< Colossians 2 >

1 I want for you to know how great a struggle I am having (for *N+kO) you and those in Laodicea and as many as not have seen the face of me in [the] flesh,
Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
2 that may be encouraged the hearts of them (being knit together *N+kO) in love and to (all *N+kO) (the *o) (richness *N+kO) of the full assurance of understanding to [the] knowledge of the mystery of God (and *K) (Father *KO) (and *K) (the *KO) Christ,
Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
3 in whom are all the treasures of wisdom and of knowledge hidden;
Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
4 This (now *ko) I say so that (no one *N+kO) you may delude by persuasive speech;
Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
5 If truly even in the flesh I am absent, yet in spirit with you I am, rejoicing and seeing your good order and the firmness of the in Christ faith of you.
Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
6 Just as therefore you have received Christ Jesus the Lord, in Him do walk
Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
7 rooted and being built up in Him and being strengthened in (in *ko) the faith even as you were taught, abounding (in to her *ko) with thanksgiving.
Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
8 do take heed lest anyone you there will be who is taking captive through philosophy and empty deceit according to the tradition of men, according to the principles of the world and not according to Christ;
Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
9 For in Him dwells all the fullness of the Deity bodily,
Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
10 and you are in Him completed, who is the head of all rule and authority;
nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
11 in whom also you were circumcised with [the] circumcision made without hands in the removal of the body (of the sins *K) of the flesh, in the circumcision of Christ,
Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
12 having been buried with Him in (baptism *N+kO) in which also you were raised with [Him] through the faith of the working of God the [One who] having raised Him out from (the *k) dead.
Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
13 And you dead being in the trespasses and in the uncircumcision of the flesh of you, He made alive together (you *NO) with Him having forgiven us all the transgressions;
Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
14 having blotted out the against us handwriting in the decrees which was adverse to us, and it He has taken out of the way having nailed it to the cross;
alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
15 Having disarmed the rulers and the authorities He disgraced [them] in public, having triumphed over them in it.
Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
16 Not therefore anyone you should judge in regard to food (or *N+kO) in regard to drink or in regard to a feast or a New Moon or Sabbaths,
Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
17 which are a shadow of the [things] coming, the however body [is] of Christ.
Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
18 No one you should disqualify delighting in humility and [the] worship of the angels, which (not *K) he has seen detailing vainly being puffed up by the mind of the flesh of him,
Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
19 and not holding fast to the head from whom all the body through the joints and ligaments being supplied and being knit together it increases with the increase of God.
na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
20 If (therefore *K) you have died with Christ away from the principles of the world, why as if living in [the] world do you submit to decrees?
Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
21 Not you may handle Not you may taste Not you may touch!
“Msishike hiki,” “Msionje kile,” “Msiguse kile!”
22 which are all unto decay with the use according to the commandments and teachings of men;
Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
23 which are an appearance indeed having of wisdom with self-imposed worship and with humility and with harsh treatment of [the] body, not of honor a certain against [the] indulgence of the flesh.
Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.

< Colossians 2 >