< Jude 1 >

1 Jude, Jesus Christ’s servant, and brother of James, unto, the called, by God the Father, beloved, and, by Jesus Christ preserved, —
Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
2 Mercy to you, and peace, and love, be multiplied!
Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
3 Beloved! though I was using all diligence to be writing unto you concerning our common salvation, yet have I had necessity to write at once unto you, exhorting you to be earnestly contending for, the faith, once for all delivered unto the saints.
Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
4 For there have crept in unobserved certain men, who, from of old, have been publicly notified for this sentence, ungodly, men, the favour of our God, turning into wantonness, and, our only Master and Lord, Jesus Christ, denying.
Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
5 I am minded, therefore, to put you in remembrance, —though ye know all things once for all, That the Lord, when a people out of Egypt he had saved, in, the next place, them that believed not, destroyed.
Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 Messengers also, even them who had not kept their own principality, but had forsaken their proper dwelling, unto the judgment of the great day in perpetual bonds under thick gloom, hath he reserved. (aïdios g126)
Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu. (aïdios g126)
7 As, Sodom and Gomorrah, and the cities around them, having in like manner to these given themselves over to fornication, and gone away after other kind of flesh, lie exposed as an example, a penalty of age-abiding fire, undergoing. (aiōnios g166)
Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote. (aiōnios g166)
8 In like manner, nevertheless, even these, in their dreamings, flesh indeed defile, while lordship they set aside, and dignities they defame.
Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
9 Whereas, Michael, the chief-messenger, when, with the adversary, disputing, he was reasoning about the body of Moses, durst not impose on him a defamatory sentence, but said—The Lord rebuke thee!
Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: “Bwana mwenyewe na akukaripie.”
10 But, these, whatsoever things, indeed, they know not, they defame; but, whatsoever things, naturally, like the irrational creatures, they well understand, by these, are they, bringing themselves to ruin.
Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
11 Alas for them! because—in the way of Cain have they gone, and, in the error of Balaam’s wage, have they run riot, and, in the gainsaying of Korah, have they perished.
Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
12 These are they—who, in your love-feasts, are hidden rocks, as they fare sumptuously together, fearlessly, themselves, shepherding, —clouds without water, by winds swept along, trees autumnal, fruitless, twice dead, uprooted,
Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
13 Wild waves of sea, foaming out their own infamies, wandering stars, for whom the gloom of darkness age-abiding hath been reserved. (aiōn g165)
Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu. (aiōn g165)
14 But the seventh from Adam, Enoch, prophesied, even of these, saying—Lo! the Lord hath come with his holy myriads, —
Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: “Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
15 To execute judgment against all, and to convict all the ungodly—of all their works of ungodliness, which they committed in ungodliness, and of all the hard things which they have spoken against him—sinners, ungodly!
kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo.”
16 These, are murmurers, complainers, according to their covetings, going on, —and, their mouth, speaketh great swelling words, —holding persons in admiration, for profit’s sake.
Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
17 But, ye, beloved! remember the things which were foretold by the apostles of our Lord Jesus Christ,
Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
18 How that they used to say to you—In the last time, there shall be mockers, —according to their own ungodly covetings, going on.
Waliwaambieni: “Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.”
19 These, are they who make complete separation, mere men of soul, Spirit, not possessing.
Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
20 But, ye, beloved! building yourselves up in your most holy faith, in Holy Spirit, praying,
Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
21 Yourselves, in God’s love, keep, —awaiting the mercy of our Lord Jesus Christ, unto age-abiding life. (aiōnios g166)
na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake. (aiōnios g166)
22 And, on some, indeed, have mercy, —such as are in doubt, be saving, out of the fire, snatching them;
Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
23 But, on others, have mercy with fear, hating even, the garment, spotted by the flesh.
waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
24 Now, unto him who is able—to guard you from stumbling, and to set you in the presence of his glory, without blemish, with exultation, —
Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
25 Unto God alone our Saviour, through Jesus Christ our Lord, be glory, greatness, dominion, and authority, before all the [by-gone] age, and now, and unto all the [coming] ages. Amen! (aiōn g165)
kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)

< Jude 1 >