< 1 Thessalonians 5 >

1 Concerning now the times and the seasons, brothers, no need you have to you to be written;
Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2 Yourselves for fully you know that (the *k*) day of [the] Lord as a thief by night in this manner comes;
Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3 when (for *k*) they may say; Peace and security, then suddenly upon them comes destruction as the labor pains to her in womb [pregnancy] having, and certainly not shall they escape.
Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4 You yourselves however, brothers, not are in darkness, that the day you like (a thief *NK(O)*) may grasp;
Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5 All (for *no*) you yourselves sons of light are and sons of day; Not we are of night nor of darkness.
Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6 So then not we may sleep as (also *k*) the others but we may watch and we may be sober.
Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7 Those for sleeping by night sleep and those becoming drunk by night get drunk;
Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8 We ourselves however of [the] day being may be sober having put on [the] breastplate of faith and love and [the] helmet [the] hope of salvation;
Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9 because not has destined us God for wrath but for obtaining salvation through the Lord of us Jesus Christ
Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10 the [One who] having died (for *NK(o)*) us, so that whether we shall watch or we shall sleep together with Him we may live.
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11 Therefore do encourage one another and do build up one another even as also you are doing.
Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12 We implore however you, brothers, to know those toiling among you and taking the lead over you in [the] Lord and admonishing you
Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13 and to esteem them super overexcessively super overexcessively super overexcessively in love because of the work of them. do be at peace among (yourselves. *NK(O)*)
Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14 We exhort now you, brothers, do admonish the unruly, do encourage the fainthearted, do help the weak, do be patient toward all.
Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15 do see that no one evil for evil to anyone may repay, but always the good do pursue also toward one another and toward all.
Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16 Always do rejoice;
Furahini daima,
17 Unceasingly do pray;
salini kila wakati
18 In everything do give thanks; this for [is the] will of God in Christ Jesus toward you.
na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19 The Spirit not do quench;
Msimpinge Roho Mtakatifu;
20 Prophecies not do despise;
msidharau unabii.
21 All things (now *no*) do test; To the good do hold fast;
Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22 From every form of evil do abstain.
na epukeni kila aina ya uovu.
23 Himself now the God of peace would sanctify you completely, and entirely your spirit and soul and body blameless at the coming of the Lord of us Jesus Christ would be preserved.
Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 [Is] faithful the [One] calling you, who also will do [it].
Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25 Brothers, do pray (also *no*) for us.
Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26 do greet the brothers all with a kiss holy.
Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27 (I adjure *N(k)O*) you [by] the Lord to be read [this] letter to all the (saints *K*) brothers.
Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28 The grace of the Lord of us Jesus Christ [be] with you. (Amen. *KO*) (to Thessalonica first It was written from Athens. *K*)
Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< 1 Thessalonians 5 >