< 1 Corinthians 12 >

1 In spirituall thinges brethren I wolde not have you ignoraunt.
Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2 Ye knowe that ye were gentyls and went youre wayes vnto domme ydoles even as ye were ledde.
Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3 Wherfore I declare vnto you that no man speakynge in the sprete of god defieth Iesus. Also no man can saye that Iesus is the lorde: but by the holy goost.
Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: “Yesu alaaniwe!” Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: “Yesu ni Bwana,” asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4 Ther are diversities of gyftes verely yet but one sprete.
Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5 And ther are differences of administracions and yet but one lorde.
Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6 And ther are divers maners of operacions and yet but one God which worketh all thinges that are wrought in all creatures.
Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7 The gyftes of ye sprete are geven to every man to proffit ye congregacion.
Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8 To one is geven thorow the spirite the vtteraunce of wisdome? To another is geven the vtteraunce of knowledge by ye same sprete.
Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9 To another is geuen fayth by ye same sprete. To another ye gyftes of healynge by the same sprete.
Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10 To another power to do myracles. To another prophesie? To another iudgement of spretes. To another divers tonges. To another the interpretacion of toges.
humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11 And these all worketh eve ye silfe same sprete devydynge to every man severall gyftes even as he will.
Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12 For as the body is one and hath many mebres and all the membres of one body though they be many yet are but one body: even so is Christ.
Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote—ingawaje ni vingi—hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13 For in one sprete are we all baptysed to make one body whether we be Iewes or getyls whether we be bonde or fre: and have all dronke of one sprete.
Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14 For the body is not one member but many.
Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15 Yf the fote saye: I am not the honde therfore I am not of the body: is he therfore not of ye body:
Kama mguu ungejisemea: “Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili”, je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16 And if ye eare saye I am not the eye: therfore I am not of the body: is he therfore not of the body?
Kama sikio lingejisemea: “Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili”, je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17 If all the body were an eye where were then the eare? If all were hearynge: where were the smellynge?
Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18 But now hath god disposed the membres every one of them in the body at his awne pleasure.
Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19 If they were all one member: where were the body?
Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Now are ther many membres yet but one body.
Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21 And the eye can not saye vnto the honde I have no nede of the: nor ye heed also to the fete. I have no nede of you.
Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: “Sikuhitaji wewe”, wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Siwahitaji ninyi.”
22 Ye rather a greate deale those mebres of the body which seme to be most feble are most necessary.
Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23 And apo those mebres of yt body which we thinke lest honest put we most honestie on. And oure vngodly parties have most beauty on.
Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24 For oure honest members nede it not. But God hath so disposed the body ad hath geven most honoure to that parte which laked
ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25 lest there shuld be eny stryfe in the body: but that the members shuld indifferetly care one for another.
ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26 And yf one member suffer all suffer with him: yf one member be had in honoure all members be glad also.
Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Ye are the body of Christ and members one of another.
Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28 And God hath also ordeyned in the congregacion fyrst the Apostels secodarely prophetes thyrdly teachers then the that do miracles: after that the gyftes of healynge helpers governers diversite of tonges.
Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29 Are all Apostles? Are all Prophetes? Are all teachers? Are all doars of miracles?
Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30 Have all the gyftes of healinge? Do all speake wt tonges? Do all interprete?
Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31 Covet after ye best giftes. Amd yet shewe I vnto you a moare excellent waye.
Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.

< 1 Corinthians 12 >