< Psalms 57 >

1 To the Chief Musician. "Do not destroy." A precious Psalm, of David. When he fled from the face of Saul into the Cave. Show me favour, O God, Show me favour, For, in thee, hath my soul sought refuge, —And, in the shadow of thy wings, will I seek refuge, Until the storm of ruin pass by.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 I will cry unto God Most High, Unto GOD, who accomplisheth on my behalf:
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 He will send out of heaven, that he may save me, He who is panting for me, hath reproached. (Selah) God will send out his lovingkindness and his faithfulness.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 My soul, is in the midst of lions, I lie down amidst flames, As for the sons of men, Their teeth, are spear and arrows, And, their tongue, is a sharp sword.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Be exalted Above the Heavens, O God, Above all the earth, thy glory!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 A net, did they fix for my steps, My soul was bowed down, —They digged before me a pit, They fell into the midst thereof! (Selah)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Fixed is my heart, O God, Fixed is my heart, I will sing, and touch the strings.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Awake, mine honour, Awake, harp and lyre, I will awaken the dawn;
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 I will thank thee, among the peoples, O My Lord, I will praise thee in song, among the races of men.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 For, great, unto the heavens, is thy lovingkindness, And, unto the skies, thy faithfulness.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Be exalted Above the heavens, O God, Above all the earth, thy glory!
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< Psalms 57 >