< Leviticus 6 >

1 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana alisema na Musa kumwabia,
2 “If any one of you you sins against me by deceiving someone—if you refuse to return what someone has lent you, or if you steal something of his, or if you find something and claim that you do not have it,
“Kama mtu akifanya dhambi na kuvunja amri kinyume na Bwana, kama kujihusisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani cha kutokuwa mwaminifu, au kama akidanganya au kuiba au amemdhurumu jirani.
3 you are guilty. You must return to its owner what you have stolen or what someone has lent you and you have not returned, or what you found that someone else had lost,
Au akiokota kitu fulani ambacho jirani yake amepoteza na kusema uongo kuhusu hicho, na kuapa kwa uongo au kwa mambo kama haya ambayo watu wanaweza kutenda dhambi.
4 or whatever you lied about.
Ndipo itakuwa hivi, kama ametenda dhambi na hatia, kwamba lazima akirudishe kwa vyovyote alichoiba au kudanganya au amedhurumu au kitu kilichopotea naye kukiokota.
5 You must not only return anything like that to its owner, but you must also pay to the owner one-fifth of its value.
Au kama amedanganya kwa jambo lolote, lazima atakirudisha kamilina kuongezea sehemu ya tano kwa kumlipa anayedai, kwa siku ile anayopatikana na hatia.
6 You must also bring to the Supreme Priest a ram to be an offering to me in order that you will no longer be guilty. The ram that you bring must be one that has no defects, one that has the value that has been officially determined.
Ataleta sadka ya hatia kwa Bwana: kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi lake kulingana na thamani yake, kama sadaka ya hatia kwa kuhani.
7 Then he will offer that ram to be a sacrifice that will cause you to no longer be guilty, and you will be forgiven for the wrong things that you did.”
Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele ya Bwana, atakuwa amesamehewa kulingana na chochote kilicho mfanya kuwa na hatia.”
8 Yahweh also said to Moses/me,
Ndipo Bwana alisema na Musa kumwambia,
9 “Tell this to Aaron and his sons: These are the regulations concerning the offerings that will be completely burned [on the altar]: The offering must remain on the altar all during the night, and the fire on the altar must always be kept burning.
“Mwagize Haruni na wanawe, kusema, 'hii ni sheria ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa lazima iwe juu ya makaa ya madhabahu usiku wote hata asubuhi, na moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.
10 [The next morning] the priest must put on his linen under-clothes and linen outer clothes. Then he must remove the ashes of the offering from the fire and put them beside the altar.
Kuhani atavaa nguo zake za kitani na atavaa nguo za kitani ndani yake. Atatoa majivu yaliyobaki baada ya moto kutekeza sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu, na ataweka majivu pembeni mwa madhabahu.
11 Then he must take off those clothes and put on other clothes, and take the ashes outside the camp, to a place that is acceptable to me.
Atavua mavazi haya na kuvaa mavazi mengine ili kuchukua majivu nje ya kambi na kupeleka mahali palipo safi.
12 The fire on the altar must always be kept burning; the priest must not allow it to (go out/quit burning). Each morning the priest must put more firewood on the fire. Then he must arrange more offerings on the fire, and burn on the altar the fat of the offerings to be burned to maintain fellowship [with me].
Moto katika madhabahu utaendelea kuwaka. Usizimike, na kuhani ataongeza kuni kila asubuhi. Atapanga juu yake sadaka ya kuteketezwa kama inavyotakiwa, na atateketeza juu yake mafuta ya sadaka ya amani.
13 The fire on the altar must be kept burning continually; the priest must not allow it to go out.”
Moto lazima utaendelea kuwaka katika madhabahu, kamwe usizimike.
14 “These are the regulations concerning the offerings made from grain: Aaron’s sons must bring them to me in front of the altar.
Hii ni sheria ya sadaka ya nafaka. Wana wa Haruni watatoa mbele ya Bwana katika madhabahu.
15 The priest must take a handful of fine flour mixed with olive oil and incense and burn that on the altar. That handful will signify that the whole offering truly belongs to me. And the aroma while it burns will be pleasing to me.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini wa sadaka ya nafaka na mafuta na ubani ambao uko juu ya sadaka ya nafaka, atateketeza juu ya madhabahu kuleta harufu nzuri ya shukrani ya kumpendeza Bwana.
16 Aaron and his sons may eat the remaining part of the grain offering. But they must eat it in a holy place, in the courtyard of the Sacred Tent.
