< Deuteronomy 1 >

1 These, are the words, which Moses spake unto all Israel, over the Jordan, —in the wilderness in the waste plain over against Suph, between Paran and Tophel, and Laban and Hazeroth and Di-zahab:
Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
2 eleven days from Horeb, by way of Mount Seir, as far as Kadesh-barnea.
(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
3 And it came to pass, in the fortieth year, in the eleventh month, on the first of the month, that Moses spake unto the sons of Israel, according to all that Yahweh had given him in charge for them;
Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
4 after he had smitten Sihon, king of the Amorites, who dwelt in Heshbon, —and Og, king of Bashan, who dwelt in Ashtaroth, in Edrei:
Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
5 over the Jordan, in the land of Moab, did Moses take in hand to expound this law, saying: —
Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
6 Yahweh our God, spake unto us in Horeb, saying, Long enough, have ye dwelt in this mountain:
Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
7 Turn ye and set yourselves forward, and enter into the hill country of the Amorites, and into all the places near, in the plain, in the mountain, and in the lowland, and in the south, and in the coast of the sea, —the land of Canaan and the Lebanon, as far as the great river, the river Euphrates.
Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
8 See! I have set before you the land, —enter and possess the land, which, Yahweh sware unto your fathers to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give unto them, and unto their seed, after them.
Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
9 So I spake unto you, at that time saying, I am unable, by myself, to carry you.
Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
10 Yahweh your God hath multiplied you, and here ye are to-day, like the stars of the heavens for multitude.
Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
11 Yahweh, the God of your fathers, be adding unto you the like of you, a thousand times, —and bless you, as he hath spoken unto you!
Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
12 How should I carry by myself the fatigue of you and the burden of you and your controversies?
Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
13 Set forth for you—men wise and discerning, and known to your tribes, —that I may appoint them to be heads over you.
Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
14 And ye answered me, —and said, Good, is the word which thou hast spoken to be done.
Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
15 So I took heads for your tribes wise men and known, and placed them as heads over you, captains of thousands, and captains of hundreds, and captains of fifties and captains of tens, and overseers for your tribes.
Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
16 And I charged your judges, at that time, saying, —Ye are to hear between your brethren and shall judge righteously, between each man and his brother and his sojourner.
Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
17 Ye shall not take note of faces in judgment—so the small as the great, shall ye hear, ye shall not shrink from the face of any man, for judgment, unto God, belongeth, —but the thing which is too hard for you, shall ye bring near unto me, and I will hear it.
Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
18 So I commanded you at that time all the things which ye should do.
Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
19 And when we brake up from Horeb, we came through all that great and terrible desert which ye saw, by way of the hill-country of the Amorites, as Yahweh our God commanded us, —and we entered in as far as Kadesh-barnea.
Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
20 Then said I unto you, —Ye are come in as far as the hill-country of the Amorites, which Yahweh our God, is giving unto us.
Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
21 See thou—Yahweh thy God hath set before thee the land, —go up—take possession as Yahweh the God of thy fathers hath spoken unto thee, do not fear, neither be dismayed.
Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
22 And ye came near unto me all of you, and said Let us send men before us, that they may search out for us the land, —and bring us back word, the way by which we must go up, and the cities whereinto we must enter,
Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
23 And the thing, was good in mine eyes, —so I took from among you twelve men, one man for each tribe.
Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
24 And they turned and went up the hill-country, and entered in as far as the ravine of Eshcol, and explored it.
Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
25 And they took in their hand of the fruit of the country, and bare it down unto us, and brought us back word, and said, Good is the land, which Yahweh our God, is giving unto us.
Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
26 Nevertheless ye were not willing to go up, —but rebelled against the bidding of Yahweh, your God;
Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
27 and murmured in your tents and said, Because Yahweh hated us, hath he brought us forth out of the land of Egypt, —to deliver us into the hand of the Amorites, to destroy us.
Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
28 Whither, are, we, to go up? Our own brethren, have made our heart melt saying—A people greater and taller than we, cities large and walled-up into the heavens, —yea, moreover sons of Anakim, have we seen there.
Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
29 Then I said unto you, —Ye must not tremble, nor be afraid of them:
Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
30 Yahweh your God, who is going before you, he, will fight for you, —according to all that he did with you in Egypt, before your eyes;
Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
31 also in the desert which thou hast seen, where Yahweh thy God carried thee as a man will carry his son, throughout all the way that ye journeyed, until ye entered as far as, this place.
na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
32 But in this thing, ye were putting no trust in Yahweh your God;
Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
33 who was going before you in the way—to search out for you a place, where ye might encamp, —in the fire by night, that ye might get sight of the way wherein ye should go, and in the cloud, by day.
ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
34 And Yahweh heard the voice of your words, —and was wroth and sware—saying:
Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
35 Surely, not one of these men, this wicked generation, —shall see the good land, which I sware to give unto your fathers:
“Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
36 saving Caleb son of Jephunneh, he, shall see it, and unto him, will I give the land through which he hath trodden, and unto his sons, —because he hath wholly followed Yahweh.
isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
37 Even with me, did Yahweh show himself angry, for your sakes, saying, —Even thou, shalt not enter therein.
Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
38 Joshua son of Nun, who standeth before thee, he, shall enter in thither, him, strengthen thou, for he, shall cause Israel to inherit it.
Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
39 And your little ones, of whom ye said they should become, a prey, and your sons who to-day know not good and evil, they, shall enter in thither, —and unto them, will I give it, and they, shall possess it.
Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
40 But as for you, turn ye, for your part, —and set forward towards the desert, by way of the Red Sea.
Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
41 Then responded ye and said unto me—We have sinned against Yahweh, We, ourselves, will go up, and fight, according to all that Yahweh our God hath commanded us. And when ye had girded on every man his weapons of war, ye foolishly went up towards the hill-country.
Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
42 Then said Yahweh unto me—Say unto them Ye shall not go up, nor fight, for I am not in your midst, —lest ye should be smitten before your enemies.
Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
43 So I spake unto you howbeit ye hearkened not, —but rebelled against the bidding of Yahweh, and presumptuously went up the hill-country.
Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
44 Then came forth the Amorites who were dwelling in that country, to meet you, and they chased you, as do, bees; and struck you down in Seir, as far as Hormah.
Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
45 So then ye returned and wept before Yahweh, —but Yahweh hearkened not unto your voice, nor gave ear unto you.
Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
46 And ye abode in Kadesh many days, —how many were the days that ye abode [there]!
Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.

< Deuteronomy 1 >