< 2 Thessalonians 1 >

1 Paul and Silvanus and Timothy To the church of [the] Thessalonians in God [the] Father of us and in the Lord Jesus Christ:
Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
2 Grace to you and peace from God [the] Father of us and [the] Lord Jesus Christ.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 To thank we ought God always concerning you, brothers, even as fitting it is, because is increasing exceedingly the faith of you and is abounding the love of one each of all you to one another;
Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
4 so as for ourselves us in you (to greatly boast *N+kO) in the churches of God about the perseverance of you and faith in all the persecutions of you and in the tribulations that you are bearing,
Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
5 [This is] a plain token of the righteous judgment of God unto to be accounted worthy you of the kingdom of God for which also you suffer;
Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
6 if indeed if indeed righteous [it is] with God to repay those oppressing you with affliction
Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
7 and to you those being oppressed repose with us at the revelation of the Lord Jesus from heaven with [the] angels mighty of Him
na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
8 in (a fire of flame, *NK+o) inflicting vengeance on those not knowing God and on those not obeying the gospel of the Lord of us Jesus (Christ; *K)
na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
9 who [the] penalty will suffer of destruction eternal away from [the] presence of the Lord and from the glory of the power of Him, (aiōnios g166)
Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios g166)
10 when He may come to be glorified in the saints of Him and to be marveled at among all those (having believed, *N+kO) because was believed the testimony of us to you in the day that.
wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
11 for which also we pray always for you that you He may count worthy of the calling of the God of us and He may fulfill every good pleasure of goodness and work of faith with power,
Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
12 so that may be glorified the name of the Lord of us Jesus (Christ *K) in you and you in Him according to the grace of the God of us and [the] Lord Jesus Christ.
Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.

< 2 Thessalonians 1 >