< 1 Corinthians 12 >

1 In spirituall thinges brethren I wolde not have you ignoraunt.
Kuhusu karama za rohoni, kaka na dada zangu sitaki mkose kufahamu.
2 Ye knowe that ye were gentyls and went youre wayes vnto domme ydoles even as ye were ledde.
Mwajua ya kuwa mlipokuwa wapagani mliongozwa kufuata sanamu zisizoongea, kwa njia zozote mliongozwa nazo.
3 Wherfore I declare vnto you that no man speakynge in the sprete of god defieth Iesus. Also no man can saye that Iesus is the lorde: but by the holy goost.
Kwa hiyo, nataka mfahamu kwamba hakuna yeyote anenaye kwa Roho wa Mungu akisema, “Yesu amelaaniwa.” Hakuna yeyote atakayesema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
4 Ther are diversities of gyftes verely yet but one sprete.
Basi kuna karama tofauti tofauti, bali Roho ni yeye yule.
5 And ther are differences of administracions and yet but one lorde.
Na kuna huduma tofauti tofauti, bali Bwana ni yeye yule.
6 And ther are divers maners of operacions and yet but one God which worketh all thinges that are wrought in all creatures.
Na kuna aina mbalimbali za kazi, lakini Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
7 The gyftes of ye sprete are geven to every man to proffit ye congregacion.
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 To one is geven thorow the spirite the vtteraunce of wisdome? To another is geven the vtteraunce of knowledge by ye same sprete.
Maana mtu mmoja amepewa na Roho neno la hekima, na mwingine neno la maarifa kwa Roho yule yule.
9 To another is geuen fayth by ye same sprete. To another ye gyftes of healynge by the same sprete.
Kwa mwingine humpa imani kwa Roho yeye yule, na kwa mwingine karama ya uponyaji kwa Roho mmoja.
10 To another power to do myracles. To another prophesie? To another iudgement of spretes. To another divers tonges. To another the interpretacion of toges.
Kwa mwingine matendo ya nguvu, na mwingine unabii. Na kwa mwingine uwezo wa kupambanua roho, mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingnine tafsiri za lugha.
11 And these all worketh eve ye silfe same sprete devydynge to every man severall gyftes even as he will.
Lakini Roho ni yule yule atendaye kazi hizi zote, kumpa kila mtu karama kwa kadiri ya uchaguzi wake mwenyewe.
12 For as the body is one and hath many mebres and all the membres of one body though they be many yet are but one body: even so is Christ.
Kwa maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote ni vya mwili ule ule, vivyo hivyo na Kristo.
13 For in one sprete are we all baptysed to make one body whether we be Iewes or getyls whether we be bonde or fre: and have all dronke of one sprete.
Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi au Wayunani, kwamba tu watumwa au huru, na wote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 For the body is not one member but many.
Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.
15 Yf the fote saye: I am not the honde therfore I am not of the body: is he therfore not of ye body:
Ikiwa mguu utasema, “kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo haiufanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
16 And if ye eare saye I am not the eye: therfore I am not of the body: is he therfore not of the body?
Na ikiwa sikio litasema, “kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo hailifanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
17 If all the body were an eye where were then the eare? If all were hearynge: where were the smellynge?
Kama mwili wote utakuwa jicho, kungekuwa wapi kusikia? Kama mwili wote ukiwa sikio, kungekuwa wapi kunusa?
18 But now hath god disposed the membres every one of them in the body at his awne pleasure.
Lakini Mungu aliweka kila kiungo cha mwili mahali pake kama alivyopanga mwenyewe.
19 If they were all one member: where were the body?
Na kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Now are ther many membres yet but one body.
Hivyo sasa viungo ni vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 And the eye can not saye vnto the honde I have no nede of the: nor ye heed also to the fete. I have no nede of you.
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “sina haja na wewe.” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, sina haja na ninyi.”
22 Ye rather a greate deale those mebres of the body which seme to be most feble are most necessary.
Lakini viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa na heshima kidogo vyahitajika zaidi.
23 And apo those mebres of yt body which we thinke lest honest put we most honestie on. And oure vngodly parties have most beauty on.
Na viungo vya mwili tunavyodhani vina heshima kidogo, twavipa heshima zaidi, na viungo vyetu visivyo na mvuto vina uzuri zaidi.
24 For oure honest members nede it not. But God hath so disposed the body ad hath geven most honoure to that parte which laked
Na sasa viungo vyetu vilivyo na mvuto havina haja ya kupewa heshima, kwa kuwa tayari vina heshima. Lakini Mungu ameviunganisha viungo vyote pamoja, na amevipa heshima zaidi vile visivyo heshimiwa.
25 lest there shuld be eny stryfe in the body: but that the members shuld indifferetly care one for another.
Alifanya hivyo ili pasiwepo mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyote vitunzane kwa upendo wa mmoja.
26 And yf one member suffer all suffer with him: yf one member be had in honoure all members be glad also.
Na wakati kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vyaumia kwa pamoja. Au wakati kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vyote vifurahi kwa pamoja.
27 Ye are the body of Christ and members one of another.
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
28 And God hath also ordeyned in the congregacion fyrst the Apostels secodarely prophetes thyrdly teachers then the that do miracles: after that the gyftes of healynge helpers governers diversite of tonges.
Na Mungu ameweka katika kanisa kwanza mitume, pili manabii, tatu waalimu, kisha wale wote watendao matendo makuu, kisha karama za uponyaji, wale wasaidiao, wale wafanyao kazi ya kuongoza, na wote walio na aina mbalimbali za lugha.
29 Are all Apostles? Are all Prophetes? Are all teachers? Are all doars of miracles?
Je sisi sote ni mitume? Sisi sote ni manabii? Sisi sote ni waalimu? Je sisi sote tunafanya matendo ya miujiza?
30 Have all the gyftes of healinge? Do all speake wt tonges? Do all interprete?
Je sisi sote tuna karama ya uponyaji? Sisi sote tunaongea kwa lugha? Sisi sote tunatafsiri lugha?
31 Covet after ye best giftes. Amd yet shewe I vnto you a moare excellent waye.
Tafuteni sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi.

< 1 Corinthians 12 >