Haruni na wanae watakula sadaka inayobaki, italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu. Watakula katika ua ya hema ya kukutania.
17 It must not have yeast mixed with it. Like the offerings for sin and the offerings to cause people to no longer be guilty of sin, that offering is very holy.
Haitaokwa pamoja na chachu. Nimewapa kama sehemu ya sadaka yangu itolewayo kwa moto, ni takatifu sana, kama sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
18 Any male descendants of Aaron are permitted to eat it, because it is forever their regular share of the offerings given to me and burned in the fire [on the altar]. Anyone else who touches those offerings made from grain will be punished by God.”
Kwa nyakati zote zijazo kupitia watu wa kizazi chako, mwanaume yeyote mzaliwa kutoka kwa Haruni aweza kula ni sehemu yake, ichukuliwayo katika sadaka ya Bwana kwa moto. Yeyote anayeigusa atakuwa mtakatifu.”
19 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana aliongea tena na Musa kumwambia,
20 “Tell Aaron and his sons that this is the offering that they must bring to Yahweh on the day that any of them (is ordained/becomes a priest): That person must bring two quarts/liters of fine flour as an offering made from grain. He must bring half of it in the morning and half of it in the evening.
“Hii ni sadaka ya Haruni na wanawe ambayo watatoa kwa Bwana katika siku ambayo kila mwana atawekwa wakfu: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama kawaida sadaka ya nafaka nusu yake asubuhi na nusu yake jioni.
21 He must mix it well with olive oil and bake it in a shallow pan. He must then break it into small pieces to be burned [on the altar]. And the aroma while it burns will be pleasing to Yahweh.
Itatengenezwa na mafuta katika kikaango, utaileta ikiwa imeandaliwa imeokwa katika vipande utatoa sadaka ya nafaka ili kuleta harufu nzuri kwa Bwana.
22 I have commanded that the descendants of Aaron who are appointed in turn to become the Supreme Priests after Aaron dies are the ones who must prepare those things. These offerings must be completely burned [on the altar] to be sacrifices to me, Yahweh.
Mwana wa Kuhani Mkuu atakayekuwa Kuhani Mkuu mpya kutoka miongoni mwa wanawe ataitoa. Kama amri ya milele, yote itateketezwa kwa Bwana.
23 Every offering that a priest gives that is made from grain must be completely burned; none of it is to be eaten.”
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itatekezwa yote. Haitaliwa kamwe.”
24 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana alisema tena Musa, kumwambia,
25 “Tell Aaron and his sons: These are the regulations concerning the offerings that people must bring to me so that I will forgive the people for the sins they have committed:
“Sema na Haruni na watoto wake kwamba, 'Hii ni sheria ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi lazima kuchinjwa mahali pa sadaka ya kuteketezwa itachinjwa mbeleya Bwana. Ni takatifu sana.
26 The animals must be slaughtered in my presence in the same place that the animals that are to be completely burned [on the altar] are slaughtered, in the courtyard in front of the Sacred Tent.
Kuhani atakayeitoa kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila. Italiwa mahali patakatifu katika ua wa hema ya kukutania.
27 Any other person who touches any of its meat will be punished by God. And if its blood is splattered on your clothes, you must wash the clothes in a holy place.
Yeyote atakayeigusa nyama yake atakuwa ni mtakatifu na kama damu itadondokea mavazi yatafuliwa mahali palipodondokewa, mahali patakatifu.
28 If the meat is cooked in a clay pot, the pot must be broken [afterwards]. But if it is cooked in a bronze pot, the pot must be scoured [afterwards] and rinsed with water.
Lakini chungu kikipikiwa kitavunjwa, kama imepikiwa katika chombo cha shaba, lazima kitasuguliwa na kusafishwa kwa maji.
29 Any male in a priest’s family may eat some of the cooked meat; that meat is very holy.
Mwanaume yeyote miongoni mwa makuhani anaweza kula nyama hiyo kwa sababu ni takatifu sana.
30 But if the blood of those sin offerings is brought into the Sacred Tent to enable the people to be forgiven for having sinned, the meat of those animals must not be eaten. The meat must be completely burned.”
Na hakuna sadaka ya dhambi italiwa ambayo damu yake imeletwa katika hema ya kukutania kufanya upatanisho katika mahali patakatifu. Ni lazima iteketezwe.

< Leviticus 6 >