< Joshua 1 >

1 And it came to pass, after the death of Moses the servant of Yahweh, —that Yahweh spake unto Joshua son of Nun, the attendant of Moses, saying:
Baada ya kifo cha Mose mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Mose:
2 Moses my servant, is dead, —Now, therefore, arise, pass over this Jordan, thou, and all this people, into the land which I am giving unto them—unto the sons of Israel.
“Mtumishi wangu Mose amekufa. Sasa basi, wewe pamoja na watu wote hawa, jiandaeni kuvuka huu Mto Yordani kuingia nchi ambayo karibu nitawapa wana wa Israeli.
3 Every place whereon the sole of your foot shall tread, unto you, have I given it, —as I spake unto Moses.
Kila mahali nyayo za miguu yenu zitakapokanyaga nimewapa, kama vile nilivyomwahidi Mose.
4 From the desert and this Lebanon, even unto the great river—the river Euphrates, all the land of the Hittites, and unto the great sea, toward the going in of the sun, shall be your boundary.
Nchi yenu itaenea kuanzia jangwa hili hadi Lebanoni, tena kuanzia mto mkubwa wa Frati, yaani nchi yote ya Wahiti, hadi Bahari ile Kubwa iliyoko upande wa magharibi.
5 No man shall stand before thee, all the days of thy life, —as I was with Moses, so I will be with thee, I will not fail thee, neither will I forsake thee.
Hakuna mtu yeyote atakayeweza kushindana na wewe siku zote za maisha yako. Kama vile nilivyokuwa pamoja na Mose, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe, sitakuacha wala sitakupungukia.
6 Be firm and bold, —for, thou, shalt cause this people to inherit the land which I sware unto their fathers, —to give unto them.
“Uwe hodari na shujaa, kwa sababu wewe ndiwe utakayewaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia baba zao kuwapa.
7 Only be very firm and bold, taking heed to do according to all the law which Moses my servant commanded thee, do not turn aside therefrom, to the right hand or to the left, —that thou mayest prosper, whithersoever thou goest.
Uwe hodari na uwe na ushujaa mwingi. Uwe na bidii kutii sheria yote aliyokupa Mose mtumishi wangu, usiiache kwa kugeuka kuelekea kuume au kushoto, ili upate kufanikiwa popote uendako.
8 This scroll of the law must not cease out of thy mouth, but thou must talk to thyself therein, day and night, that thou mayest take heed to do according to all that is written therein, —for, then, shalt thou make thy way prosperous, and, then, shalt thou have good success.
Usiache Kitabu hiki cha Sheria kiondoke kinywani mwako; yatafakari maneno yake usiku na mchana, ili upate kuwa mwangalifu kufanya kila kitu sawasawa na yote yaliyoandikwa ndani yake. Ndipo utakapofanikiwa na kisha utastawi.
9 Have I not commanded thee, Be firm and bold, do not start nor be dismayed, —for, with thee, is Yahweh thy God, whithersoever thou goest?
Je, si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na shujaa. Usihofu wala usivunjike moyo, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakuwa pamoja nawe kokote uendako.”
10 So then Joshua commanded the officers of the people, saying:
Ndipo Yoshua akawaagiza maafisa wa watu akisema,
11 Pass ye through the midst of the camp, and command the people, saying: Make ready for yourselves, provisions, —for, in three days more, are ye to pass over this Jordan, to go in and possess the land which Yahweh your God is giving you, to possess.
“Pitieni katika kambi yote mkawaambie watu, ‘Wekeni tayari mahitaji yenu. Siku tatu kuanzia sasa mtavuka hii Yordani ili kuingia na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa iwe yenu wenyewe.’”
12 And, unto the Reubenites, and unto the Gadites, and unto the half tribe of Manasseh, spake Joshua, saying:
Lakini kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, Yoshua akasema,
13 Remember the word which Moses the servant of Yahweh commanded you, saying, —Yahweh your God, is granting you rest, and doth give you this land.
“Kumbukeni agizo lile Mose mtumishi wa Bwana alilowapa: ‘Bwana Mungu wenu anawapa ninyi raha, naye amewapa nchi hii.’
14 Your wives, your little ones, and your cattle, shall remain in the land which Moses hath given you over the Jordan, —but, ye, shall pass over, armed, before your brethren, —all ye mighty men of valour, and shall help them;
Wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu watakaa katika nchi ile Mose aliyowapa mashariki ya Yordani, lakini mashujaa wenu wote, wakiwa wamevikwa silaha kikamilifu lazima wavuke mbele ya ndugu zenu. Imewapasa kuwasaidia ndugu zenu hadi
15 until that Yahweh shall grant rest unto your brethren, as unto you, so shall, they also, possess the land which Yahweh your God giveth them, —then shall ye return unto the land of your possession, and possess it, which Moses the servant of Yahweh hath given you over the Jordan, towards the rising of the sun.
Bwana awape nao raha, kama alivyokwisha kufanya kwa ajili yenu hadi wao pia watakapokuwa wamemiliki nchi ile Bwana Mungu wenu anayowapa. Baada ya hilo, mwaweza kurudi na kukalia nchi yenu wenyewe, ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa mashariki mwa Yordani kuelekea linakochomoza jua.”
16 Then responded they to Joshua, saying, —All that thou hast commanded us, will we do, and, whithersoever thou shalt send us, will we go:
Ndipo wakamjibu Yoshua, “Chochote ambacho umetuagiza tutafanya na popote utakapotutuma tutakwenda.
17 As in every thing we hearkened unto Moses, so, will we hearken unto thee, —only let Yahweh thy God be with thee, as he was with Moses.
Kama vile tulivyomtii Mose kikamilifu, ndivyo tutakavyokutii wewe. Bwana Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama vile alivyokuwa pamoja na Mose.
18 Any man who shall rebel against thy bidding, and not hearken unto thy words in all that thou shalt command him, shall be put to death, —only be firm and bold.
Yeyote atakayeasi neno lako na kuacha kuyatii maneno yako, au chochote utakachowaamuru, atauawa. Uwe imara na hodari tu!”

< Joshua 1 >