< 1 Thessalonians 1 >

1 Paul and Silvanus and Timothy To the church of the Thessalonians in God [the] Father and in [the] Lord Jesus Christ: Grace to you and peace (from of God Father of us and Lord Jesus Christ. *K)
Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba, na wa Bwana Yesu Kristo.
2 We give thanks to God always concerning all of you mention (of you *k) making in the prayers of us,
Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.
3 unceasingly remembering your work of faith and labor of love and the endurance of the hope of the Lord of us Jesus Christ before the God and Father of us;
Maana, mbele ya Mungu Baba yetu, twakumbuka jinsi mnavyoonyesha imani yenu kwa matendo, jinsi upendo wenu unavyowawezesha kufanya kazi kwa bidii, na jinsi tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo lilivyo thabiti.
4 knowing, brothers beloved by God, the election of you;
Ndugu, twajua kwamba Mungu anawapenda na kwamba amewateua muwe watu wake,
5 because the gospel of us not came to you in word only but also in power and in [the] Spirit Holy and with full assurance much even as you know what we were among you on account of you;
maana wakati tulipowahubirieni ile Habari Njema haikuwa kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, tukiwa na hakika kwamba ujumbe huo ulikuwa wa kweli. Mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi; tuliishi kwa manufaa yenu.
6 And you yourselves imitators of us became and of the Lord having received the word in tribulation much with [the] joy of [the] Spirit Holy,
Ninyi mlifuata mfano wetu, na kumwiga Bwana. Ingawa mliteswa sana, mliupokea ujumbe huo kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
7 so as for to became you (an example *N+KO) to all the believing [ones] in Macedonia and (in *no) Achaia.
Kwa hiyo ninyi mmekuwa mfano mzuri kwa waumini wote wa Makedonia na Akaya.
8 From you for has sounded forth the word of the Lord not only in Macedonia and (in *no) Achaia, but (also *k) in every place the faith of you toward God has gone abroad, so as for not need to have us to say anything.
Maana, kutokana na bidii yenu ujumbe wa Bwana umesikika si tu huko Makedonia na Akaya, bali imani yenu kwa Mungu imeenea popote. Tena hatuhitaji kusema zaidi.
9 They themselves for concerning us report what reception (we had *N+kO) from you, and how you turned to God from idols to serve [the] God living and true
Watu hao wanazungumza juu ya ziara yetu kwenu: jinsi mlivyotukaribisha, jinsi mlivyoziacha sanamu mkamgeukia Mungu aliye hai na wa kweli,
10 and to await the Son of Him from the heavens, whom He raised out from the dead, Jesus who is delivering us (from *N+kO) the wrath which is coming.
na sasa mwamngojea Mwanae ashuke kutoka mbinguni, Yesu, ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu, na ambaye anatuokoa katika ghadhabu ya Mungu inayokuja.

< 1 Thessalonians 1 >