< Psalms 45 >

1 To the Chief Musician. On Shoshannim. For the Sons of Korah. A Psalm of Instruction. A Song of Love. Overflowed hath my heart, with an excellent theme, I will recite my poem concerning the king, Be, my tongue, [like] the pen of a scribe who is skilled.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 Most beautiful thou art, beyond the sons of men, Graciousness hath been poured forth by thy lips, For this cause, hath God blessed thee, to times age-abiding.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Gird thy sword upon thy thigh, O mighty one, [’Tis] thine honour and thy majesty;
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 And, [in] thy majesty, be successful! ride forth! on behalf of faithfulness, and humility—righteousness, And let thine own right hand show thee wonderful things.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Thine arrows, are sharp—Peoples, under thee, fall! In the heart of the foes of the king.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 Thy throne, O God, is to times age-abiding and beyond, A sceptre of equity, is the sceptre of thy kingdom.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 Thou hast loved righteousness, and hated lawlessness, —For this cause, hath God, thine own God, anointed thee, With the oil of gladness, beyond thy partners.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 Myrrh and aloes, cassias, all thy garments, —Out of the palaces of ivory, the tones of strings, have rejoiced thee.
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 Daughters of kings, are among thine honourable women, Stationed is the bride at thy right hand, in gold of Ophir.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Hearken, O daughter, and observe, Incline also thine ear, Forget, then, thine own people, And the house of thy father;
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 When the king shall desire thy beauty, Surely, he, is thy lord, then bow down to him.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 Also, the daughter of Tyre, [cometh in] with a present! Thy face, shall the rich of the people appease.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 All glorious—the daughter of a king [sitteth] within, Brocades, wrought with gold, [are] her clothing!
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 In embroidered raiment, shall she be brought unto the king—The virgins that follow her, her companions, are to be conducted unto thee:
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 They shall be brought, with rejoicings and exultation, —They shall enter into the palace of the king!
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 Instead of thy fathers, be thy sons, Thou shalt make them rulers in all the earth.
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 I will keep in remembrance thy Name, through each succeeding generation, For this cause, peoples, shall praise thee, to times age-abiding and beyond.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

< Psalms 45 >