< Colossians 1 >

1 Paul an apostle of Christ Jesus through [the] will of God and Timothy the brother
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2 To those in Colossae saints and faithful brothers in Christ: Grace to you and peace from God [the] Father of us (and Lord Jesus Christ. *K)
tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3 We give thanks to the God (and *ko) Father of the Lord of us Jesus Christ continually (for *NK+o) you praying,
Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4 having heard of the faith of you in Christ Jesus and the love (that *N+kO) (you have *no) toward all the saints,
Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5 because of the hope which is being laid up for you in the heavens which you heard of before in the word of truth the gospel
Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6 which is being present unto you, even as also in all the world (and *k) it is bearing fruit (and increasing *NO) even as also among you from the day you heard and you knew the grace of God in truth,
Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7 even as (and *k) you learned from Epaphras the beloved fellow bond-servant of us, who is faithful on behalf of (of you *NK+O) a servant of Christ,
Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8 the [one] also having made known to us your love in [the] Spirit.
Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9 Because of this also we ourselves from the day we heard, not cease for you praying and asking that you may be filled with the knowledge of the will of Him in all wisdom and in understanding spiritual
Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10 to walk (you *k) worthily of the Lord in all pleasing in every work good bringing forth fruit and growing (into *k) (knowledge *N+kO) of God,
Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11 with all power being strengthened according to the might glorious of Him unto all endurance and patience with joy.
Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12 giving thanks to the Father the [One] having qualified (you *N+KO) for the share of the inheritance of the saints in the light,
Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13 who has delivered us from the dominion of darkness and transferred [us] into the kingdom of the Son the beloved of Him,
Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14 in whom we have redemption (through the blood of him *K) the forgiveness of sins;
ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15 [He] is [the] image of the God invisible, [the] firstborn over all creation;
Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 because in Him were created all things (which [are] *k) in the heavens and upon the earth, the visible and the invisible, whether thrones or dominions or rulers or authorities; all things through Him and unto Him have been created,
Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17 And He himself is before all things, and all things in Him have held together,
Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18 And He himself is the head of the body the church; who is (the *o) beginning, firstborn out from the dead, so that may be in all things He himself holding preeminence;
Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19 because in Him was pleased all the fullness to dwell
Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20 and through Him to reconcile all things to Himself, having made peace through the blood of the cross of Him, through Him whether the [things] on the earth or the [things] (in *NK+o) the heavens;
Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21 And you once being alienated and hostile in mind in the deeds evil, now however (He has reconciled [You] *NK+O)
Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22 in the body of the flesh of Him through death to present you holy and unblemished and blameless before Him.
Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23 if indeed you continue in the faith established and firm and not being moved away from the hope of the gospel that you have heard, which having been proclaimed in all creation under heaven, of which have become I myself Paul a minister.
Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24 Now I rejoice in the sufferings (of mine *k) for you and I am filling up that which is lacking of the tribulations of Christ in the flesh of mine for the body of Him which is the church;
Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25 of which became I myself a minister according to the administration of God which having been given me toward you to complete the word of God,
Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26 the mystery which hidden from the ages and from the generations, (now *N+kO) however having been manifested to the saints of Him; (aiōn g165)
ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
27 to whom has willed God to make known (what the *N+kO) riches of the glory of the mystery this among the Gentiles, (which *N+kO) is Christ in you, the hope of glory;
Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28 whom we ourselves preach admonishing every man and teaching every man in all wisdom, so that we may present every man perfect in Christ (Jesus *K)
Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29 Unto this also I toil striving according to the energy of Him who is working in me myself in power.
Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.

< Colossians 1 >