< Revelation 1 >

1 The Revelation of Jesus Christ, which God gave to him, to point out unto his servants the things which must needs come to pass with speed, —and he shewed them by signs, sending through his messenger, unto his servant John;
Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
2 who bare witness as to the word of God, and the witness of Jesus Christ, —whatsoever things he saw.
naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
3 Happy! he that readeth, and they who hear, the words of the prophecy, and keep the things, therein, written; for, the season, is, near.
Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
4 John, unto the Seven Assemblies which are in Asia, Favour to you, and peace, from—Him who Is, and who Was, and who is Coming, and from—The Seven Spirits which are before his throne,
Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5 and from—Jesus Christ, —The Faithful Witness, The Firstborn of the Dead, and The Ruler of the Kings of the Earth. Unto him that loveth us, and loosed us out of our sins with his blood, —
na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
6 and he hath made us [to be] a kingdom—priests unto his God and Father, Unto him, be the glory, and the dominion, unto the ages. Amen. (aiōn g165)
akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
7 Lo! he cometh with the clouds, and every eye shall see him, such also as pierced him; and all the tribes of the land shall smite themselves for him. Yea! Amen.
Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
8 I, am, the A, and, the Z, saith the Lord, —the, God who Is, and who Was, and who is Coming, The Almighty.
“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
9 I, John, your brother, and partaker with you in the tribulation and kingdom and endurance in Jesus, came to be in the isle that is called Patmos, because of the word of God, and the witness of Jesus.
Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
10 I came to be, in Spirit, in the Lord’s Day, and heard, behind me, a loud voice, as of a trumpet,
Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
11 saying—What thou seest, write in a scroll, and send unto the Seven Assemblies, —unto Ephesus, and unto Smyrna, and unto Pergamum, —and unto Thyatira, and unto Sardis, and unto Philadelphia, —and unto Laodicea.
Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
12 And I turned round, to see the Voice which was speaking with me, and, having turned, I saw Seven Lamps of gold;
Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
13 and, in the midst of the lamps, One like unto a Son of Man: —clothed with a robe, reaching to the feet, and girt about at the breasts with a girdle of gold,
na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
14 And his head and hair, white, like white wool—like snow, and, his eyes, like a flame of fire,
Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
15 And, his feet, like unto glowing copper, as if in a furnace refined, and, his voice, like a sound of many waters,
miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
16 And, having in his right hand, seven stars, and, out of his mouth, a sharp, two-edged sword, going forth; and, his whole appearance, as when, the sun, shineth in its strength.
Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
17 And, when I saw him, I fell at his feet as dead, and he laid his right hand upon me, saying—Do not fear! I, am the First, and the Last,
Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
18 and the Living One, —and I became dead; —and lo! living, am I, unto the ages of ages, and have the keys of death and of hades. (aiōn g165, Hadēs g86)
Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Write, therefore—what things thou hast seen and what they are; and what things are about to come to pass, after these things:
Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
20 The sacred secret of the seven stars, which thou sawest upon my right hand, and the seven lamps of gold: —The seven stars, are, messengers of the seven assemblies, and, the seven lamps, are, seven assemblies
Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.

< Revelation 1 >