celestiall bodyes and ther are bodyes terrestriall. But ye glory of ye celestiall is one and ye glory of the terrestriall is another.
Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41 Ther is one maner glory of the sonne and another glory of the mone and another glory of the starres. For one starre differth fro another in glory.
Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42 So is the resurreccio of ye deed. It is sowe in corrupcio and ryseth in incorrupcion.
Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43 It is sowen in dishonoure and ryseth in honoure. It is sowe in weaknes and ryseth in power. It is sowne a naturall body and ryseth a spretuall body.
Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44 Ther is a naturall bodye and ther is a spretuall body:
Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45 as it is written: the fyrste man Adam was made a livinge soule: and ye last Ada was made a quickeninge sprete.
Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46 How be it yt is not fyrst which is spirituall: but yt which is naturall and then yt which is spretuall.
Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47 The fyrst ma is of the erth erthy: the seconde man is ye Lorde fro heave.
Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48 As is the erthy soche are they that are erthye. And as is the hevely soche are they yt are hevenly.
Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49 And as we have borne the ymage of the erthy so shall we beare the ymage of the hevenly.
Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50 This saye I brethren that flesshe and bloud canot inheret the kyngdome of God. Nether corrupcion inhereth vncorrupcion.
Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51 Beholde I shewe you a mystery. We shall not all slepe: but we shall all be chaunged
Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52 and that in a moment and in the twinclinge of an eye at the sounde of the last trompe. For the trompe shall blowe and ye deed shall ryse incorruptible and we shalbe chaunged.
wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53 For this corruptible must put on incorruptibilite: and this mortall must put on immortalite.
Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54 When this corruptible hath put on incorruptibilite and this mortall hath put on immortalite: then shalbe brought to passe ye sayinge yt is writte. Deeth is consumed in to victory.
Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!”
55 Deeth where is thy stynge? Hell where is thy victory? (Hadēs g86)
“Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs g86)
56 The stynge of deeth is synne: and the strength of synne is the lawe.
Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57 But thankes be vnto God which hath geven vs victory thorow oure Lorde Iesus Christ.
Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58 Therfore my deare brethren be ye stedfast and unmovable alwayes ryche in the workes of the Lorde for as moch as ye knowe how yt youre labour is not in vayne in the Lorde.
Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.

< 1 Corinthians 15 >